Nafasi ya wajomba katika ndoa ya mtoto wa kike

Carnivora

JF-Expert Member
Jan 26, 2018
3,651
5,987
Habari wakuu

Katika jamii zetu za Kitanzania ni jambo la kawaida kusikia bint anapotaka kuolewa wajomba wake lazima wahusike kwa namna moja ama nyingine. Sote tunafahamu wajomba ni kaka wa mama wa mtoto anayetaka kuolewa hivyo kama ndugu wa karibu wana haki ya kujulishwa kinachoendelea. Kila jamii ina taratibu zake, hivyo uzito wa mambo hayo pia hutofautiana toka jamii moja ama nyingine. Kuna jamii nyingine mpaka wajomba nao wanahusika kupanga mahari.

Hali huwa mbaya zaidi kwa baadhi ya jamii ikiwa wajomba wataona hawajatendewa haki kwa namna moja ama nyingine. Wanaweza kupinga ama kususia mahari/harusi kabisa ya mtoto wa dada yao. Hivi mjomba ana nafasi gani katika bint anayeolewa wakati huyo mtoto si wa ukoo wao? Ni mtoto wa ukoo mwingine kazaliwa kwa dada yao. As long as dada yao ( mama wa bint) yupo, na hata kama hayuko hai wao kwanini wanaulazima watie neno ama kudai fungu la mahari? Wana haki gani? Unakuta hata hawajahusika kwa namna yoyote ile katika malezi ya huyo mwolewaji.

Ni mila tu za kizamani au ni utaratibu upi? Mi sielewi. Ifike mahali tuache kuishi kwa mazoea....wajomba, wajomba eeeh wana mamlaka gani? Kwanini wasiwe baba wadogo/wakubwa, mashangazi ambao wanaweza kusema mtoto wa kaka yao (ukoo wao)?
Yaani mimi Mgunya nimeoa mchaga tukazaa bint. Siku posa imekuja wachaga wanasimama dede kwenye posa....hivi huyu mtoto ni wa kwao? Si wanasema mtu akiolewa anahamia huko kwa mumewe....sasa nyinyi wajomba mnadai nini huku?

Katika dini ya Kiislam, mwenye mamlaka ya kuozesha ama kukataa kuozesha ni baba(kama yupo hai) wa bint. Mjomba hana haki yoyote na wala hausiki kukubali posa wala kuwakubalia waleta posa na kuwafungisha ndoa. Akatae, akubali, aridhike/asiridhike habatilishi uhalali wa ndoa kwa namna yoyote ile. Kwa maana nyingine mjomba ni mtu wa kupewa taarifa tu kuwa mpwa wako anaolewa.

Je, haya mambo ya wajomba kwa upande wa jamii yako yakoje na yapi maelekezo ya dini?

Kama sina elimu nipewe. Msinikashifu.
 
Ninafahamu vyema sema kuiweka kwenye kiswahili sijui nifanyeje.
Kiufupi kikwetu au kiujumla hakuna mtoto wa mwanaume mtoto huwa ni wa Mama, sasa wajomba wanahusika kwa sababu wanatoka upande wa mama.

Refer Israeli huko huwezi kuitwa Myahudi kama mama yako sio Myahudi hata kama Baba ni Myahudi ila Hata kama Baba ni Blaki na mama ni Myahudi basi wewe ni Myahudi.

Khan!
 
Labda itokee mtoto ni wa nje ya ndoa kiimani yangu ya kiislam ndio upande wa mama wana haki ya kuozesha mtoto wao

Kama mtoto ni wa ndani ya ndoa ikatokea baba yake amefariki bas kama ana kaka zake waliozaliwa naye anatoa idhini ya dada yake kuozeshwa ikiwa baba yu hai bas ataozesha bintiye na sio wajomba kwa mtoto wa ndani ya ndoa

Kwa mwenye ufaham zaidi ataongezea
 
mkuu mjomba ndo ndugu yako kabisa tena kabisa... ukiingia bifu mpaka na wajomba hakika kama ni binti wewe ni shangingi haswa!
back to the point: Baada ya mama kuzaa malezi na ushauri wa upande wa mama unakuwa mikononi wa wajomba ndo maana ni rahisi kuishi na mjomba kuliko mama mdogo ama mama mkubwa! mjomba ni mama pia ni baba lakini pia ni rafiki.
 
Ninafahamu vyema sema kuiweka kwenye kiswahili sijui nifanyeje.
Kiufupi kikwetu au kiujumla hakuna mtoto wa mwanaume mtoto huwa ni wa Mama, sasa wajomba wanahusika kwa sababu wanatoka upande wa mama.

Refer Israeli huko huwezi kuitwa Myahudi kama mama yako sio Myahudi hata kama Baba ni Myahudi ila Hata kama Baba ni Blaki na mama ni Myahudi basi wewe ni Myahudi.

Khan!
Duh! Ndio wale wa materlinear society?
 
