macho_mdiliko
JF-Expert Member
- Mar 10, 2008
- 21,440
- 38,682
Ushauri wako ni mzuri lakini inategemea na aina ya mtu. Wewe unaweza kuwa mchapakazi na mbunifu hata pale unapokwama kabisa lakini kuna watu wengine inawawia vigumu mno. Ndiyo maana umetowa huo mfano wa dada aliyekopa mil 400 lakini hakufanikiwa. Hii inamaanisha kuwa formula ya mafanikio sio moja kwa kila mtu. Huyu mwanzisha thread nilivyomsoma nadhani itakuwa vizuri sana kama ataendelea na kazi na hapo hapo atafute kitu cha kufanya baada ya kazi. Kuna mdau ameshauri bustani, jambo ambalo naona ni zuri na rahisi kwake. Unajua ujasiriamali ndugu yangu kila mtu ana kipaji chake. Kwa jinsi aliuliza na kujieleza tu naona anaweza ku-straggle sana kama ataamua kuacha kazi ghafla. My verdict: atafute kitu cha kufanya baada ya muda wa kazi na weekend na aendelee na kazi mpaka atakapoona ujasiriamali umekaa vizuri.Mtaji mkubwa sio tiketi ya kufanikiwa kwenye biashara na hakuna mtaji maalumu wa kuanza nao.
Kuna Mdada alikopa milioni 40o akaanzisha biashara na so fa biashara imekufa.
Unaweza anza na 10,000 na ukapata progress kubwa sana.
Biashara sio mitaji ji ubinifu.
Unaweza pewa milion hata 100 ukaanzisha biashara ya ajabu sana na ukafilisika baada ya muda fulani