Nafikiri ni wakati wa familia za viongozi wa upinzani kudai Katiba Mpya

Hakika ujinga wa uzeen lazma utakufa nao tu
Kipindi kirefu viongozi wa upinzani wameshupaza shingo kuhamasisha uhuni wa maandamano dhidi ya serikali halali ya nchi yetu.

Nafikiri muda umefika sasa na najua viongozi wote wana watoto wakubwa tu wa kuweza kutoka barabarani ingekuwa vyema kwa kuwa chadema na wanaharakati uchwara wapo kwenye kushinikiza katiba mpya,hiyo ni njia bora kuliko yale makongamano.

Wangeungana na kutoa watoto,wake,waume na mama zao,
Wajitokeze kwa wingi wamsaidie mzee wao aliyepo mahabusu.

Sisi hatuna muda wa kupoteza zaidi ya kutafuta dona la wanetu kuliko kwenda kupigania tumbo la mwingine ambaye akipata ruzuku wala hatujali.

Huu ni ushauri kila mmoja ahamasishe familia yake
1.Mbowe
2.Lissu
3.Lema
4.Msigwa
5.Heche
Najua mnyika yeye ni mstaarabu hapendi hamasisha uhuni wala hana watoto wakubwa.
Zitto kabwe na James Mbatia mkiwatoa familia zenu tutaunga mkono bila mashariti!
Nimeandika hapa baada ya kuona watu wengi wapo jela wamepata ulemavu halafu walio wahamasisha wamekimbia kujificha nje na familia zao wala hazijadhurika!
 
Back
Top Bottom