Nafasi ya Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na Wagombea

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
Chenge na Uspika

Suala la Bwana Andrew Chenge kugombea uspika limezua mjadala maeneo mbalimbali kama ilivyokuwa wakati kashfa ya radar ilipowekwa adharani (na kashfa nyingine zilizoibuka) na vile vile mijadala mbalimbali inayohusiana na kesi yake ya kuendesha gari lwa uzembe na bila kuwa na bima halali!

Hivyo si jambo geni kusikia mjadala unaomuhusu Bwana Chenge. Swali la kujiuliza kwanini ajadiliwe?

Kwa wengine hakuna sababu ya Bwana Chenge kujadiliwa. Ni haki yake ya kikatiba kugombea nafasi ya uspika! ni msomi na ni kiongozi! pia sheria iko hivi 'innocent until proven guilty na siyo 'guilty until proven innocent'.

Kwa wengine lazima ajadiliwe kwa sababu hafai! ana kesi mahakamani, hajawahi kutoa maelezo ya kuridhisha kuhusu kuhusika kwake kwenye kashfa ya radar na mikataba mingine ambayo imeisabishia serikali na nchi yetu hasara kubwa. Kama kiongozi mwenye nia ya kuongoza ni lazima angetoa maelezo kuhusu hayo yote kabla hajafikiria kuomba ridhaa ya kuongoza chombo muhimu kama bunge!!

kwangu mimi huyu Bwana Chenge lazima ajadiliwe. Lazima wadau wapate nafasi ya kutoa ma-dukuduku yao waliyonayo moyoni. Si sahihi kuruhusu hii hali iendelee ya baadhi ya viongozi kutokuwa na chembe ya aibu wala woga wa mawazo ya watu!

Hata kama yeye ni safi na hana makosa watanzania wana haki ya kujua hivyo kabla hajathubutu kugombea nafasi yoyote ya uongozi! Busara ni yeye kukaa pembeni na kuruhusu ukweli ujulikane kabla ya kurudi kwa wananchi kuomba uongozi! hii imeonekana huko Kenya kwa waziri wa mambo ya nje na katibu wake kujiuzulu siku za karibuni.

Kwa kukaa pembeni haimaanishie wewe ni mkosaji ila inaonyesha heshima uliyonayo kwa taratibu na maadili ya kiungozi. Inathibitisha uwezo na busara zako kama kiongozi!

Kwa jeuri ya kuamua kuogombea kwa kisingizio ni 'haki ya kikatiba' na 'innocent until proven guilty' ni wazi busara na heshima ya Bwana Chenge ni vitu vya kuhojiwa! Ni mtu wa aina gani huyu? Hana aibu! hana soni! hana haya!

Kwani angekaa pembeni na kujisafisha angepoteza nini? au kwa sababu hata raisi wa nchi hajasema lolote na ameendelea kukaa kimya basi anaweza kufanya na kuamua chochote? auu kwa sababu raisi alimnyanyua mkono wakati wa kampeni ameafikia mahali ameona anastahili kuwa spika na kuliongoza bunge!

Ni wapi tunakoelekea au tunakopelekwa? Kwa njia nyingine naamini inaweza kuwa ni a 'blessing in disguise' haya yote yanatokea! Mungu ameamua kutuonyesha njia za kujikwamua kutoka kwenye uongozi mbovu tulionao!

Kama raisi wa marekani alipigiwa kelele kwa kuchelewa 'kufanya maamuzi' wakati wa suala la kuvuja kwa mafuta - BP na bado anaendelea kupigiwa kelele kuhusu mambo mengine ambayo hata hakusababisha yeye, kwa nini huyu Bwana Chenge aipigiwe kelele na kufunzwa adabu kwa yote aliyoyafanya au aliyoshindwa kufanya? badala yake tunamwacha achezee karatasi zilizotengenezwa kwa fedha za wavuja jasho kujaza eti anataka kuwa spika!! amuongoze nani? kwa heshima ipi watakayompa?
 
Msando,

Kwanza karibu jukwaani. Na karibu kujadili hoja na tunatajia ushiriki wako hapa kwani wewe kama mwanasheria tunahitaji ujuzi wako. karibu
 
Chenge hajakuudhi wewe tu Msando bali amewaudhi watanzania wengi na kujiuliza anataka nini? is he serious? je nawaonaje watanzania?.

Kuna katabia ka viongozi wa ngazi za kitaifa kujiona kwamba wanajua zaidi na kwamba mtanzania ni mtu wa kusahau kirahisi. Hivi ndivyo chenge anavyojifariji, hajui tunaikumbuka sana kashfa mbaya ya Radar ambayo mpaka sasa ni mtuhumiwa aliyepaswa kuwa mahabusu.

