mahingah
Senior Member
- Oct 4, 2016
- 199
- 275
Mimi ni kijana nimemaliza chuo mwaka huu ngazi ya Degree, katika makuzi yangu ya kimasomo kuanzia darasa la kwanza hadi la saba nimekulia kwa bibi yangu mzaa mama huko kijijini, wakati naandikishwa darasa la kwa bibi aliniandikisha la ukoo na la utotoni la upande wa mama.
Nilikuwa nakuja Dar mara moja kwa mwaka wakati wa likizo hata wazazi hawakulijua hili hata mimi niliona kawaida, nikamaliza hadi form four vizuri na kupangiwa shule ya A level Iringa, nilivyo maliza form six ndio nikatambua hili kuwa jina langu ni tofauti kabisa na alilo niandikisha bibi mzaa mama.
Wakati naanza kuomba chuo mwaka 2016 pamoja na mkopo nilitakiwa kuambatanisha cheti cha kuzaliwa, nikamfuata bibi akaniambia yeye cheti changu hana niwafuate wazazi wangu, nilivyompigia baba simu akasema kipo, nikaja Dar kuja kukichukua ili niambatanishe, nikakuta vitu viwili tofauti na jina langu, hata nilipoenda kanisani nikakuta cheti cha ubatizo kinalingana na cheti cha kuzaliwa lakini vyeti vya elimu vyote majina tofauti, kwa sababu nilikuwa na haraka ya chuo mzee akabidi aongee na RITA kuambia huyu kijana hana cheti na tukatoa kidogo nikapata cheti kipya chenye jina kama la vyeti,
Sasa nina vyeti viwili vya kuzaliwa, shida yangu nataka kutumia jina langu la kubatizwa, je ninaweza kubadili majina ya vyeti vyangu vyote vya elimu kwa ngazi niliofikia ya kielimu?
Naomba msaada kwa anayejua
Sent using Jamii Forums mobile app
Nilikuwa nakuja Dar mara moja kwa mwaka wakati wa likizo hata wazazi hawakulijua hili hata mimi niliona kawaida, nikamaliza hadi form four vizuri na kupangiwa shule ya A level Iringa, nilivyo maliza form six ndio nikatambua hili kuwa jina langu ni tofauti kabisa na alilo niandikisha bibi mzaa mama.
Wakati naanza kuomba chuo mwaka 2016 pamoja na mkopo nilitakiwa kuambatanisha cheti cha kuzaliwa, nikamfuata bibi akaniambia yeye cheti changu hana niwafuate wazazi wangu, nilivyompigia baba simu akasema kipo, nikaja Dar kuja kukichukua ili niambatanishe, nikakuta vitu viwili tofauti na jina langu, hata nilipoenda kanisani nikakuta cheti cha ubatizo kinalingana na cheti cha kuzaliwa lakini vyeti vya elimu vyote majina tofauti, kwa sababu nilikuwa na haraka ya chuo mzee akabidi aongee na RITA kuambia huyu kijana hana cheti na tukatoa kidogo nikapata cheti kipya chenye jina kama la vyeti,
Sasa nina vyeti viwili vya kuzaliwa, shida yangu nataka kutumia jina langu la kubatizwa, je ninaweza kubadili majina ya vyeti vyangu vyote vya elimu kwa ngazi niliofikia ya kielimu?
Naomba msaada kwa anayejua
Sent using Jamii Forums mobile app