Nahisi simpendi mke wangu

mkuu achana nae huyo gubegube la sivyo atakuletea kila aina ya nuksi na hata kukurestisha in peace. kama anataka mgawane mali mpe, we baki kuhudumia watoto. Mali kitu gan, na anafanya hivyo makusudi akitumia ngao ya watoto na mali kuwa hutakuwa na uthubutu wa kumuacha. Tena muache kwa herufi kubwa, msomi kama wewe mwenye shahada unapelekeshwaje na huyo leyman, unatuaibisha aisee.
 
ushirikina sio lazima kuroga basi kama ni hivo nayo hii ni aina yake ya ushirikina.duuh pole sana mkuu najua jinsi inavokuumiza hii.!! huyo mwanamke balaa.
Nimeshafikiria kuachana nae na hilo limekuwa wazo linalozunguuka kwenye kichwa changu kwa muda sasa, nimepoteza mapenzi na yeye kabisa. Naona kama tunaishi nyumba mbili tofauti na ninatamani akae mojawapo ya nyumba zetu na mimi nikae nyingine. Ukweli kuna kipindi nilimwambia achukue kila kitu aniache huru tu, kwani najua hana moyo wa kutafuta.

Nimejaribu kumpeleka shule nikijua tatizo litakuwa ujinga akaamua kuacha. Akawa ananilaumu kuwa simpendi kwa kuwa hana kazi nikamwambia afungue biashara nimpe mtaji akakataa. Kuna rafiki yangu amemfungulia duka mke wake aliniomba nimkutanishe mke wake na wangu ili amfundishe biashara, mke wangu akakataa.

Nikajaribu hata kumwambia afungue salon awe anasimamia akakataa. Kila kitu yeye ni mpinzani kwangu na kila ninachofanya yeye anapinga. Nikijaribu ku-support huduma za kijamii anakuja juu kama mbogo. Hakutaka hata nichangie harusi ya ndugu yangu na nilipochanga hakuhudhuria harusi ile. Naishi maisha ya kujitenga na jamii mpaka najiona mpweke. Nimempa hela akafungue akaunti benki ili niwe namuwekea hela ya matumizi huko lakini fomu zina miaka miwili ndani hazijajazwa.
 
Nimeshafikiria kuachana nae na hilo limekuwa wazo linalozunguuka kwenye kichwa changu kwa muda sasa, nimepoteza mapenzi na yeye kabisa. Naona kama tunaishi nyumba mbili tofauti na ninatamani akae mojawapo ya nyumba zetu na mimi nikae nyingine. Ukweli kuna kipindi nilimwambia achukue kila kitu aniache huru tu, kwani najua hana moyo wa kutafuta.

Nimejaribu kumpeleka shule nikijua tatizo litakuwa ujinga akaamua kuacha. Akawa ananilaumu kuwa simpendi kwa kuwa hana kazi nikamwambia afungue biashara nimpe mtaji akakataa. Kuna rafiki yangu amemfungulia duka mke wake aliniomba nimkutanishe mke wake na wangu ili amfundishe biashara, mke wangu akakataa.

Nikajaribu hata kumwambia afungue salon awe anasimamia akakataa. Kila kitu yeye ni mpinzani kwangu na kila ninachofanya yeye anapinga. Nikijaribu ku-support huduma za kijamii anakuja juu kama mbogo. Hakutaka hata nichangie harusi ya ndugu yangu na nilipochanga hakuhudhuria harusi ile. Naishi maisha ya kujitenga na jamii mpaka najiona mpweke. Nimempa hela akafungue akaunti benki ili niwe namuwekea hela ya matumizi huko lakini fomu zina miaka miwili ndani hazijajazwa.

pole ila panga muda wa kumpa ujumbe wake wa kumuacha. Ukishafanikisha usimuongelee vibaya itakaa sana kichwani mwako na itachukua muda kuanza mahusiano mapya. Pia uwwe na mkakati mtaleje watoto. So sorry lakini maisha ni mafupi sana na we live only once. Asikustrees utapata mjinga mwingine lakini atakuja na ujinga mpya sio huo.
 
pole ila panga muda wa kumpa ujumbe wake wa kumuacha. Ukishafanikisha usimuongelee vibaya itakaa sana kichwani mwako na itachukua muda kuanza mahusiano mapya. Pia uwwe na mkakati mtaleje watoto. So sorry lakini maisha ni mafupi sana na we live only once. Asikustrees utapata mjinga mwingine lakini atakuja na ujinga mpya sio huo.

Ikitokea kuachana nitatafuta mwerevu na si mjinga.
 
Mkuu ww ndiye mwenye maamuzi hebu tuliza akili kwanza af fanya maamuzi ya busara bila kuwa na papara!!!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Pole Kwa Matatzo
Japo Ni Maelezo Ya Pande Moja
(hujaeleza Mapungufu Yako).
Najua Si Rahisi Kumuacha Kisa Unahofu Kugawana Mali Na Ukiangalia Mcharuko Wake Unahisi Bado Ataendelea Kukusumbua Hata Ukimuacha Na Kuoa Mwingne.
Nikuulize Hivi Kuna Maana Ya Maisha Zaidi Ya Furaha?
Umesoma,unafanyakazi Ulioa Ili Uwe Na Furaha, Na Nadhan Hukufunga Nae Ndoa Kwa Vile Hukumuamin,umejitahidi Kila Namna Abadilike Wapi, Je Unataka Akuuwe?
Ukisha Kufa Watoto Wataishije Wakat Mke Mwenyewe Haelewan Na Nduguzo Wala Hajui Kutafuta Hela.
Wewe Mwanaume Bwn Acha Kumuogopa, Kama Unashindwa Kumuacha Nenda Kwa Rafiki Yako Uishi Huko Yeye Asijue, Nini Mali Ukifa? Ila Usitafute Mchepuko Maana Atasimamia Humo,
 
Dah! Pole sana Mkuu, wewe ni mvumilivu sana kwa wengi ndoa kama hii ingeshavunjika siku nyingi.
 
Mkuu pole sana,,,, kumbe tupo wengi mno, na kila mmoja ana style yake ya mgogoro....hapa utapata ushauri, ila wewe ndie muamuzi wa pambano......hivi Mungu alituumba tuteseke? haiji akilini wengine wakisema ni changamoto za ndoa,,,, changamoto gani za miaka mpaka 5 na kuendelea......jipange kuwatunza wanao, maisha hayasimami.....gud luck...
 
mmmmhhhhhh kweli kazi ipo..........
1. mlishawai kupendana?
2. mlianzanaje anzanaje au makubaliano yenu yalikuwa ni nini coz nahisi ulishabugi kuanzia mwanzo?
3. uwe makini coz mwanamke akikuchukia kiasi hicho ni hatari sana.
4. tafuteni wazee wa ukoo muyaongelee.
 
Mimi ni Mkristo na kutokana na mazingira ya maisha ninaoishi nieshindwa kutangaza ndoa. Kwa hiyo naishi maisha ya kujifichaficha kanisani. Natoa sadaka, zaka na michango kwa kadri Mungu alivyonijlia lakini sishiriki meza ya Bwana. Inaniuma sana.

Kaka unahimtaji Mungu sana sasa,endelea sana na maombi,ndio iwe silaha yako ya kuzipinga hila za shetani.
 
Nilifanikiwa kuoa miaka kumi iliyopita na katika maisha yetu ya wawili tumefanikiwa kupata watoto watatu, wote wa kiume.

Migogoro katika maisha yetu ilianza mara baada ya kuanza kuishi pamoja. Mimi na mke wangu tulianza kuishi pamoja kabla ya kufunga ndoa. Binafsi nilimpenda sana na nilitamani kumfanyia kila ninaloweza ili awe na amani na furaha.

Kiukweli tulianza kuishi kwa amani na furaha mpaka pale mke wangu huyu alipoanza chokochoko dhidi ya mama yangu. Alianza kuniambia kuwa mama yangu hampendi na wala alikuwa hataki aolewe na mimi na kisha akaanza kwashambulia wifi zake. Nilijiuliza maswali mengi na baade nikagundua kuwa ni maneno ya kutunga.

Kilichonifanya niamini ni baada ya kukumbuka kwamba mimi na mke wangu tumechukuana kwa maamuzi yetu binafsi (mimi siwashirikishi wazazi) na pili ni kwamba wazazi wangu wanaishi mbali na anapoishi huyo mwanamke, na tatu hapajawahi kuwa na mahusiano yoyote na wala mawasiliano yoyote baina ya familia hizi mbili.

Hapo nikaanza kumuona mke wangu kama mtu wa shari. Mke wangu nilimtoa bara kuja kuishi naye Dar es Salaam na nilitamani kuja kufunga nae ndoa.

Baada ya kuishi naye kwa mwaka mmoja jijini Dar es Salaam na tukiwa tumefanikiwa kupata mtoto mmoja tulipanga safari ya kwenda kijijini kuwasalimia wazazi pamoja na kujitambulisha kwao. Ilipofika Jumapili nilimwambia tutaenda kanisani na tutajitambulisha tukiwa pamoja ili kanisa litupokee na baadae tuanze mchakato wa ndoa.

Tulikubaliana kwa ajili ya hilo ila tulipofika kanisani kabla ya kuingia kwenye ibada huyu mwanamke akaniambia nisimtambulishe kanisani na wala nisijaribu kumtaja. Nilipatwa na hasira iliyoharibu ibada yangu na tuliporudi nyumbani ikawa ni ugomvi tu.

Mimi ni msomi mwenye digrii na mke wangu ni mama wa nyumbani. Niliamua kuoa mama wa nyumbani kutokana na nature ya kazi yangu inayonihitaji kuwa mbali na nyumbani kwa kipindi kirefu nikiwa kwenye camp.

Maisha yaliendelea hukutukiwa na migogoro isiyoisha kila mara akinituhmu kwa mambo mbalimbali, mara nyingine alinituhumu kuwa nina mke mwingine na nimemjengea nyumba na mara nyingine ananituhumu kuwa namuua kwa UKIMWI.

Sikujisikia vizuri na mara kwa mara nilikuwa naenda kupima ili awe na amani na kuna kipindi nilikuwa namchukua kwenda kupima ila yeye anachukua vipimo vingine na kukataa kupima UKIMWI.

Mimi huwa napima na majibu namuonyesha. Katika hali hizo nilijikuta maisha yangu nyumbani yanakosa furaha na mara kwa mara ni mizozo mara huu mara ule. Hata tendo la ndoa ilikuwa nadra kulipata kwa hiari na wakati mwingine nahisi ana mwanamume mwingine anayemzuzua.

Mbali na kuwa mbali kwa muda mrefu, muda mfupi tunaopata kuwa pamoja unakuwa na majonzi tele. Kuna kipindi nilisafiri kwa wiki sita 6 na niliporudi nikadhani mwenzangu amenikumbuka ila nilichokiona usiku ni kibaya. Tulienda kulala na alipojilaza tu akavunga amesinzia usingiz mzito, nilijaribu kumuamsha ila akavunga kufa. Nilijaribu kulala ila sikuweza kupata usingizi nikaamua kwenda kulala kwenye sofa sebuleni ili nijisikie niko safarini.

Kuna kipindi nilipoteza kazi akaniambia ameonyeshwa kuwa hayo ni mapigo na wala sitakaa nipate kazi tena. Wakati huo nilikuwa nimepata kiwanja hapa Dar es Salaam na nikiwa najipanga kuanza ujenzi.

Nilikaa mtaani miezi miwili na baadae nikapata kazi mpya. Baaada ya kupata nilimwambia nataka kuanza ujenzi, yeye aliniambia ni vema nikaacha kujenga kwani nitapata hasara.

Nilimuuliza hasara gani nitapata akasema hiyo nyumba itakuja kuuzwa ili tugawane hela. Mi nilimambia simsikilii yeye ila naangalia mahitaiji ya watoto wangu kwamba wanatakiwa kuwa na nyumbani kwao.

Nilibahatika pia kupata gari na siku moja nikiwa safarini peke yangu kwenye gari nilipata ajali ya kugongwa na gari nyingine. Bahati nzuri ni gari iliharibika ila mimi nilibaki salama.

Baada ya tukio hilo siku moja tukiwa kwenye mzozo alinitolea neno kali kuwa nilipata ajali kwa maombi yake. Anadai aliomba nikipakia mwanamke kwenye gari yangu nipate ajali. Nilijisikia kumrukia nimle nyama mbichi lakini nikajizuia.

Mizozo imekuwa mingi mpaka najisikia kumtapika, sina amani wala furaha niwapo

Dunia ni yako na chaguo ni lako.
 
Acha kupotosha au hauijui biblia, talaka ipo kwa Wakristo.

Very true Matola
Watu tunapotoshana kuambiana pingu za maisha lakini in reality the new law kept it hakuna maswala ya kujifunga na mtu wa hivyo maana she will lead him to aldetary ambayo ni amoung reason to christian divorces
Alaf hawa wana presumption of marriage lakini sio wana ndoa. . . . .
 
