Nafikiria kufungua Office kubwa ya upelelezi, naomba ushauri

JembePoli

JF-Expert Member
Jul 14, 2015
1,324
993
Habari za mchana wana bodi.

Kwa jinsi mambo yalivyo magumu huku mtaani hasa biashara nimefikilia nimeona nitumie mtaji wangu wote kufungua Ofice kubwa ya upelelezi yaani niwe na leseni ya Mpelelezi binafsi.

Sasa sijajua kama sheria ya nchi hii itaniruhusu kwa anaejua tafadhari anisaidie hapo kwani najua kupitia wazo langu nitaajiri vijana wengi.
 
Habari za mchana wana bodi.

Kwa jinsi mambo yalivyo magumu huku mtaani hasa biashara nimefikilia nimeona nitumie mtaji wangu wote kufungua Ofice kubwa ya upelelezi yaani niwe na leseni ya Mpelelezi binafsi.

Sasa sijajua kama sheria ya nchi hii itaniruhusu kwa anaejua tafadhari anisaidie hapo kwani najua kupitia wazo langu nitaajiri vijana wengi.
Mkuu tuunganishe nguvu katika hilo. nina uziefu kubwa katika uchunguzi... if interested tuongee inbox
 
Ni ngumu kufungua kampuni inayojihusisha na mambo ya upelelezi ikawa na mafanikio kama wewe huna taaluma hiyo. Mambo ya upelelezi ni very technical na yana ethics zake sio kama kufungua duka la dawa. Na hata Serikali haitakuruhusu kama wewe hujasomea tena kwenye vyuo vya serikali, hii ni kwasababu mambo utakayoyapeleleza yanaweza kuingilia usalama wa taifa. Mfano Serikali inaweza kufanya assasination au kidnaping kwa mtu yeyote anayehatarisha usalama wa nchi , sasa ndugu wa huyo mtu wakija kwako wakakupa kazi ya kupeleleza then ukajua ukweli na uka u disclose hapo utakuwa unahatarisha usalama wa nachi na unaharibu mission za wenye wajibu wa kuhakikisha nchi inakuwa salama. Zipo sheria ngumu sana kwa private investigators hata katika nchi zilizoendelea kama US. Na pia lazima uangalie sheria za nchi kama zinaruhusu uchunguzi uliofanywa na taasisi binafsi kutumika mahakaman or else where? Kama hawaruhusu that means huwez kupata wateja. Na pia serikali inakuamin kiasi gan ili iruhusu idara zake kutumia ushahidi wako? Anyway ukifanikiwa naomba ajira!!!!.

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Ni ngumu kufungua kampuni inayojihusisha na mambo ya upelelezi ikawa na mafanikio kama wewe huna taaluma hiyo. Mambo ya upelelezi ni very technical na yana ethics zake sio kama kufungua duka la dawa. Na hata Serikali haitakuruhusu kama wewe hujasomea tena kwenye vyuo vya serikali, hii ni kwasababu mambo utakayoyapeleleza yanaweza kuingilia usalama wa taifa. Mfano Serikali inaweza kufanya assasination au kidnaping kwa mtu yeyote anayehatarisha usalama wa nchi , sasa ndugu wa huyo mtu wakija kwako wakakupa kazi ya kupeleleza then ukajua ukweli na uka u disclose hapo utakuwa unahatarisha usalama wa nachi na unaharibu mission za wenye wajibu wa kuhakikisha nchi inakuwa salama. Zipo sheria ngumu sana kwa private investigators hata katika nchi zilizoendelea kama US. Na pia lazima uangalie sheria za nchi kama zinaruhusu uchunguzi uliofanywa na taasisi binafsi kutumika mahakaman or else where? Kama hawaruhusu that means huwez kupata wateja. Na pia serikali inakuamin kiasi gan ili iruhusu idara zake kutumia ushahidi wako? Anyway ukifanikiwa naomba ajira!!!!.

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums

Mkuu ahsante sana kwa uchambuzi wa kina,
Ajira ni matokeo ya kufanikisha adhima yangu. Nimeona nimtafute mwasheria aniweke sawa sheria iko vipi japo mambo ya kwenda kusoma miaka 3 au 4 naweza
 
Habari za mchana wana bodi.

Kwa jinsi mambo yalivyo magumu huku mtaani hasa biashara nimefikilia nimeona nitumie mtaji wangu wote kufungua Ofice kubwa ya upelelezi yaani niwe na leseni ya Mpelelezi binafsi.

Sasa sijajua kama sheria ya nchi hii itaniruhusu kwa anaejua tafadhari anisaidie hapo kwani najua kupitia wazo langu nitaajiri vijana wengi.


mkuu wazo zuri lakini sheria hazijaruhusu hii kufanywa na watu au kampuni binafsi! mamlaka haya wanayo polisi na takukuru na vyombo vingine baadi vya serikali! wew fungia ofsi ya kisheria ya kutoa msaada wa kisheria... ushauri... pamoja na kuingia katika mambo ya kufanya mauziano ya mali na vitu kama hivyo.. mfano nataka kununua kiwanja nakufuata wew ufanye upelelezi juu ya ukweli na uhalali wa kiwanja hicho.. na mambo mengine.. hapo unakuwa unaingia mkataba na mnunuzi.. wew ndo utamwambia anunue au lah baada ya kujiridhisha upande wa kisheria.

pia nakushauri pamoja na hilo kuwa pembeni na kampuni ya kuevaluate thamani ya vitu..unatoa ushauri wa kisheria pamoja na thamanini
/value ya hiyo mali.
 
Nafikiri bado serikali haijarusu kuwa na private detectives. ila wanasaidia sana hasa kusaidia wanaoonewa. na michepuko mingi itawekwa hadharani maana nikihisi wangu anachepuka tayari nawambaia jamaa. muda tu unanaswa live !!
bado hatuko huru saana na sana sana tutawatumia vibaya kumalizana tu!!!
 
hakuna sheria inaruhusu mkuu kwa hilo tusibishane! investigation zote kwa sheria za tz hazifanywi na private institution.. leo hii tukio likitokea mfano la maauwaji au kitu kingine au wizi wanaofanya upelelezi ni polisi na taasisi nyingine za serikali.

Huu ndio ukweli mkuu, kampuni binafsi zinafanya uchunguzi wa mambo ya kawaida kama kuwatafuta wadaiwa nk, sio serious issues.

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom