Nafunga mwaka 2016 na Heroes na Non Heroes hawa.....

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,542
108,836
Nimeona nichukue fursa hii adhimu kabisa kuwataja Mashujaa wangu wa kutukuka kabisa kwa mwaka huu unaoisha leo lakini pia nitawataja wale ambao pia naona kwa mwaka huu hawajawa Mashujaa wangu nikiwa na matumaini kuwa kwa wale Mashujaa wangu wataongeza bidii ili wazidi kunifurahisha na wale wasio Mashujaa wangu basi watajirekebisha ili mwakani 2017 watende Kazi zao vizuri na kwa ufanisi.

HEROES wangu kwa mwaka 2016 ni hawa wafuatao:

  1. Rais Dkt. John Magufuli...ameonyesha uthubutu wa Kiuongozi na Kiuwajibikaji.
  2. Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa...ni Mtu mvumilivu, makini na mwenye dira.
  3. JF Co Founder and MD Maxence Melo...ni Shujaa wa kweli na mfano wa kuigwa na wengi.
NON HEROES wangu kwa mwaka 2016 ni hawa wafuatao:
  1. Waziri Mwigulu Nchemba...sidhani kama mpaka sasa anajua anachokifanya.
  2. Mchezaji wa Yanga Amis Tambwe...alinisababisha nivunje kiti Taifa kwa kutufunga Simba.
  3. Waziri Jumanne Maghembe...katupotezea Faru John wetu na bado anatuzuga tu Watanzania.
Wapo wengi sana ila waliojikita mno katika Ubongo wangu uliotukuka kwa mwaka huu 2016 ni hao watajwa hapo juu.

Hata Wewe Member najua kwa mwaka huu unao Heroes na Non Heroes wako hivyo si vibaya basi na Wewe ukatiririka nao hapa ili tuuage mwaka vizuri ila hakikisha tu wanakuwa Watatu katika kila upande.

OMBI.

Tafadhali mnapowataja hapa hao Heroes wenu Watatu na Non Heroes wenu Watatu naomba MSITUKANE na tuwe na lugha ya staha zaidi na hata kama unapiga dongo basi liwe na Kidiplomasia zaidi ila tusifanye Character Assassination nitawashkuruni sana mkilizingatia hilo.

Zaidi ya hapo sina mengi zaidi ya kusema tu GENTAMYCINE nawatakieni Members wote wa JF Kheri ya Mwaka mpya wa 2017 na naomba uwe wa fanaka na matarajio yenu yafikiwe huku mkipata baraka nyingi za Mwenyezi Mungu ILA nichukue pia nafasi hii kuwaomba radhi / msamaha wale Members wote ambao labda kwa namna moja au nyingine niliwakwaza na wakajisikia vibaya. Yachukulieni tu yale yote kama changamoto kwenu kwani kuna muda mwingine nakuwa ' mtundu mtundu ' ili tu kuweza kuchangamsha ' Jamvi ' lakini sikuwa na nia mbaya na msisahau hata katika Familia lazima kuwe na Mtoto mmoja ' mtundu ' ili Nyumba ichangamke.

Nawapendeni nyote na mbarikiwe sana akhsanteni.
 
Heroes=ghetto ambassador,magufuli,lema.. non heroes=chid Benz,makonda,mwanajf fulan
 
Kwa moyo uliosafi bila kukurupuka wala kuwa mamluki

HERO

1. Raisi msataafu wa awamu ya 4 Baba Ridhwan yani huyu mzee he will an still be my remarkable in my head na ni role model wangu yani nashindwa kueleza najihisi vipi nikiwa naskiliza hotuba zake, mzee ambaye anang'ata huku anapuliza anajua watu wanataka nn, mda wote anatabasamu lenye maswali lukuki miongoni mwa watu hats great thinker huwa hawamuelewi mzee wa msogaa,
namu wish maisha marefu mzee wangu

NON HERO

1. UKAWA, japokuwa mi ni opostion but Hivi vyama. vilivyoungana hadi sasa sielewi nini kinaendelea katika ishu ya CUF kuhusu lipumba kwa nini hawa wasisaidiane kutafuta suluhisho, na kwa nn cuf walikataa chadema wasiingile maswala yao, au ndo wanaleta ule ugomvi wa kale??

swala la kupotea kwa Ben SAA 8 sijui nn kinaendelea mpaka sasa kwa Chadema na naona wapo kimya...
 
