Nafanyaje kama line yangu ilipotea nataka ku-renew ila naona kuna mtu kaisajili kwa jina lake?

chamaclotus

JF-Expert Member
Apr 19, 2019
966
1,927
Inakuwaje waheshimiwa?

Line yangu ya airtel nilipoteza na niko kwenye mpango wa kuchukua loss report ili ni re-new ila tatizo ni kuwa kuna mtu anatumia hiyo namba tayari na naona kaisajili kwa jina lake sio langu tena, sijajua wametumia utaratibu gani.

Nafanyaje wakuu?
 
Kama ilipotea zaidi ya miezi mitatu, inabidi ufahamu kwamba ilifungwa then ikawa haina mtu, then ikawekwa wazi ili isajiliwe.

Line yoyote ambayo haifanyi matumizi ndani ya muda fulani hufungwa then huekwa wazi ili watu wengine waweze kuisajili na kuitumia.
 
Kama ilipotea zaidi ya miezi mitatu, inabidi ufahamu kwamba ilifungwa then ikawa haina mtu...then ikawekwa wazi ili isajiliwe.
Line yoyote ambayo haifanyi matumizi ndani ya muda fulani hufungwa then huekwa wazi ili watu wengine waweze kuisajili na kuitumia.
So niachane nayo mkuu
 
Kwanini wasiwe na utaratibu mtu mwingine asiweze pewa namba iliyosajiliwa hapo zamani?
 
Inaonekana ulichelewa kutoa taarifa ya kupotea. Mitandao karibu yote usipoitumia kadi yao, kwa muda wa miezi 3 wanaiingiza sokoni upya.
 
Number sio mali yako ni mali ya kampuni husika koo ukifa, ukaipoteza kwa mda fulani wao wataiuza kwa mtu mwingine ili waweze kuendelea na biashara.

Koo ww kwako mission accomplish haitakuwa yako tena labda umwombe alie nayo akupe na kukubadilishia usajili inawezekana 100% kafanye makubaliano nae mwenye nayo
 
Inakuwaje waheshimiwa
Line yangu ya airtel nilipoteza na niko kwenye mpango wa kuchukua loss report ili ni renew ila tatizo ni kuwa kuna mtu anatumia hiyo namba tayari na naona kaisajili kwa jina lake sio langu tena, sijajua wametumia utaratibu gani.

Nafanyaje wakuu?
Mimi ilinitokea kwa line yangu ya voda kwakuchelewa kwangu kurenew akawa amepewa mtu mwengine. Nilipoenda voda na kugundua ipo hewani walinishauri niongee nakumuomba huyo mtu afute usajiri wake alafu nijisajiri mimi katika hiyo number. Ni uamuzi wake akubali au akatae na wengine huwa wanahitaji fedha ili kufuta usajiri wake. Ila inawezekana
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom