James Hadley Chase
JF-Expert Member
- Mar 25, 2020
- 1,565
- 2,638
Mpaka sasa nina miaka 25 ndio kwanza nipo Diploma mwaka wa kwanza Semester ya 2 inaanza tarehe 4 Aprili 2022. Bado nakaa na kaka yangu japo naye ana familia yake.
Najihisi kama nimechelewa kuanza maisha vile, nimesoma kwa kuungaunga tu, washkaji na rafiki zangu niliomaliza nao sekondari mwaka 2014 wengi wao wameoa, wengine washaolewa.
Yaani nikionana nao au kupishana nao njiani ni aibu tu, bora tuishie kuchati tu kupitia aidha sms, WhatsApp, Facebook. Nipo tu kama digidigi vile sina hili wala lile.
Hata akiba sina, siugui ovyoovyo. Siku nikitimuliwa home sijui itakuwaje. Japo Sir God analinda ile mbaya.
Najihisi kama nimechelewa kuanza maisha vile, nimesoma kwa kuungaunga tu, washkaji na rafiki zangu niliomaliza nao sekondari mwaka 2014 wengi wao wameoa, wengine washaolewa.
Yaani nikionana nao au kupishana nao njiani ni aibu tu, bora tuishie kuchati tu kupitia aidha sms, WhatsApp, Facebook. Nipo tu kama digidigi vile sina hili wala lile.
Hata akiba sina, siugui ovyoovyo. Siku nikitimuliwa home sijui itakuwaje. Japo Sir God analinda ile mbaya.