Nahisi jamiiforums imesababisha airtel wakasikia kilio chetu

Igombe fisherman

JF-Expert Member
Apr 28, 2017
2,027
3,565
Juzi jumatano nimejiunga kifurushi cha wiki cha UN cha airtel cha tsh 5000 nikitegemea sitonunua tena vocha kwa ajiri ya kuwapigia jamaa ndugu na marafiki. Ila kitu cha kushangaza jana tarehe 19/12/2019 napiga simu naambiwa huduma katika sim card yangu zimethitishwa. Wakati ninadakika zaidi ya 600 ndani ya sim card nilichoka.

Nikafungua data nikakuta wengi wanalalamika hapa jamiiforums nikahesabu maumivu.

Nikalidhika na kutuma sms tu na kuchati fb na jf kupitia hilo salio. Ila kitu cha kushangaza nilipiga simu kimakosa tu. Badala ya kuruhusu card two ifanye kazi mi nikaamuru card one ifanye kazi na simu ikawezeshwa ndio nikagundua wamenifungulia huduma. Tena bila lile tangazo la usajiri wa nida.

Nawashukuru sana airtel kwa kutusikia japo mlikuwa na makosa kutufungia kabla ya muda mnaotuimbia kila siku tukipiga simu. Sasa hivi nalonga bila kiwewe mpaka mtakapoifunga tena tarehe 31/12 maana sina hiyo namba yenu mnayoitaka. Japo kuna watu mnawatumia namba zao na mimi kwenye kujiandikisha katika vitambulisho nilitumia namba yenu katika form. Kama vipi nitumieni nami namba ya NIDA. Maana huku kwa wavuvi mumetawala ninyi tu katika mawasiliano hivyo tukio la jana limetudhuru sana watu wa nyanza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pesa yako lakini unamshukuru Airtel kwa kufungulia huduma baada ya kukufungia kwa muda fulani. Afrika raha sana
Kumtawala muafrika ni rahisi sana. Nilikuwa nashangaa kwanini British, Arabs, Portuguese na wengine walikuwa wanajichagulia wafrika kama matunda yaliyondondoka mtini.
 
Nadhani kuna kitu walikuwa wanatukumbusha. Mi sijawashukuru kwa kufunga na kufungua bali kwa kuisikiliza jamiiforums. Hivyo nimegundua kuwa jamiforums ni nzuri kwa malalamiko pale unapoona hutendewi haki. Nadhani kwa tukio lingine watatusaidia endapo tutaandika hapa
Pesa yako lakini unamshukuru Airtel kwa kufungulia huduma baada ya kukufungia kwa muda fulani. Afrika raha sana
Kumtawala muafrika ni rahisi sana. Nilikuwa nashangaa kwanini British, Arabs, Portuguese na wengine walikuwa wanajichagulia wafrika kama matunda yaliyondondoka mtini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unawashukuru ? Hivi haujui kuwa ni wao ndio watakaoathirika zaidi kuliko wewe kutokana na mapato yao kushuka kwa wewe kutotumia simu. Operating costs zitakuwa kubwa kuliko faida.
 
Unawashukuru ? Hivi haujui kuwa ni wao ndio watakaoathirika zaidi kuliko wewe kutokana na mapato yao kushuka kwa wewe kutotumia simu. Operating costs zitakuwa kubwa kuliko faida.
Nimewashukuru kwa kupita hapa japo hawana special thread kama wenzao. Ila wamepita na kulekebisha. Si unajua selikari hii niyafaini wakati mwingine wako sawa kwa kuogopa faini na mamilioni kama tunayopigwa huku wavuvi. Kpsa dogo faini milioni mbili kisa unamtaji wa milioni 50 hivyo itabidi ulipe tu familia iende chooni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom