NACTE Ingilieni Kati Huu ni Wizi wa Wazi Wazi

Sagungu 1914

JF-Expert Member
Jun 21, 2016
930
579
Ninaomba nacte mutasaidie kuhusu huu wizi wa baadhi ya vyuo vya private,kwani miongoni mwao wameandikia wanafunzi waende kuripoti na pesa ya majengo(Building contibution).Sasa mimi nauliza hawa wamiliki wa chuo husika inakuaje uanzishe chuo bila kuwa na majengo ya kutosha?,na inakuaje NACTE wasajili chuo ambacho hakina majengo ya kutosha kwa ajili ya wanachuo?.Mfano wa chuo kinachotaka wanafunzi waende na LAKI MOJA kwa ajili ya ujenzi wa majengo ni "Shirati school of nursing" kilichopo Rorya-Mara.Je huu si wizi wa wazi wazi?.
 
Yaani mkuu ukiangalia joining instruction yao ilivyojaa "ujanjaujanja" mwingi unatamani hata usimpeleke mtoto shule.Halafu wanajiita watu wa Mungu ambao wanataka sisi wazazi ndio tuwajengee chuo kwani imekua shule ya kata hiyo?.
 
Hivyo vyuo uchwara mnavichagua vya nini? Mi siwezi fikria kupeleka mtoto wangu kwenye hivyo vyuo aisee
 
Hivyo vyuo uchwara mnavichagua vya nini? Mi siwezi fikria kupeleka mtoto wangu kwenye hivyo vyuo aisee
Chuo chochote ni chuo uchwara endapo mwanaafunz atakuwa amefaauulu vizuuri na kuwa na uhakika wa kupata chuo kizuri au mwanafunz ambae anauhakika mzazi wake anauwezo wa kumlipia chuo chochote kizuri... lakin kwa mwenya ufaulu wa wastani na mzazi uwezo hana lazima mtu ataona kinamfaa.... tusizarau chuo ilihali kimesajiliwa... semaa tu matatizo madog madog yanakuwepo ya kuyasemea yarekebishwe...
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom