Naapa kuwa sirudii tena kumsaidia Mtanzania -- never!

Naonaga wakati wa kutoka ndio hata hawaangaliii vizuri, nilihisi hata ukiover stay watakugongea tu exit yani wako busy mno...
Nchi nyingi kutoka siyo issue, nina Family members Marekani passport zao wakitoka huwa hawagongewi hata muhuri wa exit.
 
South Africa ya siku hizi ina watu wema hivyo? Yani umkute mtu analia uende kumuuliza analia nini unamsemesha kizulu then unagunduwa ni Mtanzania unampeleka kwako.

Konda tafadhali nishushe hapahapa nimefika, mwendo wa dereva ni hatarishi.
Hapo ndio niliposhangaa
 
Naonaga wakati wa kutoka ndio hata hawaangaliii vizuri, nilihisi hata ukiover stay watakugongea tu exit yani wako busy mno...
Ukizidisha siku zinasoma kwenye computer hawawezi kuwa busy hivyo lazima wakupige siku za kutosha kutoingia kwao..
 
Na je vipi kuhusu wewe kusaidiwa huogopi?
Napenda kuwa huru na maisha yangu, bila kupangiwa masharti ya maisha.
Misaada mingi ya watu huwa imejaa masharti na manyanyaso lukuki.

Nimekataa dili kibao tu na nafasi kubwa ambazo ni Life Changing...
And truth be told, I have never regretted my decisions......
 
Ukizidisha siku zinasoma kwenye computer hawawezi kuwa busy hivyo lazima wakupige siku za kutosha kutoingia kwao..
Huwa naona kama wao hawafatilii sana
Tofauti na Europe mtu anakagua taratiiibu yani kama vile hamna foleni ya watu inayosubiria huduma hiyo hiyo!!!
 
Kweli mkuu, ndo nimemwambia homeboy fulan hapo juu kuwa wabongo nao sio watu wa kucheza nao. Nimemtolea mfano wa nchi ambazo wapopo wamevamia kwa kasi na kupiga hela ndefu kupitia uzuzu wa raia wa nchi hizo, lkn kwa Tanzania imekuwa tofauti, kila wapopo wanapojaribu kutengeneza chaka ili wapige mpunga kama wapigavyo katika nchi nyingine wabongo ananyea, kila wakijaribu wabongo wananyea hadi wapopo wenyewe wanasanda na kuamua kujisogeza katika nchi zingine za jirani kama vile Kenya, Zambia, Rwanda nk, ambapo pamoja na elimu nzuri ya raia zao, lkn bado nchi hizo zimejaza mazuzu wa kumwaga kwahiyo wapopo wanapata mwanya wa kutengeneza chaka la kupigia hela kupitia raia hao. Wapo wanaopiga hela nchi hizo kupitia mgongo wa kanisa, biashara za halali na haramu, uchenjishaji hela, mambo ya internet nk. Hapa Kaburu ukitoa dili la kwenda kupiga mchomoko usiku katika sehem hatarishi basi utapata 70% ya wabongo ambao wako tayari kwenda na ww lkn kwa upande wa wapopo unaweza kupata 15% kwa vile hawapo tayari kufa kwa ajili ya pesa, ila wapo tayari kufungwa hata miaka 10 jela kwa ajili ya kuuza ngada maana anajua akikamatwa anaweza kuonga kesi ikaisha. Kuna mpopo aliwahi kunambia kuwa ni rahisi mpopo kupiga hela ndefu katika nchi zenye vita kama centre africa, congo nk kuliko kupiga hela katika nchi ya Tanzania. Wanajua.
Nasema tena kkoo wapopo wapo kibao wanapiga pesa..wao mizigo yao wanauzia store wachache wana maduka...
 
South Africa ya siku hizi ina watu wema hivyo? Yani umkute mtu analia uende kumuuliza analia nini unamsemesha kizulu then unagunduwa ni Mtanzania unampeleka kwako.

Konda tafadhali nishushe hapahapa nimefika, mwendo wa dereva ni hatarishi.
Amapantsula indaaabaaa kabani
 
Hii ni sifa mbaya sana kuanza kuhofiwa kwa wizi na utapeli nje ya nchi sasa tutapataje michongo wazee kama hatuaminiki kiasi hiki, ndio maana nasikiaga fununu wa bongo 99% walioko SA kazi yao kubwa ni kuuza sembe sijui hili limekaeje wazee
 
Habar zenu ndugu zangu. Ama baada ya salam ningependa kuendelea na kile kilichonifanya niandike uzi huu. Ndugu zangu kama ilivyo ada au kama tulivyofunzwa na misingi yetu ya Taifa kwamba watanzania popote tulipo haijalishi ni ndani au nje ya nchi, sisi ni watu wamoja. Kwahiyo kwa misingi hiyo sisi tulio nje huwa na desturi au utamaduni wa kusaidiana bila kujali tofauti zetu za kikabila, dini, rangi, jinsia au kanda ya mtu anayotokea ilimradi sote ni watanzania na tunatokea kwenye ardhi ya Tanzania basi ni ndugu.

Sasa basi miezi 3 iliyopita kuna kijana aliingia Kaburu akitokea bongo kwa lengo la kuja kutafuta maisha. Kijana anadai kuna rafiki yake wa kitaa, kwa sasa anaeishi Capetown ndio alimshawishi kuja maisha haya, lkn alipoingia tu "Kaburu" yule rafiki yake akamzimia simu na kumkosa kabisa online.

Kijana akachanganyikiwa asijue wapi pakwenda wala nini cha kufanya. Nikiwa katika mizunguko yangu mitaa ya park station Johannesburg, ghafla nikapita sehem na kumuona kijana akiwa kajiinamia na begi lake huku machozi yakimtoka. Nikamsogelea taratibu na kujaribu kumuuliza kwa lugha ya wenyeji, ghafla nikasikia jamaa akiongea kiswahili, hii ikanipa nguvu ya kumsogelea na kumuuliza zaidi baada ya kugundua kuwa naongea na mtu anaetoka nchini kwetu. Baada ya maongezi ya hapa na pale nikagundua kuwa jamaa ameingizwa cha kike na mwenyeji wake, kwahiyo nikachukua jukumu la kumsaidia.

Nikaondoka na jamaa hadi nyumban, akaoga, akala, baada ya kula nikampa sehem ya kupumzika akalala. Kwa kuwa mimi nina familia ikanibidi niende kuongea na homeboy fulan ambae ni single ili ampe hifadhi ya miezi kadhaa wakati nikiendelea na mchakato wa kumtafutia shughuli ya kufanya, mshikaji akakubali lkn kwa masharti ya kumsaidia kulipa rent.

Kwa kuwa nilikuwa nimeamua kumsaidia kijana, basi nikaona poa tu acha nimsadie kulipa rent ili aweze kuishi nae. Kijana tumekaa nae mwezi wa kwanza, wa pili na sometimes nilikuwa naenda nae kwenye mishe zangu ili kumzoesha mazingira ya nchi, na mishe za hapa na pale. Mwezi mmoja uliopita kuna rafiki angu Mkenya ambae tuliwahi kufanya nae kazi huko Gezina, Pretoria.

Mkenya alikuwa anatafuta mtu wa kumuachia saluni yake kubwa na ya kisasa iliyopo nje kidogo ya jiji la Pretoria huko Nellmapius, kwa malipo ya R600 kwa week (sawa na sh elfu 85 au elf 90) kula na kulala bure. Kwa vile nilikuwa na kijana na tayari alishanambia kuwa bongo kazi yake kubwa ilikuwa ni ukinyozi, nikaona YES maji ya mvua yameangukia juu ya mgongo wa bata. Nikampanga kijana, kesho yake mapema nikampeleka mpaka Pretoria kwa yule Mkenya na kumkabidhi.

Kweli bwana baada ya siku mbili kijana akaanza kazi huku Mkenya akiniomba nimtafutie vijana wengine ambao wataenda kusaidizana nae, maana saluni ni kubwa ilihitaji vinyozi zaidi ya watano, lkn pia kijana lugha ni tatizo, so alitaka ambao wangeweza pia kusaidiana hata katika mambo ya lugha za wenyeji ili kuwateka vizuri wateja wa kizawa.

Nikamuahidi jamaa kumtafutia hao vijana. Wakati namuacha kwa yule Mkenya kijana wang nilimuachia sim kwa ajili ya mawasiliano yetu, au ndugu zake wa bongo, au boss wake (Mkenya). Dogo tukawa tunawasiliana ananipa taarifa za kazi na mimi nampa mpa moyo kuwa akomae ili atimize malengo ya kile kilichomleta hapa nk. Siku tatu zilizopita sikumpata online, nikajua labda simu imepata tatizo ghafla.

Sasa jana yule rafiki angu Mkenya amenipigia simu na kuniambia kuwa jamaa amemuibia kila kitu cha saluni, na hela ambazo yule Mkenya anaendaga kuzichukua kwa week jamaa katimka nazo. Simu yake haipiti na hatujui tutamtoa wapi. Nilipotaka kumlipa yule Mkenya nusu ya hasara ya vitu alivyoiba jamaa, Mkenya amkataa amesema nisijali kwa vile sio kosa langu ni kosa la mtu mungine kwahiyo mimi sistahili kumlipa na ukizingatia na rafiki yangu.

Hiki kitendo cha huyu jamaa kimenisononesha na kunivunja nguvu. Imenifanya sasa niwachukie wabongo wenzangu, maana hii ni mara pili sasa nawasaidia wabongo afu wanaharibu na kutimkia kusikojulikana, japo kwa huyu sikutegemea hata kidogo kutokana na upole na muonekano wake.

Najua binadamu tunatakiwa tusamehe, lkn kwa mikasa hii sioni sababu ya kusamehe kwa lengo la kurudi kumsaidia mungine labda yule nimjuae A to Z. Ndugu zangu wabongo tubadilike, hii dunia tunapita tu. Kumuharibia mtu anaekusaidia sio ujanja bali ni ujinga wa mwisho. Hii ni tahadhari nimetoa kwa vijana wengine kuwa makini sana. Asanteni
Pole sana

Ila msamehe afu sahau
 
Nyimyi watanganyika kazi zenu ni wizi na ujambazi ndio maana uaminifu kwenu ni zero tofauti na wazanzibar wanavoaminiwa ndani ya nchi yao mpaka njee ya nchi yao
Halafu nyinyi mnajikutaga watakatifu sana, mtafikiri nyinyi sio wezi,wazinzi.... kemea tabia ya mtu na sio asili ya mtu acheni ubaguzi
 
Na sijasema nchi za Sadc. Ni nchi zenye mifumo imara ya teknolojia.
Hong Kong hawagongi pia na Iran walikua hawagongi watu wakienda kutalii pale walikua wanasumbuliwa Nchi zingine maana waliwekewa vikwazo kugonga kwa Nchi zetu ni nzuri mitandao ikigoma waona...
 
Habar zenu ndugu zangu. Ama baada ya salam ningependa kuendelea na kile kilichonifanya niandike uzi huu. Ndugu zangu kama ilivyo ada au kama tulivyofunzwa na misingi yetu ya Taifa kwamba watanzania popote tulipo haijalishi ni ndani au nje ya nchi, sisi ni watu wamoja. Kwahiyo kwa misingi hiyo sisi tulio nje huwa na desturi au utamaduni wa kusaidiana bila kujali tofauti zetu za kikabila, dini, rangi, jinsia au kanda ya mtu anayotokea ilimradi sote ni watanzania na tunatokea kwenye ardhi ya Tanzania basi ni ndugu.

Sasa basi miezi 3 iliyopita kuna kijana aliingia Kaburu akitokea bongo kwa lengo la kuja kutafuta maisha. Kijana anadai kuna rafiki yake wa kitaa, kwa sasa anaeishi Capetown ndio alimshawishi kuja maisha haya, lkn alipoingia tu "Kaburu" yule rafiki yake akamzimia simu na kumkosa kabisa online.

Kijana akachanganyikiwa asijue wapi pakwenda wala nini cha kufanya. Nikiwa katika mizunguko yangu mitaa ya park station Johannesburg, ghafla nikapita sehem na kumuona kijana akiwa kajiinamia na begi lake huku machozi yakimtoka. Nikamsogelea taratibu na kujaribu kumuuliza kwa lugha ya wenyeji, ghafla nikasikia jamaa akiongea kiswahili, hii ikanipa nguvu ya kumsogelea na kumuuliza zaidi baada ya kugundua kuwa naongea na mtu anaetoka nchini kwetu. Baada ya maongezi ya hapa na pale nikagundua kuwa jamaa ameingizwa cha kike na mwenyeji wake, kwahiyo nikachukua jukumu la kumsaidia.

Nikaondoka na jamaa hadi nyumban, akaoga, akala, baada ya kula nikampa sehem ya kupumzika akalala. Kwa kuwa mimi nina familia ikanibidi niende kuongea na homeboy fulan ambae ni single ili ampe hifadhi ya miezi kadhaa wakati nikiendelea na mchakato wa kumtafutia shughuli ya kufanya, mshikaji akakubali lkn kwa masharti ya kumsaidia kulipa rent.