Kitendo cha Chenge kujidai kuita press conference na kutangaza nia yake ya kutaka kugombea USPIKA ni sawa na Kuwa- BEEP au kuwa kanyaga watanzania kwa Makusudi ili aone reaction zao.

CCM ijue kubebana kutakiua chama cha mapinduzi kwani MWANANCHI WA MWISHO ATAKAPOPOTEZA IMANI NI CHAMA CHA KIJANI hapo ndipo mwisho wake. CCM isome alama za nyakati na ijifunze katika uchaguzi uliomalizika na ifahamu kwamba idadi ya watanzania wanaoamini kwamba bila CCM HAIWEZEKANI imepungua sana na next election 2015 idadi hii itapungua zaidi.

Jibu la ni kwa nini popularity ya CCM ina fade out ni kwa mambo kama Chenge anawafanyia Watanzania. Hii ni dharau kwa Wabunge safi tuliowachagua sisi kuongozwa ni SPIKA FISADI. Chenge atachafua Bunge letu, Chenge atalitia taifa aibu tunashauri akae pembeni kwani lengo lake tunalijua; siyo zuri asilani.
Maelezo aliyoyatoa ya kujisafisha ni Unafki mbele ya watanzania, awe na aibu awe na Staha akae kando kwa heshima yake na mustakabali wake wa kisiasa.
 
Msando nakushukuru sana. Umeelezea hisia za walio wengi wetu. Mwanzoni nilisema katika thread moja kuwa kugombea kwa huyu bwana kunanitia kichefu chefu. Ilikuwa kwa sababu kama hizi hizi. Lakini kinachonisikitisha zaidi ni ile hali ya viongozi wakuu wa Chenge na chama chake kisivyoona umuhimu wa kuwajibika kwa wananchi kwa makosa yao. Siku hizi kumeingia kautamaduni kwa kujiuzulu unaposhinikizwa kwa sababu ya makosa kunatosha hata kama umeacha maswali mangapi yasiyojibiwa kwa makosa hayo.

Hizi ni zama za critical thinking, watu hawawezi tena kuburuzwa kama zamani za "zidumu fikra za mwenyekiti." Watu sasa wameamka, na wanafikiri kwa kina kabla ya kukubali jambo. Profesa wangu alituambia darasani wakati fulani, "If two people are talking, and one of them agrees with everything the other says, he is not thinking." Siku hizi hakuna mtu mmoja afikiriaye kwa niaba ya wengine, kila mtu na afikiri. Hili ndilo Chenge na ccm yake wanahitaji kujua. CCM, get this loud and clear: ZAMA ZA "ZIDUMU FIKRA ZA M/KITI" ZIMEKWISHA.
 
Chenge na Uspika

Suala la Bwana Andrew Chenge kugombea uspika limezua mjadala maeneo mbalimbali kama ilivyokuwa wakati kashfa ya radar ilipowekwa adharani (na kashfa nyingine zilizoibuka) na vile vile mijadala mbalimbali inayohusiana na kesi yake ya kuendesha gari lwa uzembe na bila kuwa na bima halali!

Hivyo si jambo geni kusikia mjadala unaomuhusu Bwana Chenge. Swali la kujiuliza kwanini ajadiliwe?

Kwa wengine hakuna sababu ya Bwana Chenge kujadiliwa. Ni haki yake ya kikatiba kugombea nafasi ya uspika! ni msomi na ni kiongozi! pia sheria iko hivi 'innocent until proven guilty na siyo 'guilty until proven innocent'.

Kwa wengine lazima ajadiliwe kwa sababu hafai! ana kesi mahakamani, hajawahi kutoa maelezo ya kuridhisha kuhusu kuhusika kwake kwenye kashfa ya radar na mikataba mingine ambayo imeisabishia serikali na nchi yetu hasara kubwa. Kama kiongozi mwenye nia ya kuongoza ni lazima angetoa maelezo kuhusu hayo yote kabla hajafikiria kuomba ridhaa ya kuongoza chombo muhimu kama bunge!!

kwangu mimi huyu Bwana Chenge lazima ajadiliwe. Lazima wadau wapate nafasi ya kutoa ma-dukuduku yao waliyonayo moyoni. Si sahihi kuruhusu hii hali iendelee ya baadhi ya viongozi kutokuwa na chembe ya aibu wala woga wa mawazo ya watu!

