Nahisi mke wangu anani-cheat, nifanye nini kumkamata?

He! Jamani sura ya makenikia si hii hapo asee🤣🤣🤣.Makenikia alishafumua mbususu ya mkeo kitambo tu tena alikuwa akifuliwa adi hizo gwanda za kimakenikia.
 
Katika kitu sifanyi ni kukagua simu ya mtu wang. Mapenz moto moto mapresha ya nn. Yan nkshika simu jua nataka kumuacha
 
Hellow, Habari Wana JF. Sorry Mimi sio muandishi mzuri hua nachanganya capital letters katikati,

As normal Jf imekuwa na member bright sana ambao wengine washachomwa mishale mingi sana kwenye maisha ya mahusiano hivyo kuwafanya kuwa watu wenye experience kubwa katika kutatua changamoto yoyote ya kimahusiano inayowahusu kwa kutumia busara zaidi bila shari au hata kujaribu kuwashauri wale wenye uhitaji wa ushauri kutoka kwao ikiwemo mimi pia ambae nahisi bado kabisa ndo kama nachipukia kwenye hii kitu inayoitwa mahusiano ya mapenzi (I'm 21yrs).

Let's go to the point
Naishi na mwanamke huu mwaka wa pili Sasa(pika pakua) jinsi tulivyoanza kuishi nadhani Leo sio siku ya special ya kuelezea hilo, ila katika safari ya miaka hio miwili nimeshakutana na changamoto ya usaliti Kutoka kwake, Mwanzoni nilikuwa nikifuma messages za kunicheat katika cm yake alikuwa ni mtu anaejua kupoteza ushahudi sana, kwa mfano; Kuna siku nilifuma messages zake za WhatsApp akichart na jamaa fulani ambae kiukweli ndo kama alikuwa akimtongoza(it's normal kwa wanawake kutongozwa) ila kilichoniuma katika conversation yao alionekana kukubali Ile appointment ya jamaa(he! jamani hapa si alikuwa anaenda kuliwa kabisa???) kile kitu kilifanya nikapanick sana coz Ukizingatia ndo first time Dah!

Nilijikaza nikarudisha simu nikajikausha kama sijaona chochote aliporudi kufanya manunuzi ya vitu dukani akapika fresh tukaanza kula, Kidume nilijikaza nikawa najitia kula lakini chakula ngumu kumeza wakati huo mwenzangu anabugia matonge Tena na simu yake kama anachat hivi na katabasam kwa mbaliiii nikaona eh! uvumilivu unanishinda nikawaza ngoja nakiamsha hapahapa kama mbwai iwe mbwai.

Mimi; Mary em Simu yako
(akaniangalia kisha akafanya kama anasikitika fulani na kucheka kama dharau hivi Kisha akanipa Simu niliporudi kuzicheki zile messages ambazo ndo kama chanzo changu cha ushahidi wa kunikingia ubavu bwanae! sikuona chochote zilikuwa deleted tayari (Hawa viumbe ni waajabu sana yani wapo very sharp. Sasa sijui alijuaje, na kumbe ndo maana hakusita kunipa simu yake) Ile kitu ilinikasirisha sana na ikanifanya nione kwamba kumbe mwanamke ninaeishi nae ni hatari hivi, Sikuonesha reaction yoyote nilijifanya tu kama nilitaka simu yake kwa lengo la kucaluculate kitu tu Ila roho haikutulia kabisa na chakula nilishindwa kukila kabisa.

Mara ya pili nilihisi tu kwamba kuna jamaa jirani yangu ambae ni fundi makenika kama vile yupo kwenye root za kumnyemelea mwanamke ambae ninaishi nae kama mke na mume, Nilihisi hivyo kwa kuwa alikuwa ni jamaa fulani kama anajishtukia sana tukionana macho kwa macho basi nikasema ngoja nifuatilie bhana we! kwani nilikosea basi?

Ni kitendo cha kucheki simu ya mwanamke nikaona kwenye call history Kuna namba inaonekana kumpigia sana wife ila haipo saved then ukiangalia kwenye history inaonekana wanaongea muda mrefu sana imagine 6dk-10dk alafu Namba ya wazazi wake naijua na ninayo pia, Ya Ndugu zake karibu wote ninayo na pia sio mwanamke wa kukaa na namba ambayo haipo saved kwenye Simu yake basi nikajiuliza huyu ni Nani anaongea nae kwa muda mrefu hivi? (Kumbuka wife ni mtu tunakutana jioni tu maana kutwa yupo kazini kwake na Mimi nipo kazini kwangu) nikachukua Ile namba nikaisave kwangu then nikaenda kuichungulia whatsapp He! jamani sura ya makenikia si hii hapo asee safari hii sikulaza damu nikakiamsha sana Ila baadae mwanamke alikiri kuwa jamaa ndo alikuwa akimtongoza lakini hakumkubali,

Pale nikakosa nguvu ya kumuwajibisha kwa sababu sikuwa na ushahidi kama je, mwanamke alimkubalia??? maana ni kweli wanawake kutongozwa ni normal tu Yule makenika Nakumbuka siku iliyofuata nilipoona nae jicho kwa jicho kiukweli yule jamaa najisi alfahamu kabisa kwamba Mimi Kuna kitu nimegundua baada ya pale nahisi waliambiana nimewaahtukia yule makenika sikuwahi kumuona tena (Aisee Hawa wanawake kuwakamata vizuri hadi akose pa kutokea ni kazi ngumu sana. hua nawakubaligi sana Wanaume wanaowafumania wake zao na ushahidi wa kutosha Aisee Hawa watu wanakuwaga maginious sana, Ukiona mwanaume kamfumania mwanamke ata akichukua maamuzi mabaya yaheshimu sana maana Hawa viumbe kuwafumania inahitajika akili iliyotulia hasa kwa wale watu wenye kuhitaji ushahidi wa kutosha) Tuachane na Hilo maana Hilo lilipita salama.