Last edited by a moderator:
Nilijaribu kumpeleka kwao lakini hata mwezi haukuisha akarudi na fujo zake. Nikimsihi kubadilika yeye anasisitiza juu ya mali. Kwa hiyo kutafuta kwangu inakuwa mwiba kwangu.

Mali zangu zinataka kunitoa roho mwenyewe kwa kujaribu kuvumilia ili niokoe mali zangu ninazopata kwa shida. Nimejenga nyumba nzuri ila nalala kama mara sita kwa mwezi, muda wote niko field kutafuta, wanaojivunia nilicholeta hawataki kuuona mzigo niliobeba. Na kwa tabia yangu kila nikija lazima nibebe kifurushi lakini kuna muda huwa sipokelewi.

Kuna kipindi nilikuja Dar na samaki kutoka Mwanza nikatamani zingeibiwa maana baada ya kushuka kwenye taxi nilibeba mizigo yangu watu wamesimama kwenye nyumba wananiangalia bila hata kuja kunipokea. Niliwaza sana nikasema kwa sauti nimepotea nyumba???

wee jamaa una roho ngumu sana....

Ila watu kama wewe lazima wawepo ili dunia izunguke na equation iwe balanced...

In short,unatudhalilisha wanaume wenzio...tena sana....tena unaidhalilisha taaluma yako pia...mimi ndo maana niligoma kabisa kuoa mwanamke mwenye elimu fupi....hawanaga akili kabisa

Simama kama mwanaume.....nahisi amekuloga tayari,ila waweza kujinasua....Pangani,Kigoma,Rufiji et all pako wazi muda wote,....waweza kwend kuokoa maisha yako mapema....

BTW mimi ningekuwa wewe,ningemuua huyo mwanamke immediately.....tena kistaarabu kabisa(kama livyouliwa sheikh Ilunga)....make hapa nakuhesabia tu.....huyo mwanamama atakupoteza wakati wowote....
Stay tuned,ila kama unapenda kumuona bado anapumua it means wewe utapotea....ili usipoteza vyote,andika urithi kwa wanao mapema,ili hata ukifa,wanao wapate pa kuanzia,otherwise....you are going to lose everything,just everything.....

The Magnificent,
Under the sun.
 
kwakifupi kuoana nikufanana huyo hamfanani ndio maana mzozo kila leo, sasa ili usife na presha au asije akakuekea sumu kwenye chakula au akakuendea kwa waganga wakienyeji bora ugawe talaka mapema kabla madhara makubwa hayajatokea, bora utafute binti mwingine uoe kuliko kuishi mtego Kama huyo
 
Kaka Naomba kwanza nikupe pole nyingi kwa maisha unayopitia. Naomba nikushauri machache nawe unaweza kuona kama kuna baadhi yanafaa ·

Mkeo hajaridhia mahusiano yenu: Bila mume na mke wote kuona kuwa ujenzi wa mahusiano yetu ni juhudi zetu za dhati sisi wawili hakuna ndoa/mapenzi. Methali ya kale ya waingereza inasema “it takes two to tangle” imeweka wazi kuwa jambo jema lazima lihuishe effort ya watu wawili. Pengine hajatambua kuwa ndoa ni wawili , siri ni zenu na hajatambua nafasi yake kama mshauri mkuu. Na tukigeuza shilingi labda humpi nafasi ya kuona nafasi yake kwako. Kwanza una moyo sana wa kuishi kwa uvumilivu, ni wanaume wachache sana wanaoweza kuvumilia wanawake wenye viburi kama mkeo. Ndio maana biblia imesema ishi na mwanamke kwa akili maana ni viumbe wasiotabirika. Ila kwa kiasi Fulani baadhi ya tabia umezijenga mwenyewe, mfano siku ya mwanzo kabisa aliposema usinitambulishe kanisani-that was the very first warning sign . Kwangu mini ningehypothesize mambo haya o Ana mtu wake wa zamani, hataki kuonyesha kuwa amemuacha o Ana dark spirits ambazo kudeclare kutengana navyo mbele ya altare ni hatari sana sana o Ana personal greedy nature ambayo inamwambia huyu bado hastahili kuwa mume hivyo anajishikiza tu—kuna watu wana roho hizi hadi wanazeeka bado hawaja “own “ ile hali ya kuwa wanandoa yaani wana hisia kuwa they are about to leave.