Kwa kuwa nilikuwa nimeamua kumsaidia kijana, basi nikaona poa tu acha nimsadie kulipa rent ili aweze kuishi nae. Kijana tumekaa nae mwezi wa kwanza, wa pili na sometimes nilikuwa naenda nae kwenye mishe zangu ili kumzoesha mazingira ya nchi, na mishe za hapa na pale. Mwezi mmoja uliopita kuna rafiki angu Mkenya ambae tuliwahi kufanya nae kazi huko Gezina, Pretoria.

Mkenya alikuwa anatafuta mtu wa kumuachia saluni yake kubwa na ya kisasa iliyopo nje kidogo ya jiji la Pretoria huko Nellmapius, kwa malipo ya R600 kwa week (sawa na sh elfu 85 au elf 90) kula na kulala bure. Kwa vile nilikuwa na kijana na tayari alishanambia kuwa bongo kazi yake kubwa ilikuwa ni ukinyozi, nikaona YES maji ya mvua yameangukia juu ya mgongo wa bata. Nikampanga kijana, kesho yake mapema nikampeleka mpaka Pretoria kwa yule Mkenya na kumkabidhi.

Kweli bwana baada ya siku mbili kijana akaanza kazi huku Mkenya akiniomba nimtafutie vijana wengine ambao wataenda kusaidizana nae, maana saluni ni kubwa ilihitaji vinyozi zaidi ya watano, lkn pia kijana lugha ni tatizo, so alitaka ambao wangeweza pia kusaidiana hata katika mambo ya lugha za wenyeji ili kuwateka vizuri wateja wa kizawa.

Nikamuahidi jamaa kumtafutia hao vijana. Wakati namuacha kwa yule Mkenya kijana wang nilimuachia sim kwa ajili ya mawasiliano yetu, au ndugu zake wa bongo, au boss wake (Mkenya). Dogo tukawa tunawasiliana ananipa taarifa za kazi na mimi nampa mpa moyo kuwa akomae ili atimize malengo ya kile kilichomleta hapa nk. Siku tatu zilizopita sikumpata online, nikajua labda simu imepata tatizo ghafla.

Sasa jana yule rafiki angu Mkenya amenipigia simu na kuniambia kuwa jamaa amemuibia kila kitu cha saluni, na hela ambazo yule Mkenya anaendaga kuzichukua kwa week jamaa katimka nazo. Simu yake haipiti na hatujui tutamtoa wapi. Nilipotaka kumlipa yule Mkenya nusu ya hasara ya vitu alivyoiba jamaa, Mkenya amkataa amesema nisijali kwa vile sio kosa langu ni kosa la mtu mungine kwahiyo mimi sistahili kumlipa na ukizingatia na rafiki yangu.

Hiki kitendo cha huyu jamaa kimenisononesha na kunivunja nguvu. Imenifanya sasa niwachukie wabongo wenzangu, maana hii ni mara pili sasa nawasaidia wabongo afu wanaharibu na kutimkia kusikojulikana, japo kwa huyu sikutegemea hata kidogo kutokana na upole na muonekano wake.

Najua binadamu tunatakiwa tusamehe, lkn kwa mikasa hii sioni sababu ya kusamehe kwa lengo la kurudi kumsaidia mungine labda yule nimjuae A to Z. Ndugu zangu wabongo tubadilike, hii dunia tunapita tu. Kumuharibia mtu anaekusaidia sio ujanja bali ni ujinga wa mwisho. Hii ni tahadhari nimetoa kwa vijana wengine kuwa makini sana. Asanteni
Huyo dogo bora ungemlengesha kwa manjagu arudishwe TZ tumfunge miezi 6 kwa kosa la kutoroka Nchini
 
Napenda kuwa huru na maisha yangu, bila kupangiwa masharti ya maisha.
Misaada mingi ya watu huwa imejaa masharti na manyanyaso lukuki.

Nimekataa dili kibao tu na nafasi kubwa ambazo ni Life Changing...
And truth be told, I have never regretted my decisions......
Ahsante Mungu kwa kukutana na comment ya mtu ambaye tuna-share ideology na personalities, hata mimi nipo hivyo mkuu! Ni jambo la furaha mno kuona comment yako.
 
Back
Top Bottom