Nabii 'mtoto' Daniel Daniel Shilla aliyetikisa Dar kwa mkwanja afutiwa usajili wa kanisa

MLAU

JF-Expert Member
Aug 23, 2007
4,726
3,354
nabii-daniel-shilah-4.jpg

KIONGOZI wa Kanisa la Bethel Ministry nchini, Nabii Daniel Daniel Shilla, amefutiwa usajili wa huduma hiyo kwa madai ya kujihusisha na siasa.

Shilla ambaye ana umri wa miaka 22, kanisa lake limekuwa gumzo kutokana na staili yake ya mavazi, nywele na maisha yake kwa ujumla kwa mfano kwenda kwenye kumbi za starehe na kugawa fedha mtaani na kwa waumini wake, amefutiwa usajili huo kwa madai ya kumtabiria ushindi mgombea wa chama cha upinzani katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa Jimbo la Kinondoni, uliofanyika Februari 17, mwaka huu.

Nabii Shilla ambaye kanisa lake limesajili chini ya mwavuli wa Kanisa la Great Revival Mission Christian linaloongozwa na Askofu Peter Mlai, alisema taarifa ya kufungiwa huduma hiyo alipatiwa na Askofu aliyemfanyia usajili huo kwa malalamiko ya kwamba amekuwa akijihusisha na siasa.

Nabii Shilla pasipo kufafanua, alisema kabla ya kupatiwa taarifa hizo alikuwa akifuatiliwa na Serikali kwa takribani wiki mbili.

“Askofu wangu aliniambia amesumbuliwa sana na Serikali, ninajihusisha na siasa nikamwambia nimejihusishaje na siasa mbona sihubiri siasa, akaniambia uchaguzi wa Kinondoni uliposti kwenye akaunti yako kwamba mshindi atatoka upinzani na ni kweli maana mpaka sasa sijafuta kwa sababu sio binadamu ni Mungu ndiye amenionyesha.

“Mimi nasema niliongozwa na Mungu kwa sababu sijasema ni uhakika wala sijatangaza kisheria kama wameshinda upinzani, ni haki yangu kikatiba kwa sababu mimi nilikuwa mtumishi wa Mungu, ni mchungaji ni prophet (nabii) kwa wakati ule nilikuwa na kibali kwanini wameenda kumtishia Bishop (Askofu)?” alihoji Nabii Shilla.

Alisema haamini kama sababu hiyo inatosha kumzuia kutoa huduma hiyo ya kiroho kwa kuwa yeye ni mtu wa maombi na kila anachoongea kinakuwa kimetokana na maombi aliyoyafanya.

Alisema askofu huyo alimweleza kuwa amechukuwa hatua hiyo ili aweze kuokoa huduma yake kwa kuwa amekuwa akisumbuliwa na Serikali.

Shilla pia alionyesha vyeti vitatu vya usajili wa huduma yake, alisema ameamua kuweka wazi suala hilo ili Watanzania wajue kwa sababu pia anahofia usalama wake.

“Nimeweka hivi ni kwa usalama wangu, kama nafanyiwa hivi na Watanzania wasipojua naweza nife hata kesho nikaokotwa kwenye kiroba, katika kitu kibaya ambacho Serikali wasiguse watumishi wa Mungu mimi sijawahi kuipinga Serikali, huwa namwombea Magufuli (Rais Dk. John Magufuli), Mkuu wa Mkoa, chama tawala, wapinzani na Watanzania wote,” alisema Nabii Shilla.

Alisema yeye ni nabii wa ukweli hivyo hawezi kukaa kimya akiona kama kuna kifo cha Mtanzania aliyepigwa risasi na akifanya hivyo atakuwa mtumishi wa uongo.

“Nabii wa ukweli anaitabiria Serikali au nabii wa ukweli anaongea kitu anachoongozwa na Mungu, mimi ni nabii wa Mungu simtumikii binadamu ndiyo maana si mwoga,” alisema Nabii Shilla.

Alisema kutokana na hali hiyo, amepata taarifa ya wito wa kwenda mkoani Dodoma kuonana na Msajili wa Vyama na Jumuiya.

Kanisa la Bethel Ministry lenye namba ya usajili 14783, lilisajiliwa Aprili 19, 2008 chini ya mwavuli wa Kanisa la The Great Revival Mission Christianity Church.
nabii-daniel-shilah-7.jpg
 
View attachment 718247
KIONGOZI wa Kanisa la Bethel Ministry nchini, Nabii Daniel Daniel Shilla, amefutiwa usajili wa huduma hiyo kwa madai ya kujihusisha na siasa.

Shilla ambaye ana umri wa miaka 22, kanisa lake limekuwa gumzo kutokana na staili yake ya mavazi, nywele na maisha yake kwa ujumla kwa mfano kwenda kwenye kumbi za starehe na kugawa fedha mtaani na kwa waumini wake, amefutiwa usajili huo kwa madai ya kumtabiria ushindi mgombea wa chama cha upinzani katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa Jimbo la Kinondoni, uliofanyika Februari 17, mwaka huu.

Nabii Shilla ambaye kanisa lake limesajili chini ya mwavuli wa Kanisa la Great Revival Mission Christian linaloongozwa na Askofu Peter Mlai, alisema taarifa ya kufungiwa huduma hiyo alipatiwa na Askofu aliyemfanyia usajili huo kwa malalamiko ya kwamba amekuwa akijihusisha na siasa.

Nabii Shilla pasipo kufafanua, alisema kabla ya kupatiwa taarifa hizo alikuwa akifuatiliwa na Serikali kwa takribani wiki mbili.

“Askofu wangu aliniambia amesumbuliwa sana na Serikali, ninajihusisha na siasa nikamwambia nimejihusishaje na siasa mbona sihubiri siasa, akaniambia uchaguzi wa Kinondoni uliposti kwenye akaunti yako kwamba mshindi atatoka upinzani na ni kweli maana mpaka sasa sijafuta kwa sababu sio binadamu ni Mungu ndiye amenionyesha.

“Mimi nasema niliongozwa na Mungu kwa sababu sijasema ni uhakika wala sijatangaza kisheria kama wameshinda upinzani, ni haki yangu kikatiba kwa sababu mimi nilikuwa mtumishi wa Mungu, ni mchungaji ni prophet (nabii) kwa wakati ule nilikuwa na kibali kwanini wameenda kumtishia Bishop (Askofu)?” alihoji Nabii Shilla.

Alisema haamini kama sababu hiyo inatosha kumzuia kutoa huduma hiyo ya kiroho kwa kuwa yeye ni mtu wa maombi na kila anachoongea kinakuwa kimetokana na maombi aliyoyafanya.

Alisema askofu huyo alimweleza kuwa amechukuwa hatua hiyo ili aweze kuokoa huduma yake kwa kuwa amekuwa akisumbuliwa na Serikali.

Shilla pia alionyesha vyeti vitatu vya usajili wa huduma yake, alisema ameamua kuweka wazi suala hilo ili Watanzania wajue kwa sababu pia anahofia usalama wake.

“Nimeweka hivi ni kwa usalama wangu, kama nafanyiwa hivi na Watanzania wasipojua naweza nife hata kesho nikaokotwa kwenye kiroba, katika kitu kibaya ambacho Serikali wasiguse watumishi wa Mungu mimi sijawahi kuipinga Serikali, huwa namwombea Magufuli (Rais Dk. John Magufuli), Mkuu wa Mkoa, chama tawala, wapinzani na Watanzania wote,” alisema Nabii Shilla.

Alisema yeye ni nabii wa ukweli hivyo hawezi kukaa kimya akiona kama kuna kifo cha Mtanzania aliyepigwa risasi na akifanya hivyo atakuwa mtumishi wa uongo.

“Nabii wa ukweli anaitabiria Serikali au nabii wa ukweli anaongea kitu anachoongozwa na Mungu, mimi ni nabii wa Mungu simtumikii binadamu ndiyo maana si mwoga,” alisema Nabii Shilla.

Alisema kutokana na hali hiyo, amepata taarifa ya wito wa kwenda mkoani Dodoma kuonana na Msajili wa Vyama na Jumuiya.

Kanisa la Bethel Ministry lenye namba ya usajili 14783, lilisajiliwa Aprili 19, 2008 chini ya mwavuli wa Kanisa la The Great Revival Mission Christianity Church.
View attachment 718248
Lilisajaliwa April 2018 mbona hiyo April 2018 haijafika na ndo tupo March 2018
 
Huyu jamaa mimi naona ,serikali walichelewa kumfungia ,yaani alikuwa anaichezea imani ya kikristo.Mavazi,muonekano wake,mikogo unaweza sema ni Mbongo fleva anaenda kutambulisha nyimbo.Tatizo iman ya Kikristo inachezewaa sababu tu tuliambiwa "Tusihukumu",lkn hawa wanaharibu iman ya kikristo kwa kuuweka usasa na swaga.Maswala ya kiimani yanatakiwa kuwa kama yalivyoandikwa hamna kuongeza kitu wala kupunguza.Sometime waislam nawaona wapo serious na iman yao ukizingua tu wazee hawakucheleweshi unachezea mikwaju hapo hapo, upuuzi wako ukaufanyie kwengine lkn si katika imani yao.
 
Kanisa la Bethel Ministry lenye namba ya usajili 14783, lilisajiliwa Aprili 19, 2008 chini ya mwavuli wa Kanisa la The Great Revival Mission Christianity Church.
Kama kwa sasa ana miaka 22 ina maana alisajili kanisa lake akiwa na umri wa miaka kama 11 au 12 hivi.
 
Huyu jamaa mimi naona ,serikali walichelewa kumfungia ,yaani alikuwa anaichezea imani ya kikristo.Mavazi,muonekano wake,mikogo unaweza sema ni Mbongo fleva anaenda kutambulisha nyimbo.Tatizo iman ya Kikristo inachezewaa sababu tu tuliambiwa "Tusihukumu",lkn hawa wanaharibu iman ya kikristo kwa kuuweka usasa na swaga.Maswala ya kiimani yanatakiwa kuwa kama yalivyoandikwa hamna kuongeza kitu wala kupunguza.Sometime waislam nawaona wapo serious na iman yao ukizingua tu wazee hawakucheleweshi unachezea mikwaju hapo hapo, upuuzi wako ukaufanyie kwengine lkn si katika imani yao.
Kama hauna dhambi uwe wa kwanza kupiga mkwaju
 
Back
Top Bottom