muafi
JF-Expert Member
- Oct 6, 2015
- 2,113
- 4,793
View attachment 808369
Kampuni ya ulinzi ya KK Security Tanzania Ltd. Yenye ofisi yake Capripoint mbele kidogo na Kamanga Fery Mwanza na ofisi kuu Mikocheni B Dar es Salaam, Inatangaza nafasi ya kazi Ya ulinzi.
VIGEZO
HATUA
- Elimu: Kidato cha nne na kuendelea.
- Uwezo wa kusoma, kuandika na kuongea kiingereza.
- Umri wa miaka 23 - 42
- Urefu futi 5.7 na kuendelea (kwa wanaume)
- Afya njema
- Asiwe na makosa yeoyote ya jinai
- Awe tayari Kazi Mkoa wowote wa Tanzania.
- Mwombaji Afike na barua ya maombi ya kazi iliyoandikwa kwa mkono na mwombaji kwa kiingereza
- Nakala za vyeti na vyeti halisi, cheti cha kuzaliwa au hati ya kiapo.
- Barua ya utambulisho kutoka kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa.
- Barua za wadhamini wawili (zipiigwe muhuri kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa juu ya picha na Wasiwe walinzi au wanafunzi).
- Mdhamini awe na kitambulisho halali.
- Mwombaji awe na picha 5 za pasipoti zilizopigwa hivi karibuni
- Mwombaji awe tayari kwa mahojiano na usaili.
Usaili utafanyika kuanzia Tarehe 16 July , Ofisini kwetu Capripoint Mwanza kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni.
Epuka matapeli, Hakuna rushwa ni vigezo tu vinazingatiwa.
Broo nataka kumsendi mdogo wangu juma tatu aje vigezo vyote anavyo but naomba unieleweshe hapo je, anaweza kuja na barua ya wadhamini walioko nje ya mwanza au mpaka apate wadhamini wote kutoka hapo hapo mwanza? Maana yeye si mkazi Wa mwanza