Tuje tukio Hili lililopelekea kuandika huu uzi, ni Kitu kama Cha week mbili zilizopita Kutoka Leo wife ameniambia kapanda cheo kidogo kazini kawa supervisor na kutokana na Hilo atakuwa analazimika kuchelewa kutoka kazini nikajibu "Alhamdulillah mke wangu MUNGU anasikia maombi yetu hongera sana) basi saa 3 usiku ndo akaanza kurudi nyumbani, Sio siri inaboa sana lakini no way ili tutimize malengo kila mmoja yabidi achacharike.

Sasa jana muda yeye kashalala (Mimi hua nachelewa kulala sana maana napenda kuutumia usiku kupitia maswala ya biashara yangu) sijui kilinisibu nini nikajikuta nimeshika simu yake ambayo ni ndogo nikajikuta nimeenda sehemu ya kuhifadhi messages (inbox) ndipo nikakutana na ujumbe wa jamaa kamsave "Robert" umetumwa neno My love,, picha nitakuwekea hapo chini, Aisee huyu mwanamke hajawahi kunifuma mimi maana Sina tabia za kimalaya mbona aisee ni mimi Kila siku tu ndo naumia??? Basi kukusanya data kamili nikaanza kutafuta muendelezo, Kiukweli jamaa inaonekana ndo kama wameanzaanza

Nikapata kwenye call history nikakuta jamaa ametoka kuwasiliana nae ahsubh na wametumia sec kama 60 na mchana kama dk 2 hivi, nikachukua Ile namba nikaenda kucheki profile ya WhatsApp naona jamaa sio asili ya kitanzania, Anaonekana kama muhindi fulani hivi na pia nikagundua wanafanya kazi kampuni moja na kimuonekano Anaonekana ni boss nilijua Hilo baada ya kuona kitambulisho cha jamaa kipo the same na Cha wife, Sasa kiukweli I'm tired of this shit,

Nataka nipate ushahidi wa kutosha kabisa ili siku namwambia it's over iwe inamake sense maana hawachelewi kusema nilimchoka tu, Please ambae anaejua jinsi ya mimi kufanya ili ikiwezekana nimfumanie vizuri hadi achanganyikiwe maana anajionaga ni mtu innocent sana alafu mjuaji sana huyu mwanamke kumbe ana tabia zake mbaya za chinichini, Sikatai mwanamke kutongoza kawaida ila Kukubali je, Mtu humtaki inasave namba yake ya Nini? unaahundwa hata kuiblock basi sawa ishieni kwenye chatting pekee he! call history inaonekana mnaongea Tena sana tu, Au ndo aliempa cheo? Au navyoniambia anachelewa kwaajili ya kazi usikute ndo muda wao wa kuenjoy?

Please kama Kuna mtu wa kunisaidia njia ya kumfunia huyu mwanamke naomba anisaidie tafadhali, Nimeacha na sina wala kushobokea mwanamke mwingine kwaajili yake, Inaniuma sana kwa mwanaume kujinyima kama hivi kwaajili ya pimbi kama huyu Inakuwaga na maumivu eti wazee Bora ningekuwa Malaya.

View attachment 1921712
Bwana mdogo kifua chako bado cha plastic, bado haujawa na uhimilivu katika mapenzi. Na huyo binti ameshakujua unampenda ndo maana yuko hivo, usiyape nafasi sana mapenzi had ukae unschunguza simu ya mwenzi wako.
 
Mwambie aache kazi mdogo wangu...

Kuna jamaa yangu mwingine ameoa nesi aisee,majanga yani yako yana afadhari..
 
Hapa tatizo ni umri wenu haukufaa kuwa kwenye ndoa ungesubiri ukiwa 24. Ona sasa unatafuta sababu ya kumfumania wakati sababa unazo.

Uliona sms za mapenzi alivyorudi akafuta unataka nini tena. Hapo tayari ilionyesha anakazwa.

Hata uisihangaike kutafuta fumanizi wakati akili yako imeshaamua kumuacha. Sepa kiroho safi sio lazima mtengeneze mazingira ya kukatana mapanga. Angalia utarudi huna macho.
 
Ukimchunguza Sana Bata hakika hutoweza kumla, ktk ulimwengu huu wa fujo na taabu hakika Mambo yote ni madogo isipokua uhai tulio nao nakifo kilicho mbeleyetu, zungumzeni kwa upendo, busara na amani na hakika kila Jambo litakwisha, waswahili tunasema Tembo hashindwi na mkonga wake.
 
kwanza hongera miaka 21 na umeweza kuweka maneno yenye mpangilio wa mawazo katika maandishi japokuwa ni statment ila nimeona unakitu special, kitaalamu huwa hamna ushauri wa kisaikolojia katika mahusiano huwa mshauri anakupa nafasi ya kufuata moyo wako unavyotaka, ila kwa upande wangu ni mapema sana kwa umri ulionao kuvumilia mambo yanayokuzidi umri, achana nae hakuna haja ya kutaka ajiridhishe yy kwamba umeona ile hali ukimwambia ukweli ataamini umeona na umetambua
 
Back
Top Bottom