Ngamanya Kitangalala
JF-Expert Member
- Sep 24, 2012
- 501
- 1,214
Tanzania nchi yetu kama ilivyo kawaida kila baada ya miaka mitano, tunafanya uchaguzi mkuu wa kupata viongozi wa kututumikiakatika kipindi kingine cha miaka mitano
Sasa tukiwa tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2020,Kwa muda mrefu kumekuwepo na dhana potofu juu za nafasi za kugombea za kuwatumikia wananchi, kuna baadhi ya watanzania wachache wenye kuamini kupata nafasi ya kuwatumikia wananchi ni mapambano ya kufa na kupona
Kwa mtizamo wangu, nafasi za kugombea kuwa mtumishi wa wananchi, sio za kukimbilia wala kupambana na kupigana vikumbo, kuna mambo matatu(3) muhimu ya kuzingatia
Kwanza , ni mwenyezi Mungu , yeye pekee ndiye mwenye uwezo na mamlaka ya kuamua nani awe wapi na kwa wakati gani, ni sahihi kwa mtu huyo kutumikia wananchi wa eneo husika
Pili , ni wananchi wenyewe, wao kwa umuhimu walionao, wana nafasi kubwa zaidi ya kufanya tathimini na kuamua nani awe mtunishi wao na kwa wakati gani
Mwisho , japokuwa sio mwisho kwa umuhimu, ni chama unachoamini kwenye itikadi zake, Chama kama taasisi wana sheria, taratibu na kanuni zinazoendesha zoezi la kuamua nani awe mtunishi wa wananchi na katika eneo gani la uwakilishi,
Chama kama taasisi wana utaratibu wa kufanya tathimini ya nani anafaa kuwa mtumishi wa wananchi kwa kuzingatia vigezo walivyojiwekea
Kwa hiyo, ukiyazingatia hayo hapo juu, nafasi za kuwa mtumishi wa wananchi sio za kukimbilia, sio za kupambana wala sio kufa na kupona
Sasa tukiwa tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2020,Kwa muda mrefu kumekuwepo na dhana potofu juu za nafasi za kugombea za kuwatumikia wananchi, kuna baadhi ya watanzania wachache wenye kuamini kupata nafasi ya kuwatumikia wananchi ni mapambano ya kufa na kupona
Kwa mtizamo wangu, nafasi za kugombea kuwa mtumishi wa wananchi, sio za kukimbilia wala kupambana na kupigana vikumbo, kuna mambo matatu(3) muhimu ya kuzingatia
Kwanza , ni mwenyezi Mungu , yeye pekee ndiye mwenye uwezo na mamlaka ya kuamua nani awe wapi na kwa wakati gani, ni sahihi kwa mtu huyo kutumikia wananchi wa eneo husika
Pili , ni wananchi wenyewe, wao kwa umuhimu walionao, wana nafasi kubwa zaidi ya kufanya tathimini na kuamua nani awe mtunishi wao na kwa wakati gani
Mwisho , japokuwa sio mwisho kwa umuhimu, ni chama unachoamini kwenye itikadi zake, Chama kama taasisi wana sheria, taratibu na kanuni zinazoendesha zoezi la kuamua nani awe mtunishi wa wananchi na katika eneo gani la uwakilishi,
Chama kama taasisi wana utaratibu wa kufanya tathimini ya nani anafaa kuwa mtumishi wa wananchi kwa kuzingatia vigezo walivyojiwekea
Kwa hiyo, ukiyazingatia hayo hapo juu, nafasi za kuwa mtumishi wa wananchi sio za kukimbilia, sio za kupambana wala sio kufa na kupona