G-Mdadisi
Senior Member
- Feb 15, 2018
- 157
- 99
Migogoro ni hali inayotokana na mvutano unaosababishwa na hisia, kauli, vitendo, maono na maslahi na kupelekea kutofautiana mtu na mtu, chama na chama, Dini na dini.
Migogoro hutokea pale ambapo wawili au zaidi huamini katika masilahi kinzani. Katika mgogoro kuna matokeo chanya na hasi. Matokeo hasi ni kusababisha uvunjifu wa amani kwa kuchochea vurugu, na matokeo chanya migogoro ni chanzo cha fursa.
Migogoro sio vurugu na wala vurugu si migogoro kwasababu migogoro ni asili (natura), ni kawaida (normal) na pia ni kati kwa kati (neutral). Kimsingi migogoro haiwezi kuepukika katika maisha ya binaadam kwa hali yoyote ile ila tu kinachoweza kuepukika ni vurugu zinazotokana na migogoro.
Migogoro isiposhughulikiwa kwa wakati au ikishughulikiwa kwa upendeleo ndiyo huzaa vurugu.
Migogoro hutokea pale ambapo wawili au zaidi huamini katika masilahi kinzani. Katika mgogoro kuna matokeo chanya na hasi. Matokeo hasi ni kusababisha uvunjifu wa amani kwa kuchochea vurugu, na matokeo chanya migogoro ni chanzo cha fursa.
Migogoro sio vurugu na wala vurugu si migogoro kwasababu migogoro ni asili (natura), ni kawaida (normal) na pia ni kati kwa kati (neutral). Kimsingi migogoro haiwezi kuepukika katika maisha ya binaadam kwa hali yoyote ile ila tu kinachoweza kuepukika ni vurugu zinazotokana na migogoro.
Migogoro isiposhughulikiwa kwa wakati au ikishughulikiwa kwa upendeleo ndiyo huzaa vurugu.