Mtumbatu
JF-Expert Member
- Apr 27, 2012
- 362
- 170
Wajumbe wa baraza la wawakilishi wamepitisha makadirio ya mapato ya matumizi ya wizara ya nchi ofisi ya rais utumishi wa umma na utawala bora kwa mwaka wa fedha wa 2012/2013 huku wajumbe hao wakitaka nafasi zaidi za ajira kwa wazanzibari katika serikali ya jamhuri ya muungano.
Pamoja na mambo mengine wajumbe hao walizungumzia kwamba wanahiotaji mgawanyo sawa au angalau asilimia 40 ya nafasi za kazi ndani ya seikali ya muungano. Wajumbe kadhaa walisema nafasi za ajira ndani ya serikali ya muungano ni muhimu ziwe sawa ili kuondosha manunguniko kwa upande mmoja wa muungano.
Wajumbe wa baraza la wawakilishi pia walitaka serikali ya Zanzibar kuondosha michango ambayo inachangishwa kwa vikosi vya ulinzi na polisi michango ya aina mbali mbali na kwamba ni kinyume na sheria za utumishi wa umma kuhusu mishahara.
MMH! YOU WILL SEE OUR TRUE COLOUR NOW