Habari zenu wakuu kuna hali huwa inanitokea ya kufananishwa na watu tofauti tofaut wengine nawafaham na nisio wafaham, nimeona nije nishee hapa pengine kuna jambo ila mi ndo silijui,
Nitaweka kumbukumbu kwa uchache ambazo hata mimi zilishangaza japo matukio ni mengi ya kufananishwa.
Kuna siku kuna jamaa nafahamiana nae kapita dukani kwangu akaniambia duh mara usharudi?nikamuuliza kutoka wapi?akaniambia ww si tumekutana kariakoo wwe ulikuwa unaenda mimi narudi na tulisalimiana ila juu kwa juu ndomana nashangaa nimekukuta hapa!siku hiyo mi sijatoka kwenda kokote nikamwambia lakin jamaa hakuamin, nikamuuliza nguo hizhizi nimevaa? akajibu hapana ila ni wewe ikabid nimwache tu.
Kuna kipindi nilikuwa nakula kaya (bangi)sasa siku hiyo nipo maskani nakula kuku moshi ghafla wakaingia watu watatu hatuwafaham, vijana wanawaita vidali au mbavu tukataka kukimbia tukijua askar jamaa wakatwambia msikimbie kuna mtu tunamtafuta amemkaba ndugu yetu.
jamaa wakaanza kutukagua mmoja baada ya mmoja ghafla alokabwa akanipoint mimi wakati najua michezo hiyo sina kabisa, moyo ulilipuka paa! jamaa wakaniambia simama juu nilivyosimama jamaa akasema dah sio huyu ila wanafanana sura yule alikuwa mrefu halafu mbavu huyu mfupi, Ndo ikawa pona yangu.
Nyingine nipo sehem nimesimama naongea na jamaa yangu nikaguswa bega kwa nyuma ikabidi nigeuke alikuwa mzee wa makamo nikamwamkia akanijibu kisha akaniuliza kazi yangu umemaliza?nikamuuliza kazi gani mbona sikufaham?akawa kama kaduwaa akiniangalia vizur kisha akajibu samahani nimekufananisha kuna kijana mmefanana sana.
Kuna siku kaja jamaa dukani kwangu akanisalimia john vp nikamwambia poa akauliza siku hiz umehamia dar? nikamwambia mi maisha yangu yote nipo hapa halafu mi sio john kwani vp ?akaniuliza kama nna undugu naye john wa Arusha nikamwambia hapana akasema basi jamaa yuko hivyohivyo.
kuna demu nae kashawah sema alikuwa na x wake anafanana sana na mimi jamaa wakawa wanasema amenikubali anataka kupigwa mkia lakin mi nilijua itakuwa kweli manake dem hakuwa na shobo zozote kusema labda kanipenda.
Juzi wamekuja wadada Ndio nikaona nishee na matukio yaliyopita hawa hawakuniambia kitu ila walioneshana kisha wakasema mmh! Wamefanana sema huyu mweupe sana tutamwambia aje amuone pacha wake.
Je kuna anaekutana na hali hii?manake kwa upande mwingine kama ni hatar naweza fananishwa na jambazi nikauwawa.
Eti wanasema bhangi zangu! wakati hii ni kweli kama unavyosema kuna mtu anakuja anakuletea stor inabid nawewe ujifanye unamjua tu mamake ukimuuliza imakuwa bado humfaham, nashukuru mkuu kumbe sio peke yangu ni hali ya kawaida tuHii hali ya kufananishwa huwa inanikuta sana tokea utotoni. Mbaya zaidi nafananishwa mpaka na watoto wa watu wanajua mimi ndio mzazi. Kuna kipindi nilikua mboka manyema kuna jamaa aliniganda sana kuwa tumekutana Kigoma hali mimi sijawahi kukanyaga kigoma. Town nishafananishwa na watu kama 30 hivi na ushekhe mpaka saaa nishazoea. Kuna watu huwa napiga map story tu kwa kunifananisha na mi naunga humo humo.
Nimefananishwa sana na mbaya zaidi mikoa tofauti si kwa mchaga si kwa msukuma si kwa mmanyema wala mzaramo...
Kukazia zaidi kuna jamaa nilisoma nae form 1 mpaka 4 watu wakawa wanatuchanganya. Mwingine nilisoma naye elimu nyingine vile vile na cha ajabu yule wa 4 na huyu wa elimu nyingine hawafanani...
Siku hizi ukinifaninisha sikatai nasubiri ushtuke mwenyewe. Kuna siku nitakula bingo ya mtu wacha waendelee.
Eti wanasema bhangi zangu! wakati hii ni kweli kama unavyosema kuna mtu anakuja anakuletea stor inabid nawewe ujifanye unamjua tu mamake ukimuuliza imakuwa bado humfaham, nashukuru mkuu kumbe sio peke yangu ni hali ya kawaida tu
Hayo mambo ya nyota sijawahi kufatilia naona kama usanii sijui nina nyota gani.
Ndo nini hiyo ibilisiUna nyota ya punda au mashuke huwa inawatokea sana watu wa nyota hiyo