Nahitaji kujifunza kuongea Kiingereza kwa mtiririko mzuri

UNIQUEMAN1

JF-Expert Member
Mar 20, 2018
378
448
Wakuu vipi, hamjambo? Kama kichwa cha habari hapo juu kinavyojieleza naomba msaada wa namna ya kujua kuongea ung'eng'e vizuri mbele ya watu.

Nimesoma mpaka digrii ya kwanza lakini najiona fala tu, hasa linapokuja suala la kuwasilisha mada kwa lugha ya Kiingereza.

Niombe kwa yeyote mwenye linki online anisaidie. Wana Jf hawajawahi kushindwa kitu. Baada ya Jf kuniokoa na umauti nimetokea kuiamini mnoo.

Usishangae nina degree lkn bado sijaamini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu vipi, hamjambo? Kama kichwa cha habari hapo juu kinavyojieleza naomba msaada wa namna ya kujua kuongea ung'eng'e vizuri mbele ya watu. Nimesoma mpaka digrii ya kwanza lakini najiona fala tu, hasa linapokuja suala la kuwasilisha mada kwa lugha ya KIINGEREZA. Niombe kwa yeyote mwenye linki online anisaidie. Wana Jf hawajawahi kushindwa kitu. Baada ya Jf kuniokoa na umauti nimetokea kuiamini mnoo. Usishangae nina degree lkn bado sijaamini

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama upo Dar nenda britishcouncil

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tafuta tutorials hizi 》》 Effortless English: Learn to Speak English Like a Native

Kuna dvd. Video audio na pdf ..kwa maelekezo zaidi unaweza kuja ibobo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ukipata connection niunganishe na mimi, kitu cha kuongea kwa dakika moja kwenye kiswahili kwenye kingereza natumia dk hata kumi, yu know zinakuwa nyingi.
gharama za kukwepa kusoma english medium mbeleni huwa kubwa kupindukia
vitoto vya chekechea vya english medium vinaongea kingereza cha uhakika humu watu wazima wanahaha!!! wazazi pelekeni watoto english medium
 
gharama za kukwepa kusoma english medium mbeleni huwa kubwa kupindukia
vitoto vya chekechea vya english medium vinaongea kingereza cha uhakika humu watu wazima wanahaha!!! wazazi pelekeni watoto english medium
we unajua kila mtu anaishi kwa mboga saba, we mtoto wa masaki kaa kimya.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom