Daudi Mchambuzi
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 62,204
- 128,020
Mnamuonea bure tu nabii wa watu yeye alikua anaziombea tu hizo pesa kumbe kati yake kuna noti moja chafu ndiyo gafla moto kutoka mbinguni ukazichoma hizo pesa.
Siku nyingi mkuu..TBC wamepana dau naona..SAM MAHELA kahamia TBC?
Huyu ndio yupi tena .au ni yule aliyeoa kitoto cha miaka tisa .Baada ya nabii Issa(Yesu) kilipita kipind kirefu sana then akaletwa nabii Muhammad (mtume /nabii wa mwsho):
hao wengine wa sasa ni completely FAKE!
Esa ziombewe ili ziongezeke? Jamaa wajinga mno.habari wakuu,
Kwenye taarifa ya habari ya TBC leo usiku wametangaza habari ya nabii Mbugua wa kanisa la CAG kudaiwa kuwatapeli waumini wake. Mchungaji huyo anadaiwa kuagiza waumini wapeleke pesa ili aziombee ziwe nyingi kisha atawarudishia bila kuchukua hata shillingi.
kama mnavyojua ndugu zetu wapenda dini wana kitu kimoja in common (low thinking capacity) nabii kawapiga hela siku aliyowaambia wakachukua kawaambia hela zimungua mlimani alivyokuwa kwenye maombi.
kwa mara ya kwanza namuona huyu nabii kwenye channel ten nilijua tu ni tapeli jinsi anavyofundisha na mavazi yake kavaa kama shehe ana coach watu watoe ushuhuda,
Walokole amkeni mtapigwa na manabii feki mpaka lini acheni kuhangaika hakuna kitu kinachoitwa maombi na miujiza just live your faithful life, wenzenu waislamu wametulia na mtume wao wala hawatarajii hata kamuujiza kokote ni kupambana na maisha na huo ndio uhalisia.
Mambo ya abunuasi na sufuria lake
Hahaha nakueletea pesa uziombee zizaeNjoo nikuombee baby tena uje na libriefcase nimtandike shetani vizuri
TBC, Sam Mahela?Katika taarifa ya habari ya saa 2 usiku TBC kutoka kwa reporter SAM MAHELA, kuwa nabii huyo anayepatikana DAR anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kutapeli fedha waumini wake ambapo waumini wawili wamethibitisha hilo mmoja akitapeliwa laki 6 na mwingine laki 2 eti aliwashawishi wampelekee hela aziombee na baadaye akadai zimeungua na moto.
Binafsi ukiachilia mbali kutokuwakubali hawa wanaojiita manabii,lakini huyu alivuka kiwango cha kutokubalika maana hajui hata kuhubiri kazi yake ni kutoa matumaini tu mazurizuri kwa waumini na kisha kuombea watu na hata kuwataka walishike vazi lake ili kupata baraka kisha inafuata promo ya miujiza.
Nilishaona pale ni 0 lakini nikashangaa kuona watu wanamshangilia na wanajazana kanisani kwake ndipo nilipobaini shida kubwa ya sisi wabongo kwa kupigwa kijinga.
Hakuna cha nabii hapa wala BULLDOZER, MWAMPOSA, MITI MINGI n.k ijapo hawa kwangu wana unafuu kwenye mahubiri yao kwamba si haba wanajitahidi kuwa huwezi toka kapa ila sio mazingaombwe yao ya kuombea.
Mkome.
T B Joshua ndio tapeli la kutupwa...Serikali ya Cameroon wamepiga marufuku wananchi wake kwenda kwa tb joshua kutapeliwa...Huko nyuma ķoote nimeunga mkono ukosoaji wenu kuhusu manabii wa uongo.ILA HILI LA KUMHUSISHA/KUMUUNGANISHA T.B.JOSHUA NA HAO MANABII FAKE, NASEMA NOOO! YES, BIG NOOO..
Huko nyuma ķoote nimeunga mkono ukosoaji wenu kuhusu manabii wa uongo.ILA HILI LA KUMHUSISHA/KUMUUNGANISHA T.B.JOSHUA NA HAO MANABII FAKE, NASEMA NOOO! YES, BIG NOOO..
Teh teh teh.Kama imefikia hatua ya nabii kuwatapeli waumini wake iko siku kila mtu atasali kivyake nyumbani kwake tu!!