Nadhani katiba mpya inahitajika haraka!

mtundu27

Member
Jul 17, 2018
78
123
Habarini wadau. Natumai mmeamka salama na mmeanza shughuli za kujiongezea mapato.

Nadhani hii nchi ilipofika kuna uhitaji mkubwa wa katiba mpya itakayopunguza nguvu za urais pamoja na kumfanya kila mtanzania kujihisi yuko huru kwenye nchi yake.

Nasema haya sababu mambo yanayoendelea yanaumiza pamoja na kufedhehesha. Tumemsikia juzi juzi mwenyekiti wa uvccm akitoa kauli za ajabu kabisa, zenye kuleta ubaguzi wa wazi lakini si polisi wala msajili aliyekemea.

Juzi kajiuzulu waitara jana ndugai kwa haraka kashapokea barua kama ile ya lipumba kuhusu wabunge, hivi haki iko wapi? Majibu kuhusu kushambuliwa kwa lissu hadi leo hatujasikia aliyekamatwa.

Jana tena mbunge wa monduli kajiuzulu kisa kuunga mkono juhudi za rais, mimi nadhani mtu akijiuzulu kwasababu hiyo, kwanza hilo jimbo ateuliwe tu mtu wa chama alichotoka mpaka uchaguzi mkuu maana haya mambo si sawa, waitara kajiuzulu akisema alihoji matumizi ya ruzuku ya 237milioni kwa mwezi akatishwa, huku akisahau kujiuzulu kwake na kuitisha uchaguzi mpya ni zaidi ya bilioni 2.

Rais anasema anapigania watanzania wa hali ya chini na maendeleo hayana vyama, hizi kauli zinafika mahali zinakwaza tu. Matumizi ya trilioni na nusu hayajulikani, matumizi ya chato hamna anayehoji, kila mtu kimya maana ukiongee wata 'ku pyu pyu' ila wao ni ruksa kufanya chochote. Ifike mahali tuheshimu utu pamoja na kudai katiba mpya.

Karibuni tujadiliane
 
Last edited by a moderator:
Kama tulishindwa wakati wa Jakaya, Basi awamu hii tarajia kuitwa mchochezi iwapo utasikika ukizungumzia "katiba mpya"
 
Katiba mpya sio kitu kwani ikiwa mpya haiwezi kuvunjwa?
Inaweza kuvunjwa, Ila kama nguvu ya anayevunja si kubwa sana inakuwa ngumu sana kuivunja. Ukiweka uzio nyumbani kwako haimaanishi kwamba hutaibiwa, Ila mwizi/kibaka itabidi aruke ukuta. Ukiweka na nyaya za umeme juu unazidi kumpa wakati mgum kibaka au mwizi. We sema unajuaje kama kweli unataka katiba mpya? Tukishamuondolea raisi nguvu, tunampa nani hiyo nguvu na huyo tunayempa nguvu aliyonayo sasa anaitumiaje? Hii iliyopo ni kweli haiheshimiwi? Kama ni kweli, sababu ni nguvu ya kikatiba za asiyeiheshimu au ni udhaifu wa matumizi ya nguvu za kikatiba walizopewa mihimili mingine? Inawezekana tatizo lipo kwa hii mihimili mingine, labda si katiba. Kwa hiyo hata ukiwaongezea nguvu bado wasitumie hiyo nguvu. Anyway Sijajua bado kama tunajua tunataka nn, nafasi ya katiba mpya tulikuwa nayo awamu iliyopita.
 
Inaweza kuvunjwa, Ila kama nguvu ya anayevunja si kubwa sana inakuwa ngumu sana kuivunja. Ukiweka uzio nyumbani kwako haimaanishi kwamba hutaibiwa, Ila mwizi/kibaka itabidi aruke ukuta. Ukiweka na nyaya za umeme juu unazidi kumpa wakati mgum kibaka au mwizi. We sema unajuaje kama kweli unataka katiba mpya? Tukishamuondolea raisi nguvu, tunampa nani hiyo nguvu na huyo tunayempa nguvu aliyonayo sasa anaitumiaje? Hii iliyopo ni kweli haiheshimiwi? Kama ni kweli, sababu ni nguvu ya kikatiba za asiyeiheshimu au ni udhaifu wa matumizi ya nguvu za kikatiba walizopewa mihimili mingine? Inawezekana tatizo lipo kwa hii mihimili mingine, labda si katiba. Kwa hiyo hata ukiwaongezea nguvu bado wasitumie hiyo nguvu. Anyway Sijajua bado kama tunajua tunataka nn, nafasi ya katiba mpya tulikuwa nayo awamu iliyopita.
 