Hata kama yeye ni safi na hana makosa watanzania wana haki ya kujua hivyo kabla hajathubutu kugombea nafasi yoyote ya uongozi! Busara ni yeye kukaa pembeni na kuruhusu ukweli ujulikane kabla ya kurudi kwa wananchi kuomba uongozi! hii imeonekana huko Kenya kwa waziri wa mambo ya nje na katibu wake kujiuzulu siku za karibuni.

Kwa kukaa pembeni haimaanishie wewe ni mkosaji ila inaonyesha heshima uliyonayo kwa taratibu na maadili ya kiungozi. Inathibitisha uwezo na busara zako kama kiongozi!

Kwa jeuri ya kuamua kuogombea kwa kisingizio ni 'haki ya kikatiba' na 'innocent until proven guilty' ni wazi busara na heshima ya Bwana Chenge ni vitu vya kuhojiwa! Ni mtu wa aina gani huyu? Hana aibu! hana soni! hana haya!

Kwani angekaa pembeni na kujisafisha angepoteza nini? au kwa sababu hata raisi wa nchi hajasema lolote na ameendelea kukaa kimya basi anaweza kufanya na kuamua chochote? auu kwa sababu raisi alimnyanyua mkono wakati wa kampeni ameafikia mahali ameona anastahili kuwa spika na kuliongoza bunge!

Ni wapi tunakoelekea au tunakopelekwa? Kwa njia nyingine naamini inaweza kuwa ni a 'blessing in disguise' haya yote yanatokea! Mungu ameamua kutuonyesha njia za kujikwamua kutoka kwenye uongozi mbovu tulionao!

Kama raisi wa marekani alipigiwa kelele kwa kuchelewa 'kufanya maamuzi' wakati wa suala la kuvuja kwa mafuta - BP na bado anaendelea kupigiwa kelele kuhusu mambo mengine ambayo hata hakusababisha yeye, kwa nini huyu Bwana Chenge aipigiwe kelele na kufunzwa adabu kwa yote aliyoyafanya au aliyoshindwa kufanya? badala yake tunamwacha achezee karatasi zilizotengenezwa kwa fedha za wavuja jasho kujaza eti anataka kuwa spika!! amuongoze nani? kwa heshima ipi watakayompa?

Wakati wengine tukiwa bado tunaugulia majeraha tuliyopata kwenye uchaguzi Mkuu,

Wakati tukiwa bado hatujalipa hata madeni tuliyokopa ili kuhakikisha kuwa CCM inashinda uchaguzi wa mwaka huu,

Wakati bado tunatafakari kilichojili kwenye uchaguzi wa mwka huu kwa lengo la kuweka mazingira ya kushinda kwa kishindo 2015,

Wakati wengine tukiwa bado hata hatujapata maneno bora ya kuwashawishi ndugu zetu tuliyogombana nao wakati wa uchaguzi kwa lengo la kumaliza uhasama uliyojitokeza,

Wakati wengine tukiwa tunatafuta siku nzuri inayofaa kwenda kutubu dhambi tulizotenda wakati wa kuhakikisha kuwa CCM inashinda,

Wakati Bw. Chenge akijua fika kwamba kitendo chake cha kushindwa kujieleza mbele ya waandishi wa Habari juu ya fedha zilizokuwa kwenye akaunti yake ya nje kimekigharimu Chama chetu cha CCM kwenye uchaguzi wa mwaka huu,

Na Wakati Bw. Chenge akijua ukweli juu ya mchango wake katika uongozi wa nchi hadi akaitwa Mzee Simple yaani wa kila kitu ni rahisi,

Napata shida sana kuamini yafuatayo:

1. Iwapo ni kweli ana dhamira ya dhati ya kugombea Uspika,

2. Iwapo kugombea kwake kuna agenda zaidi ya aliyoyaongea,

3.Iwapo hakusudii kumchanganya na kumtisha JK wakati huu ambao anatafakari ni namna gani atatibu majeraha ya Taifa baada ya Uchaguzi, Kwani inajulikana kuwa JK hakumlinda dhidi ya sakata la RADAR. Kwa hiyo anatafuta fursa ya kulipiza kisasi kwa ajili yake na wenzake.

4. Iwapo hana ajenda ya 2015,

Baada ya hofu juu, nakuomba Bw. Chenge tuache tupumzike na vituko vyako umetupitisha njia ya miba kwa muda mrefu na hivyo tunahitaji angalau kupumua.

Nitashukuru iwapo utaahirisha mpango wako wa kutuvuruga.
 
Back
Top Bottom