Naombeni msaada wa ushaur ,mawazo na mafunzo ya ukalimani na tafsiri.naipenda sana kaz hii lakini.sina dira nianzie wap ili nipate kujua kaz hizi vzr.mm nimemakiza chuo kikuu ,katka taaluma ya kiswahili lunguistics
Nakushauri ungeenda kuwasiliana na watu wafanyao kazi katika taasisi kama BAKITA, TATAKI, TUKI, nk. Wangekusaidia zaidi. Mimi pia ninasoma English Linguistics (Bachelor), na hizo kozi ni miongoni mwa kozi ambazo ninazisoma, isipokuwa, tunazisoma kiujumla, na endapo mwanafunzi mwenyewe binafsi atataka kuiva katika upande fulani, basi hana budi kwenda kusoma upya, kiundani zaidi. PIA NENDA KAWAONE "TANZANIA TRANSLATORS ASSOCIATION / CHAMA CHA WAFASILI TANZANIA (CHAWATA/TTA). Watu hao natumaini watakuwa ni msaada mzuri kwako kwa kukupatia maelekezo sahihi yahusuyo taaluma hii.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.