Nadharia ya demokrasia ndani ya CHADEMA na ukomo wa kipindi cha Uenyekiti

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,316
24,181
Ni kiherehere changu tu kujiuliza swali la kimsingi kabisa la demokrasia ndani ya CHADEMA. Mimi si mwanachama wa chama hiki cha upinzani lakini ndio chama rasmi kinachoongoza kambi ya upinzani bungeni.

Sasa hivi CHADEMA wamo katika mchakato wa uchaguzi ndani ya chama na kati ya vinyang'anyiro ni uchaguzi wa Mwenyekiti. Kati ya majina yanayofikiriwa ni kumrudisha tena kwa mara nyingine Freeman Mbowe.

Huu ni usultani! Huwezi kuendesha demokrasia kwa kuwa na Mwenyekiti yule yule, timu ile ile, na uongozi ule ule katika upinzani, halafu tukajidai watatetea demokrasia ya nchi. Kama CHADEMA hawawezi ndani ya chama chao kurekebisha katiba kuweka ukomo wa uenyekiti, mtu anajiuliza kwa Taifa je? Si ni yale yale?

Kimsingi kutobadilisha katiba ili kuweka ukomo wa madaraka sababu yake ni kuendeleza ulaji. Wakati CCM wamebadili wenyeviti mara kadhaa ndani ya miongo miwili, upinzani majina ni yale yale; Mbowe, Maalim Seif n.k.

Dhana ya demokrasia haionekani ndani ya vyama vya upinzani. Ni unafiki kufikiri watatetea katiba mpya kitaifa pindi wakipata madaraka.

=====
Maoni ya wachangiaji
(MODS hapa mmeingilia uhuru wangu wa maoni. Ieleweke na wachangiaji kuwa hii quote sijai attach mimi)

Mkuu naomba utofautishe matakwa ya katiba yaliyopo katika vyama tofauti vya siasa. Kila chama kina mila na desturi zake katika uendeshaji wake ili likapate kufikia malengo yake yaliyowekwa na itikadi kinayoisimami.

Huwezi kufananisha uendeshaji wa masuala ya kichama yaliyopo ndani ya vyama kwa kuingalia CCM kama role model katika mazingira ya kisiasa yaliyopo hivi sasa. TANU yenyewe katika uchanga wake kiliongozwa na Mwl. Nyerere kwa muda mrefu tu.

Kwa hiyo basi vyama hivi vilivyoanzishwa miaka ya 1990's bado vinahitaji "nurturing" kupitia viongozi wazoefu kutokana na changamoto zilizopo. Kwa hiyo basi bado CHADEMA inamuhitaji Mh. Mbowe katika nafasi hiyo ili kisiweze kuwa "derailed" na rafu za kisiasa zilizopo hivi sasa.
 
Mkuu naomba utofautishe matakwa ya katiba yaliyopo katika vyama tofauti vya siasa. Kila chama kina mila na desturi zake katika uendeshaji wake ili likapate kufikia malengo yake yaliyowekwa na itikadi kinayoisimami.

Huwezi kufananisha uendeshaji wa masuala ya kichama yaliyopo ndani ya vyama kwa kuingalia CCM kama role model katika mazingira ya kisiasa yaliyopo hivi sasa. TANU yenyewe katika uchanga wake kiliongozwa na Mwl. Nyerere kwa muda mrefu tu.

Kwa hiyo basi vyama hivi vilivyoanzishwa miaka ya 1990's bado vinahitaji "nurturing" kupitia viongozi wazoefu kutokana na changamoto zilizopo. Kwa hiyo basi bado CHADEMA inamuhitaji Mh. Mbowe katika nafasi hiyo ili kisiweze kuwa "derailed" na rafu za kisiasa zilizopo hivi sasa.
 
Kuna katiba ya chama cha siasa na kuna katiba ya nchi.

Kufuata katiba ya chama cha siasa ni hiari kwa maana ni hiari ya mtu kujiunga nacho.

Kufuata katiba ya nchi ni lazima si hiari ya mtu.

Ukiiona tofauti, utajua maana. Je katiba ya CCM ina ukomo kwenye nafasi ya Mwenyekiti?
 
Kuna katiba ya chama cha siasa na kuna katiba ya nchi.

Kufuata katiba ya chama cha siasa ni hiari kwa maana ni hiari ya mtu kujiunga nacho.

Kufuata katiba ya nchi ni lazima si hiari ya mtu.

Ukiiona tofauti, utajua maana. Je katiba ya CCM ina ukomo kwenye nafasi ya Mwenyekiti?
CHADEMA ingeiga hata 10% ya utaratibu wa ukomo wa uongozi katika CCM, wangekuwa mbali.
 
Mbowe ndie ameshindwa kusoma alama za nyakati. Anafikiri ataendelea kupendwa tu muda wote. Yeye na wafuasi wake wanapumbazana. Wamesahau kilichowatokea viongozi mbalimbali waliokuwa wanadhani wanapendwa mwishowe wakaondolewa kwa aibu. Wadadisi tunaendelea kutahadharisha.
 
Mbowe ndie ameshindwa kusoma alama za nyakati. Anafikiri ataendelea kupendwa tu muda wote. Yeye na wafuasi wake wanapumbazana. Wamesahau kilichowatokea viongozi mbalimbali waliokuwa wanadhani wanapendwa mwishowe wakaondolewa kwa aibu. Wadadisi tunaendelea kutahadharisha.
Marupu rupu ya Usultani yatawavutia wengi ili na wao wayapate.
Principles za uongozi zimewapiga chenga CHADEMA.
 
Kama CHADEMA hawawezi ndani ya chama chao kurekebisha katiba kuweka ukomo wa uenyekiti, mtu anajiuliza kwa Taifa je? Si ni yale yale?
Nakuunga mkono, LAKINI kwa dhamira kuu ya Magufuli kuua upinzani,hotuba yake ya 2.5/2016 ??? ngoja top management ibaki! Naomba Mboqe abaki. Maana it is true kuwa Jiwe yuko bussy kuweka mamluki. Kuna watu wanaaminika, wako tayari kufa kwa ajili ya CDM, hao acha wabaki. Vinginevyo nakubalian na wewe Mbowe ilibidi aondoke apishe wenginwe. Ingelikuwa wakati wa Kiwete, Mbowe ilibidi aondoke. Unalisemeaje hilo?
 
Nakuunga mkono, LAKINI kwa dhamira kuu ya Magufuli kuua upinzani,hotuba yake ya 2.5/2016 ??? ngoja top management ibaki! Naomba Mboqe abaki. Maana it is true kuwa Jiwe yuko bussy kuweka mamluki. Kuna watu wanaaminika, wako tayari kufa kwa ajili ya CDM, hao acha wabaki. Vinginevyo nakubalian na wewe Mbowe ilibidi aondoke apishe wenginwe. Ingelikuwa wakati wa Kiwete, Mbowe ilibidi aondoke. Unalisemeaje hilo?
Mkuu hayo yalisemwa sana hata wakati wa Awamu ya Nne.

Principle no 1: Kiongozi akibaki madarakani muda mrefu, hakuna ubunifu wowote kiuongozi.
Priple no 2: kioghozi huyo anarudi na watu wale wale
Principle no 3: Its business as usual.
 
Mkuu hayo yalisemwa sana hata wakati wa Awamu ya Nne.

Principle no 1: Kiongozi akibaki madarakani muda mrefu, hakuna ubunifu wowote kiuongozi.
Priple no 2: kioghozi huyo anarudi na watu wale wale
Principle no 3: Its business as usual.
Yote uliyoandika ni sawa kabisa! Awamu ya nne, Kikwete hakuapa, haadharani au kuonyesha dhamira ya kuua upinzani. Kweli muda ule ilibidi Mbowe aondoke. Lakini kwa sasa ndani ya magufuli, hapana! hapana!
Nakusubiri , maana nina uhakika 100% Magufuli atabadili katiba aongoze milele! Nitakusubiri urudi unieleze!
 
Jidu La Mabambasi, Nadhani wewe wewe ni mweupe kuhusu demokrasia....

Democracy is all about makubaliano ya watu wengi...

Dictatorship is all about matakwa ya mtu mmoja....
Kwa hiyi mtaalam.
Sisi CCM tukikubaliana JPM akae madarakani na afanye vitu vyake vya maendeleo chanya kama tunavyoona , si itakuwa demokrasia vile vile?
 
Kwa hiyi mtaalam.
Sisi CCM tukikubaliana JPM akae madarakani na afanye vitu vyake vya maendeleo chanya kama tunavyoona , si itakuwa demokrasia vile vile?

..Jpm na wana-ccm wanaweza kubadilisha katiba ya chama chao.

..katiba ya nchi Uraisi ni miaka 5, na inaruhusiwa kugombea vipindi viwili.

..kubadilisha katiba ya nchi inahitaji MUAFAKA WA KITAIFA.
 
Back
Top Bottom