Labda itokee mtoto ni wa nje ya ndoa kiimani yangu ya kiislam ndio upande wa mama wana haki ya kuozesha mtoto wao

Kama mtoto ni wa ndani ya ndoa ikatokea baba yake amefariki bas kama ana kaka zake waliozaliwa naye anatoa idhini ya dada yake kuozeshwa ikiwa baba yu hai bas ataozesha bintiye na sio wajomba kwa mtoto wa ndani ya ndoa

Kwa mwenye ufaham zaidi ataongezea
Naam upo sahihi. Unakuta sehem wajomba wamesusua kisa labda hawakuitwa kwenye kusoma barua (posa). Au wajomba nao wanapanga sisi katika mahari tuletewe ng'ombe 2. Kwanini?
 
mkuu mjomba ndo ndugu yako kabisa tena kabisa... ukiingia bifu mpaka na wajomba hakika kama ni binti wewe ni shangingi haswa!
back to the point: Baada ya mama kuzaa malezi na ushauri wa upande wa mama unakuwa mikononi wa wajomba ndo maana ni rahisi kuishi na mjomba kuliko mama mdogo ama mama mkubwa! mjomba ni mama pia ni baba lakini pia ni rafiki.
Pana ukakasi hapa.
 
Naam upo sahihi. Unakuta sehem wajomba wamesusua kisa labda hawakuitwa kwenye kusoma barua (posa). Au wajomba nao wanapanga sisi katika mahari tuletewe ng'ombe 2. Kwanini?
Kiislam mahari anataja binti mwenyewe sababu ndiye anayeenda kumanuliwa miguu hukooo.... Hao wajomba ni wambea tu
 
Habari wakuu

Katika jamii zetu za Kitanzania ni jambo la kawaida kusikia bint anapotaka kuolewa wajomba wake lazima wahusike kwa namna moja ama nyingine. Sote tunafahamu wajomba ni kaka wa mama wa mtoto anayetaka kuolewa hivyo kama ndugu wa karibu wana haki ya kujulishwa kinachoendelea. Kila jamii ina taratibu zake, hivyo uzito wa mambo hayo pia hutofautiana toka jamii moja ama nyingine. Kuna jamii nyingine mpaka wajomba nao wanahusika kupanga mahari.

Hali huwa mbaya zaidi kwa baadhi ya jamii ikiwa wajomba wataona hawajatendewa haki kwa namna moja ama nyingine. Wanaweza kupinga ama kususia mahari/harusi kabisa ya mtoto wa dada yao. Hivi mjomba ana nafasi gani katika bint anayeolewa wakati huyo mtoto si wa ukoo wao? Ni mtoto wa ukoo mwingine kazaliwa kwa dada yao. As long as dada yao ( mama wa bint) yupo, na hata kama hayuko hai wao kwanini wanaulazima watie neno ama kudai fungu la mahari? Wana haki gani? Unakuta hata hawajahusika kwa namna yoyote ile katika malezi ya huyo mwolewaji.

Ni mila tu za kizamani au ni utaratibu upi? Mi sielewi. Ifike mahali tuache kuishi kwa mazoea....wajomba, wajomba eeeh wana mamlaka gani? Kwanini wasiwe baba wadogo/wakubwa, mashangazi ambao wanaweza kusema mtoto wa kaka yao (ukoo wao)?
Yaani mimi Mgunya nimeoa mchaga tukazaa bint. Siku posa imekuja wachaga wanasimama dede kwenye posa....hivi huyu mtoto ni wa kwao? Si wanasema mtu akiolewa anahamia huko kwa mumewe....sasa nyinyi wajomba mnadai nini huku?

Katika dini ya Kiislam, mwenye mamlaka ya kuozesha ama kukataa kuozesha ni baba(kama yupo hai) wa bint. Mjomba hana haki yoyote na wala hausiki kukubali posa wala kuwakubalia waleta posa na kuwafungisha ndoa. Akatae, akubali, aridhike/asiridhike habatilishi uhalali wa ndoa kwa namna yoyote ile. Kwa maana nyingine mjomba ni mtu wa kupewa taarifa tu kuwa mpwa wako anaolewa.

Je, haya mambo ya wajomba kwa upande wa jamii yako yakoje na yapi maelekezo ya dini?

Kama sina elimu nipewe. Msinikashifu.
Kwetu sisi mama ni mtu muhimu sana kwa mtoto. Mama hasingiziwi, tofauti na baba (naomba msinirushie madongo). Siku hizi kuna DNA Test ya kuthibitisha vinasaba vya baba, lakini zamani kulikuwa hakuna namna ya kuthibitisha kuwa huyo anayetajwa kuwa baba wa mwana ni baba kweli au kasingiziwa. Kwa mantiki hiyo ndipo heshima kubwa kwenye kuozesha Binti au Kijana walipewa wajomba. Heshima kwa baba iko pale pale, haipingwi, lakini kwa niaba ya mama wajomba lazima wasimame kama wazazi wa upande wa pili. Samahani kama nimekukwaza, nimejaribu kueleza mantiki hiyo kama ninavyoijua mimi.
 
Back
Top Bottom