NACTE kuna tatizo kwenye suala la usimsmizi wa mitihani

kibaravumba

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
6,636
7,005
Mitihani ya vyuo vinavyosimamiwa na NACTE husimamiwa na wasimamizi wa nje wanaotoka vyuo tofauti.Hili ni jambo zuri.Ila zipo changamoto zilizotengenezwa maksudi ama kwa kutokujali zinazofanya usimamizi huu uwe duni kabisa.
Kwanza kitendo cha kupanga msimamizi yule yule katika kituo kimoja kila mwaka.
Jambo hili lina madhara makubwa na athari kwa ubora kwani baadhi wamekuwa hawana maadili kiasi kwamba wanashirikiana na wamiliki kusaidia wanafunzi ili wafaulu.Kuna mashaka makubwa kuwa wanachukua mlungula na hakuna ufuatiliaji wa karibu kwenye suala hili.
Baadhi kutaka kushiriki ngono na baadhi ya watoto wa kike na wanaokataa wanatishwa kwani kila mwaka anatarajiwa kurudishwa katika chuo kile kile kuwa msimamizi.
Pamoja na mitihani kuwekewa utaratibu wa udhibiti lakini upo uwezekano wa baadhi ya vyuo kuwa huwa wanapata mitihani au baadhi ya maswali ya mitihani hiyo.
Je kwa nini usiwekwe utaratibu wa udhibiti kama mitihani ya NECTA?
Mimi nawapa tahadhari tu maana tayari tumeanza kuona dalili mbaya ambazo zinahitaji hatua za umakini zichukuliwe.
Si vema kufanya kazi kwa mazoea,au mnaweza kuleta sintofahamu isiyo ya lazima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una uhakika gn kua NECTA wana usimamizi mzuri kwenye mitihani?
Au kwa sababu hubadilisha vituo kila mwaka ndio unaona wako vzr??
 
Una uhakika gn kua NECTA wana usimamizi mzuri kwenye mitihani?
Au kwa sababu hubadilisha vituo kila mwaka ndio unaona wako vzr??
Mitihani ya NECTA imedhibitiwa kwa kiasi kikubwa.Nawapongeza kwa hili japo changamoto hazikosekani.Na imekuwa ni rahisi hata kugundua iwapo kuna changamoto imejitokeza
Huko NACTE bado kuna shida kubwa sana.Hakuna umakini na wakati mwingine kuna uzembe wa maksudi unafanywa na hapa unaona kabisa kuna watu wanafaidika na mfumo huu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
We unajua ugum wa iyo mitihan kwanza,kunamitihan mingine inakuja tofauti na mtaara kabsa so njia mubadala lazma itumike bn bila ivo nakwambi watu lazma kila chuo wamalize 10 wakienda zaid 15
 
Naona hapo umelenga sana vyuo vya private ila kiukweli kwenye maswala ya elimu yanayohusu afya ya binadam lazima serikalk iangalie tusijepata matabibu vilaza zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We unajua ugum wa iyo mitihan kwanza,kunamitihan mingine inakuja tofauti na mtaara kabsa so njia mubadala lazma itumike bn bila ivo nakwambi watu lazma kila chuo wamalize 10 wakienda zaid 15
Naamini ndiyo maana watanzania wengi tu wababaishaji.Kwani wanaotunga mitihani wanakuwa na nia gani kuleta vitu nje ya mtaala?
Jawabu nionavyo kwa mtazamo wangu,huu ubabaishaji ili uishe,ni kwa NACTE kuwa makini na kazi yao.
Mara nyingi tunaona wanafanya vitu kwa kikomoa ili watengeneze tatizo,na wenye kujaribu kulitatua kwa "njia mbadala" huenda wanawa
faidisha baadhi yao huko NACTE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naamini ndiyo maana watanzania wengi tu wababaishaji.Kwani wanaotunga mitihani wanakuwa na nia gani kuleta vitu nje ya mtaala?
Jawabu nionavyo kwa mtazamo wangu,huu ubabaishaji ili uishe,ni kwa NACTE kuwa makini na kazi yao.
Mara nyingi tunaona wanafanya vitu kwa kikomoa ili watengeneze tatizo,na wenye kujaribu kulitatua kwa "njia mbadala" huenda wanawa
faidisha baadhi yao huko NACTE

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeonge sahihi kabsa mkuu naona kuna kiac wanapata maana kwa mfano vyuo vya private mtu akiwa na sup inabid alipe laki4,ebufikili hicho kitu naukichek mwaka Jana sup ziko kama njugu Tz nzima yan nishida tupu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom