Nahitaji kufahamu hili suala kwenye masuala mazima ya taasisi ya Urais

mcTobby

JF-Expert Member
Feb 16, 2018
2,985
9,316
Salamu kwa wakubwa zangu na madogo zangu humu natumai nyote ni wazima wa afya.

Ni kweli kila mtu anajua Rais ndio kiongozi wa nchi na ana majukumu kadha wa kadha hususan katika kuleta maendeleo kwa kuzingatia sheria na kanuni za nchi husika.

Mimi ninachojua kwa mtu yeyote kuna tabia fulani fulani au tuseme kasumba lazima awe nazo hivyo kwa kuwa Rais naye ni mtu tu wa kawaida basi pasi na shaka kuna vijitabia lazima awe navyo haijalishi ni vijitabia vizuri au vibaya.

Ninachotaka kujua
1. Je, Rais yeyote anapokabidhiwa Ikulu (madaraka) kunakuwa na jopo la wataalamu wa masuala ya Saikolojia kwa ajili ya kumsaidia na kumshauri namna ya ku-behave mbele ya watu akiwa umma?

Nimeuliza hivi kwa sababu mtu anakuwa na vijitabia Mfano kuna tabia nyingine tuseme kuropoka , kujikuna sehemu za siri au kutema makohozi mbele za watu n.k.

2. Je, pia kuna mwalimu/mentor specifically anayemfundisha namna ya kuongea kwenye umma wa watu? Yaani aongee nini , wakati gani, mahali gani na kwa ajili ya nini?.

3. Unapokuwa Rais kuna tabia nyingine lazima uziache kutokana na hadhi ya cheo husika. Mfano umalaya,ulevi n.k je kuna kitengo maalumu cha kufuatilia tabia za Rais binafsi ambazo ni mbaya akiwa out of public eyes?

4. Na je kama hataki kuacha hivyo vijitabia, kuna mtu ambaye anaweza kumfokea huko Ikulu kwamba acha hizo tabia ili asijidhalilishe yeye mwenyewe na cheo kizima cha Urais?.

Natanguliza shukrani .
 
Mkuu navyoona nchi nyingi zilizoendelea, Rais ni muwakilishi tu wa wananchi, hivyo vitu vingi sana huwa anatayarishiwa including speech. lakini anaweza kufanya inavyompendeza.
 
Mimi nikiwa Rais sitawabagua na kuwachukia wanawake weusi kama Rais fulani wa nchi fulani ya dona kantri.
 
Mbona unauliza maswali maraisi sana?Kwani kila alieoa ameoa mke anaempenda?Unaelewa ya kwamba zaidi ya asilimia 70 ya ndoa watu wameoana kwa bahati mbaya na hawapendani?
Mkuu ni kwamba unachukulia vitu so serious, magu kuhusu wanawake weupe ni utani tu, we mtu alilazimika kuvuka maji kwenda kuposa afu useme ameoa kwa bahati mbaya, get serious ..
 
Mkuu ni kwamba unachukulia vitu so serious, magu kuhusu wanawake weupe ni utani tu, we mtu alilazimika kuvuka maji kwenda kuposa afu useme ameoa kwa bahati mbaya, get serious ..
Magufuli siyo raia wa kawaida.Yeye ni Rais wa nchi.Kila analofanya linafuatiliwa dunia nzima na watu tofauti tofauti pamoja na mashirika tofauti tofauti na kutafsiriwa kwa namna yake yenye athari kwa Tanzania.Kila analofanya linawakilisha watanzania.

Utani wa Rais unatakiwa kuwa tofauti na utani wa mtu wa kawaida.Utani wa Rais unatakiwa kuwa na vimelea vya kujenga zaidi na siyo vimelea vya kubomoa na ubaguzi.Magufuli hajui yote hayo.Magufuli hajui yote hayo kwa sababu ni country bumpkin.
 
Magufuli siyo raia wa kawaida.Yeye ni Rais wa nchi.Kila analofanya linafuatiliwa dunia nzima na watu tofauti tofauti pamoja na mashirika tofauti tofauti na kutafsiriwa kwa namna yake yenye athari kwa Tanzania.Kila analofanya linawakilisha watanzania.

Utani wa Rais unatakiwa kuwa tofauti na utani wa mtu wa kawaida.Utani wa Rais unatakiwa kuwa na vimelea vya kujenga zaidi na siyo vimelea vya kubomoa na ubaguzi.Magufuli hajui yote hayo.Magufuli hajui yote hayo kwa sababu ni country bumpkin.
Basi sawa! Ila mkuu we chama gani, maana isije ikawa unateseka ..
 
Inawezekana ni hivyo mkuu ,huoni ameacha yale mashati ya maua na suit oversize...
 
Mambo mengi yako under assumption kuwa by the time mtu anakuwa Rais keshaona Urais ukoje..wote wanakuwa mawaziri mda mrefu
 
Back
Top Bottom