Heroes
1.The one and only The bold
Amenifanya niumalize mwaka vizuri, ni kama sikuishi kabisa kabla ya kufahamiana nae.
Sasa hivi ndio naishi,he give me life.

2.Edward Ngoyai Lowassa
Huyu Mzee sijui niseme nini kudhihirisha kiasi gani namkubali,nakosa maneno sahihi kabisa.
Kauli yake ya "Tulishinda lakini tukadhulumiwa,ila ushindi mkubwa zaidi ni kuvumilia kuepusha kumwaga damu za wananchi wasio na hatia"
Ishi maisha marefu my super hero E.N Lowassa

3. Maxence Melo
Huyu kama wengi tunavyofahamu ni mwanaharakati na mpigania uhuru wa kutoa maoni.Pia muanzilishi wa JamiiForums

Kitendo chake cha kijasiri kukataa kutoa taarifa zetu sisi watumiaji wa JF kimenifanya nimkubali na kumheshimu zaidi ya hapo kabla.
Ni mfano wa kuigwa na kila mmoja.
Mungu ampe nguvu na afya njema ya kuishinda vita iliyo mbele yake...amen.

Non Heroes
1.Malaika,Mtukufu sana...
Huu ni mwaka mbaya sana kutokea kiuchumi tokea nilipokuwa na akili na kuanza kujitegemea.
Mengi na mengine mengi mengi lakini maisha magumu yanayotukabili Watanzania tulio wengi yamenifanya nimchukie sana.
Japo sikumpa kura yangu sababu sijawahi kuvutiwa na uongozi wake lakini ameshindwa kuituma nafasi ya cheo chake kunipa sababu hata moja tu ya kumkubali.
Hadi mwaka unaisha hakuna lolote alilolifanya na maana kwangu.
Huyu ni failure wa mwaka.

2.Humphrey Polepole
Huyu kaka jamani mwaka jana alitokea kuniteka sana.
Hoja zake nzitonzito zilinifanya nimfuatilie na kumkubali, ila mwaka wa 2016 kayafichua makucha yake.
Amedhihirisha rangi yake ya asili aliyoificha kutupumbaza.
Kanivunja moyo sana kama kijana niliyemtegemea kutokuongozwa na tumbo.
Najua yupo humu... "UMENIANGUSHA POLEPOLE!"

3.Naibu Spika wa Bunge Tulia
Huyu mama katutia aibu wanawake wote.
Bunge lake limekosa viwango hata vya chini kabisa.
Ametumia madaraka yake kuzima sauti za wabunge wa upinzani.
Hakuna siku aliyonikera kama alipomzuia Mh. Mbowe kumuuliza swali Waziri Mkuu Majaliwa kuhusiana na rushwa ya mil. 10 walizogaiwa wabunge wa CCM kupitisha muswada wa habari.

Nami nichukue nafasi hii kuwatakia wanachama wenzangu wote wa JF heri ya mwaka mpya.
Kila la kheri na Mungu awabarik,nawapenda wote.
 
Heroe wangu ni..

Dr. Martin Luther King JR.
Huyu alishatutangulia mbele za haki miaka ya 60's lakini kwangu mimi ni shujaa wangu wa 2016.
Anaendelea kuishi kifikra mwaka hadi mwaka na katika mwaka huu mengi aliyoyapigania na kuyapinga yamezidi kujitokeza na kuhatarisha zaidi amani ya dunia.
Hakika King ni mwanaharakati ambaye hadi sasa hajatokea mwingine kama yeye au zaidi yake.
Nakupenda sana King na bado unaishi kwenye fikra za wengi.

Non Heroe
Rais Magufuli huyu mpaka sasa hajafanya chochote kwenye elimu yani ameisahau.
Wengi wamekosa mikopo ya elimu ya juu na wamerudi nyumbani kushindwa kugharamia masomo halo sifa na vigezo vya kupewa mikopo vyote wanavyo.
Hakuna nchi ya uchumi wa kati na viwanda pasipo na elimu bora.
Haijawahi kutokea duniani kote maybe iwe Tanzania na itakuwa maajabu ya dunia.
 
Back
Top Bottom