Upo sahihi mkuu, nilitegemea upinzani wafikirie na wapiganie zaidi suala la katiba mpya kuliko hata uchaguzi wa 2020, ni upuuzi wa kiwango cha juu mno kufikiria kuiondoa CCM madarakani kwa katiba hii tuliyonayo, yani ni upuuzi kweli kweli.
 
Hivi kama katiba ya zamani wameshindwa kuiheshimu itawezakana vipi kwa hiyo mpya?
Watakapoona watu wameidai kwa nguvu hata ikistahili damu kumwagika, heshima itakuwepo, si hii ya kutumia hela za walipa kodi kukandamiza wapinzani, kuwanunua, kurudia uchaguzi na kufanya mambo nje ya bajeti as if bunge ni hewa.
 
Watakapoona watu wameidai kwa nguvu hata ikistahili damu kumwagika, heshima itakuwepo, si hii ya kutumia hela za walipa kodi kukandamiza wapinzani, kuwanunua, kurudia uchaguzi na kufanya mambo nje ya bajeti as if bunge ni hewa.
Damu ya nani hiyo unayosema imwagike?
 
Ndio. Kwa mawazo yangu bado Sijajua tunataka nn. Hapa naongelea watanzania bila kujali chama. Tz kuna pande kubwa mbili. Kuna upande wao wanalaumu kila lifanywalo na serikali ya ccm, na kuna upande wao wanatetea hata makosa as long yamefanywa na serikali ya ccm. Raisi akisema sasa tuwe na Katiba mpya, usishangae wanaosema katiba si kipaumbele wakasema ni kipaumbele kweli kweli. (Hapa katiba tu). Na waliokuwa wanasema tunahitaji katiba wakabadilika, yaan ni vurugu tupu hapa kwetu.
 
Habarini wadau. Natumai mmeamka salama na mmeanza shughuli za kujiongezea mapato.

Nadhani hii nchi ilipofika kuna uhitaji mkubwa wa katiba mpya itakayopunguza nguvu za urais pamoja na kumfanya kila mtanzania kujihisi yuko huru kwenye nchi yake.

Nasema haya sababu mambo yanayoendelea yanaumiza pamoja na kufedhehesha. Tumemsikia juzi juzi mwenyekiti wa uvccm akitoa kauli za ajabu kabisa, zenye kuleta ubaguzi wa wazi lakini si polisi wala msajili aliyekemea.

Juzi kajiuzulu waitara jana ndugai kwa haraka kashapokea barua kama ile ya lipumba kuhusu wabunge, hivi haki iko wapi? Majibu kuhusu kushambuliwa kwa lissu hadi leo hatujasikia aliyekamatwa.

Jana tena mbunge wa monduli kajiuzulu kisa kuunga mkono juhudi za rais, mimi nadhani mtu akijiuzulu kwasababu hiyo, kwanza hilo jimbo ateuliwe tu mtu wa chama alichotoka mpaka uchaguzi mkuu maana haya mambo si sawa, waitara kajiuzulu akisema alihoji matumizi ya ruzuku ya 237milioni kwa mwezi akatishwa, huku akisahau kujiuzulu kwake na kuitisha uchaguzi mpya ni zaidi ya bilioni 2.

Rais anasema anapigania watanzania wa hali ya chini na maendeleo hayana vyama, hizi kauli zinafika mahali zinakwaza tu. Matumizi ya trilioni na nusu hayajulikani, matumizi ya chato hamna anayehoji, kila mtu kimya maana ukiongee wata 'ku pyu pyu' ila wao ni ruksa kufanya chochote. Ifike mahali tuheshimu utu pamoja na kudai katiba mpya.

Karibuni tujadiliane
Mkuu, nakubaliana na hoja yako kwa asilimia mia moja....hali ni tete Tanzania kwa sasa na kama hakuna katiba itakayoweka maslahi ya Taifa mbele hali itaendelea kuwa mbaya zaidi! Watanzani tunahitaji kubadilika, hii katiba ni kwa ajili ya watu wote na si kwa maslahi ya chama au kikundi fulani.
 
Back
Top Bottom