Yaan kazi yangu mishen town sinaga likizo kabisa hata siku moja, leo nasema ngoja nijipumzishe kidogo home nikae na mama watoto wangu na mwanangu anione walau kutwa nzima maana siku zote naingia home usiku ashalala! Tanesco na wenyewe wanafanya yao! Sasa hivi nimetoka nje kibarazani nalazimisha kiupepo chenyewe kina umoto moto balaaa. Bora ningeenda kuingiza hata ef tano aisee. Nilihama buguruni nkasema nikaishi tabata kwa washua kumbe huku ndo mambo magum kabisa kila siku umeme unazingua ndo nn hii?
Habari zenu! Nimejaribu kufikiria takribani one month kuhusu huu umeme unaopatikana huku kanda ya ziwa. Umeme umekuwa ukikatika Leo kesho haupo takribani wk nne tokea hili zoezi limeanza. Kama uamini uliza watu wa ukanda wa Shinyanga, Kahama, Tinde, Isaka, Maganzo na Mwadui. Umeme huku kwetu umekuwa wa mgao kiasi kwamba inarudisha nyuma jitihada za Raisi za Tanzania ya viwanda.
Operation cost za kuwasha Generator siku nzima ni ghari mno mpaka inafikia mahali tunaanza kumkumbuka Mhe. Prof Sospeter Muhongo maana tokea alivyoingia madarakani alituahidi kwamba hakuna mgao wa umeme na kweli hatukuona mgao huo. Mnyonge mnyongeni lkn haki yake mpeni. Ukweli Prof Muhongo alijitahidi kumaliza tatizo la umeme, Takribani miezi miwili aondoke tumeanza kurudi nyuma kufikiria umeme wkt Kwa hii karne umeme hautakiwi kuwa shida.
Nimejaribu kuongea na baadhi ya wafanyakazi wa Tanesco ili waniambie huu mgao wa umeme for how long? Wengi wameshindwa kujibu wakasema sio wasemaji wa Kampuni. Rahi yangu naomba uongozi wa Tanesco Shinyanga watuambie wateja wao huu ndo mgao wa umeme?
Nahisi kama unatengeneza mazingira ionekane muhongo kaonewa na umeme ulikuwa haukatiki, mkuu siasa eka pembeni au ulikuwa hukai nchi hii hadi upinzani kusema yeye ni prof muongo? Uwe na kumbukumbu vzr kama ulivosema nyala... fisadi na leo uimbe wimbo ule ule yasijekuwa ya lowa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.