Opportunity Cost
JF-Expert Member
- Dec 10, 2020
- 9,035
- 6,907
Ndivyo ilivyo siku zote mbonaWale Mliosoma IFm,Cbe na Arusha Tech Pokeeni Hii Taarifa Wakuu.
----
Dkt. Geofey Oleke - Mkurugenzi wa Udhibiti, Tathmini na Ufuatiliaji NACTE amesema haya
Watu huwa wanachanganya kati ya NECTA Na NACTE kwa sababu ya maneno kushabihiana NACTE ni baraza la Taifa la elimu ya Ufundi wakati NECTA ni baraza la Mitihani la Taifa. Sisi kazi yetu ni kusajili vyuo na kuangalia ubora katika vyuo vya elimu ya kati, ni vyuo ambayo sio vyuo vikuu ambayo vinatoa ngazi ya cheti, diploma, degree mpaka degree za juu.
Vyuo ambayo sio vyuo Vikuu ni IFM, CBE, Arusha Tech., hizi ni taasisi za elimu zinatoa ngazi ya cheti hadi Masters vyote vipo chini na NACTE.
Vyuo vikuu vyote vipo chini ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kama UDSM, UDOM na vingine.
Tupo kwenye msimu wa Udahili na kawaida kabla ya wanafunzi kwenye vyuoni kuripoti wanafanyiwa uhakiki.
Wanafanya maombi kwenye vyuo vyao halafu baadaye vyuo vinaleta majina ya wanafunzi wote wanaotakiwa kusajiliwa ili sifa zao zifanyiwe uhakiki kwa mfano unataka kusoma program ya afya kumbe hauna vigezo vya kusoma kazi yetu kubwa kama baraza ni kuangalia ubora tumeshafanya kwenye program ya afya kwenye vyuo vya Serikali kwenye vyuo vingine mchakato unaendelea umeanza tarehe 5 kuangalia sifa za wanafunzi vyuo vyote vimeleta majina ya wanafunzi wao. Hii kazi itakwenda mpaka tarehe 15 September