sunday isdory
Member
- May 16, 2011
- 23
- 1
Nafasi za Masomo !
Chuo cha Ualimu Kihinga ni chuo cha binafsi kinacho waandaa wanafunzi kuwa waalimu bora katika shule za sekondari. Chuo kinatoa mafunzo ya hali ya juu na kina waalimu waliobobea katika fani ya ufundishaji na masomo ya ziada kama komputa na stadi za jamii. Hakuna mabweni ya wanafunzi kwa sasa, wanafunzi watakuwa wa kutwa ikiwa na maana kwamba watajitafutia malazi na chakula. Barua za maombi zinakaribishwa kwa wote wenye sifa katika mafunzo ya stashahada (Diploma) kabla ya tarehe 28/08/2011
STASHAHADA YA UALIMUSifa za kujiunga kwa wanafunzi watarajali: 1. Kidato cha sita akiwa amefaulu Principal Pass 1 na subsidiary pass 1 kwa masomo yanayofundishwa sekondari kidato cha 1-42. Kidato cha Sita na kufaulu kiingereza katika kidato cha 4 kwa alama A, B, C and D Sifa za kujiunga kwa wanafunzi waliopo kazini:1. Cheti cha ualimu daraja la III na awe amefanya kazi kwa zaidi ya muaka 1.2. Kidato cha sita na principal pass I na subsidiary I kwa masomo yanayofundishwa sekondari kidato cha 1-4. Fomu za maombizinapatikana shule ya sekondari Kihinga au kutumia barua pepe baada ya kupokea ada ya Shs. 10,000/= kwa kuiweka kwenye akaunti Na. 0150087144204 Kihinga TTC CRDB. TUMA BARUA YA MAOMBI, ANUANI KAMILI, CV NA NAKALA YA VYETI KWA: Mkuu wa Chuo,
Chuo cha Ualimu, Kihinga
S.L.P 270
Kigoma, Tanzania.
Simu: 0759192671, 054767490, 0784 425 399 Barua pepe: kihingattc.principal@boc-tz.org