Nabii Frank Julius Kiwalah ni nani?

Open school

JF-Expert Member
Jul 13, 2015
458
480
Leo wakati nawasha televisheni yangu ghafla nikakutana na kipindi chake cha uponyaji wa maradhi. Nimeona watu wakitoa shuhuda mbalimbali na wengine wakipokea uponyaji mbele ya camera, nikapata shauku ya kumfahamu huyu mtumishi ni nani maana inaonekana huduma zake si mchezo maana watu wanatoa shuhuda kupona maradhi wanayosema kwamba walishindwa kutibiwa hospitalini.
 
Leo wakati nawasha televisheni yangu ghafla nikakutana na kipindi chake cha uponyaji wa maradhi. Nimeona watu wakitoa shuhuda mbalimbali na wengine wakipokea uponyaji mbele ya camera, nikapata shauku ya kumfahamu huyu mtumishi ni nani maana inaonekana huduma zake si mchezo maana watu wanatoa shuhuda kupona maradhi wanayosema kwamba walishindwa kutibiwa hospitalini.
Mhuni mpiga dili kwa wasiojielewa. Alikuwa na kanisa Tanga-majestic cinema hall. amefukuzwa sijui yuko wapi. Mhuni tu!
 
Mhuni mpiga dili kwa wasiojielewa. Alikuwa na kanisa Tanga-majestic cinema hall. amefukuzwa sijui yuko wapi. Mhuni tu!
Don't judge you will be judged..! Huwa sihukumu watumishi wa Mungu maana walishaniponya kutoka kwenye marogo ya dunia na Nina tabia tu ya kuwa non-judgemental.

Nimeona na bango lake pale Posta kwamba atakuwa na Semina kubwa ya kuvuka Mwaka kuanzia tarehe 27 jijini Dar pale Boko Magengeni..nitahudhuria kusikiliza injili ya bwana.
 
Don't judge you will be judged..! Huwa sihukumu watumishi wa Mungu maana walishaniponya kutoka kwenye marogo ya dunia.
Acha upuuzi huo, hakuna cha kuhukumu hapa. Tumepewa akili tuzitumie. Aende mawodini, Ocean road kuna watu wana cancer aende awaponye tuamini, awaponye watu siyo anadanganya watu mabarabarani, Kuna nyuzi nyingi humu zinamuongelea kama tapeli
 
Wakuu,mhuni?mpiga dil? Etc ndio nini?hebu ongeeni uhalisia ,Kwa mtu asiemjua na anataka kumjua nini maelezo ya ziada
 
Ushaambiwa alikuwa na kanisa na akafukuzwa UNACHOHOJI NI KIPI?

huyo ni mpiga dili sababu dili la kwanza lilibuma ila hili la sasa limewateka vizur wakazi wa Dar ambao wasiokuwa na upeo mkubwa
Dili la kwanza lililobuma ni lipi na lina uhusiano gani na watu kupata uponyaji?
 
Tafuta maana ya mpiga dili! Au wewe ndiye yeye? Nimekuchoma!
Haya umepona kapime ukimwi umepona- stupid! HIV virus anaondoka mwilini kwa kuguswa, stupid, kuwadanganya masikini wagonjwa!
Wewe kama unamfahamu tiririka watu wamjue, hakuna sababu ya kusema ni mpiga dili halafu hutaki kusema namna anavyopiga dili. Huenda unachosema ni kweli maana nimeona namba za mitandao na akaunti za benki kwa ajili ya kuchangia huduma zake lakini vipi ikiwa watu wanaopitia kwake wanapata uponyaji?
 
Dili la kwanza lililobuma ni lipi na lina uhusiano gani na watu kupata uponyaji?
Kama nilivyoandika mwanzo
Dili la kwanza ni huko Tanga

Uponyaji wake huenda watu wanapona ila ndio hawa wanaotumia nguvu za giza

Na ndio mana nikasema hawa ni waganga wa kienyeji sababu kwenye tunguli kumekosa soko ila mfumo wa kutumia kanisa ndio habar ya mjini

HAPA NDIPO KAULI YA YESU INAPOENDELEA KUTIMIA

...nyakati za mwisho watatokea manabii wengi wa uongo na wote watakuja kufanya ishara(uponyaji kutoa pepo) kwa jina langu..
 
huyu jamaa anaponya 100% naaamini alimponya mdogo wangu alikua na kifafa ila sipendi watu wanavyomuabudu kanisani kwake akiingia wote mnampigia magoti hilo halikunifurahisha ila kwasababu nlikua na shida nlipiga na dogo akapona
 
Acha upuuzi huo, hakuna cha kuhukumu hapa. Tumepewa akili tuzitumie. Aende mawodini, Ocean road kuna watu wana cancer aende awaponye tuamini, awaponye watu siyo anadanganya watu mabarabarani, Kuna nyuzi nyingi humu zinamuongelea kama tapeli
Weka link za hizo nyuzi ili tumfahamu.
 
  • Thanks
Reactions: dtj
"nabii wa uongo" ni roho itendayo kazi kwa kasi sana katika dunia ya sasa. (nabii wa uongo sio mtu, bali ni roho iliyo katika watu)

Maandiko yako wazi sana kuhusiana na hili, hasa katika Kitabu cha UFUNUO WA YOHANA.
 
Back
Top Bottom