·
Mkeo hana trust na wewe: Hivi mtu unayempenda unaanzaje kumtuhumu kuwa ataleta ukimwi? How dare she? Napo hapa kaka naona umejenga kitu kibaya kwa kumuendekeza na maneno yake makali , anapoanza kulalamika mambo yasiyokuwa na ushahidi wala dalili hiyo inaashiria haya; o Yeye si Mwaminifu na hajawahi kuwa mwaminifu. Wanasaikolojia wanasema “what you say is a refection of yourself” mfano kuna watu watatu wamepita sehemu wakamwona mwanamke amesimama pembeni ya mti wa kivuli, mtu wa kwanza akasema huyu mwanadada atakuwa changudoa anasubiri mteja wake, wa pili akasema jamani mnajua siku hizi majambazi na matapeli ni kina mama , ona kama huyu ametega mingo amwingize mtu chaka, mtu wa tatu akasema jamani dunia hii bila sala za kina mama tungekwisha ona huyu mama anasubiri basi awahi maombi. Wote wanatoa conclusion ya tukio based on what they have either done, seen , or think. Hivyo ni dhahiri mkeo si mwaminifu na anaonyesha chembe hizo kwa maneno yake. Mfano mwingine ni mtu asiye na amani na mwenzi wake na kupekua simu , barua pepe , kompyuta kisa ana hofu kuwa huyu ni mzinzi, tabia hii ni reflection kuwa either yeye ni mzinzi na anataka kuprove kama mwenzie naye yupo hivyo au ana insecurities . Kama unapenda mtu haumchonoi na kumuwazia vibaya bali mnaongea kwa upendo juu ya nini unaweza kuwa wasiwasi wako mwenzio anapokuwa mbali. Imagine mpo mbali mbali mwenzio hasemi kama anakumis , hasemi hofu ya yeye kuwa mpweke , hakusisitizi kujulinda (japo ni obvious kuwa kujilinda ni vema ila ktk mapenzi watu hukumbushana) ila unaporudi tu nyumbani ni kelele au kupekuliwa kuwa umedanganya? ni dhana inayomfanya mtu asiamini chochote juu yako.

Upendo umekufa kwake: Kuna methali inasema “To be trusted is a greater compliment than to be loved” yaani msingi mkuu wa upendo ni Imani. Mwenzio amesafiri unaamini kuwa yupo kazini, yupo salama , ananipenda na tunajenga maisha . Upendo unapotoka ndipo tunapoanza kusema na kuhisi aah leo ana mwanamke , leo ana huyu. ·

Mkeo ni Mchoyo: Mnapoingia kwenye ndoa na Mmoja anawaza mali saa zote na jinsi gani mkiachana mtagawana ni dalili ya hatari sana . Mali ni matokeo ya upendo na kazi ya wawili. Na mali haiwezi kuleta faraja pasipo na upendo. Nakusihi uwe makini na mustakabali wa watoto wako , mfano elimu; Pindi mkiachana (hatuombei) anaweza akauza kila kitu na watoto wakakosa hela ya kusoma. Unaweza kuoana na mwanasheria akakushauri jinsi ya kuandika will ili tu iwe kitu kinachotambulika kisheria in case of anything.
·

Your health and life is at great risk: Mtu anayeweza kukwambia kwa kinya kuwa nakuombea mabaya ni Zaidi ya shetani. Mtu wa hivi ana visasi na vinyongo na haoni tabu kukuua. Naona umepuuzia kauli nyingi sana ila kwa mtiririko wa simulizi hizi ungeweza kupeleka haya kwa wazee wa kanisa au vyombo vya sheria. Tumeshuhidia kina baba wengi wakipewa sumu au kuuliwa kisa mali na chuki . Thus be extra careful and don’t neglect any word or gesture. ·

Wrong company of friends:
Mkeo ana washauri wabaya, marafiki wabaya na amewakumbatia. Kwa kuwa muda mwingi upon je kikazi na kwa kuwa yeye yupo idle , anatumia muda huo kusengenyana. Remember “an idle’s mind is a devils workshop”.

Baada ya yote haya tafakari kipi bora: Lying to the world that you are happily married and killing your soul or facing the truth and save your soul. Its never too late to make a decision. Biblia hairuhusu divorce ila inapofika afya na maisha yapo hatarini –then u need to decide na ushukuru hamjafunga “Pinngu” maana in this case ingekuwa real Pingu.

May God guide u accordingly.
 
Nimeshafikiria kuachana nae na hilo limekuwa wazo linalozunguuka kwenye kichwa changu kwa muda sasa, nimepoteza mapenzi na yeye kabisa. Naona kama tunaishi nyumba mbili tofauti na ninatamani akae mojawapo ya nyumba zetu na mimi nikae nyingine. Ukweli kuna kipindi nilimwambia achukue kila kitu aniache huru tu, kwani najua hana moyo wa kutafuta.

Nimejaribu kumpeleka shule nikijua tatizo litakuwa ujinga akaamua kuacha. Akawa ananilaumu kuwa simpendi kwa kuwa hana kazi nikamwambia afungue biashara nimpe mtaji akakataa. Kuna rafiki yangu amemfungulia duka mke wake aliniomba nimkutanishe mke wake na wangu ili amfundishe biashara, mke wangu akakataa.

Nikajaribu hata kumwambia afungue salon awe anasimamia akakataa. Kila kitu yeye ni mpinzani kwangu na kila ninachofanya yeye anapinga. Nikijaribu ku-support huduma za kijamii anakuja juu kama mbogo. Hakutaka hata nichangie harusi ya ndugu yangu na nilipochanga hakuhudhuria harusi ile. Naishi maisha ya kujitenga na jamii mpaka najiona mpweke. Nimempa hela akafungue akaunti benki ili niwe namuwekea hela ya matumizi huko lakini fomu zina miaka miwili ndani hazijajazwa.

yeleuwiiiiiiiiiiiiiiiiii

mimi nisingewezaaaa......kwa nn sikupata mke wa namna hii pengine ningekua nisharudi ujanani ubachelani napiga gambe sinza...kwani umezaliwa nae mkuu?? muache harakaaa unaishi na jinii...harakaa kabla hajakuuuaaa mkuu wangu kaka yangu mpendwa ilo ni jini narudia tenaaa......liache harkaaaaa
 
Acha kumtisha mwenzio. Amuache kabisa huyo mwanamke na asijichanganye zaidi kwa kuokoka au kuingia kwenye dini kupata suluhisho
Kwani nimemlazimisha??? kwanza wewe una watoto? mme unaye? kama ni ndiyo hebu jaribu kwanza kuachana na mmeo halafu chukua watoto hao ulionao ukaolewe na mme mwingine unayedhani(huna uhakika) hana shida kama hutachanganyikiwa kuliko huyu kaka. Suluhisho ni YESU tu. kuokoa ndicho kilichomleta la sivyo asingekuwa na sababu ya kuja, hata wewe anakuhitaji ili uwe na akili njema zaidi.
 
mmmmhhhhhh kweli kazi ipo..........
1. mlishawai kupendana?
2. mlianzanaje anzanaje au makubaliano yenu yalikuwa ni nini coz nahisi ulishabugi kuanzia mwanzo?
3. uwe makini coz mwanamke akikuchukia kiasi hicho ni hatari sana.
4. tafuteni wazee wa ukoo muyaongelee.

Ni stori ndefu nikisimulia jinsi tulivyoanzana, ila nahisi kuna kitu kilitumika kuingia kwenye dimbwi hili. Tangu nasoma O-Level nilikuwa nimejiwekea vigezo vya nani atakuwa mke wangu. Mpaka nikaviandika kwenye daftari. Juzi kati nikiwa nasoma kwenye library yangu nikakuta vigezo hivyo hivyo niliviandika nikiwa Chuo Kikuu, ia kilichotkea huwezi amini, uzuri wa sura na vingne vilinchaganya ama kulikuwa na nguvu ya ziada ya kunitoa akili.
Sijui kama hao wazee wataweza kubadilisha maisha ya huyu mwanamke kwani tumeshaongea na mama yake mara nyingi na kuahidiwa atabdilika. Lakini mpaka leo nasubiria mabadliko siyaoni. Mpaka hapa tunapozngumza ingawa mke wangu ni mama wanyumbani na tuna mfanyakazi nguo nanyosha mwenyewe kwa miaka yote. Taa ikiungua niko safarini nasubiriwa nije nibadili mwenyewe. Muda si mrfu nimepigiwa simu kuwa umeme umeisha nyumbani. Ninunue ilhali niko mikoani mingine yeye yuko ndani. Hela ninayomwachia ni nyingi nikisema hapa watu watadhan nafanya promo.
 
Back
Top Bottom