NAANZA KUAMINI UHUSIKA WA SERIKALI TUKIO LA KUTEKWA ROMA NA WENZIE

roma ameniangusha sana........na serikali nayo kila mission haipatiwi ufumbuzi. sijui kwa nn.......!!!!
 
Huyu si alikua anaimba yuko tayari kufa!!!
Kumbe alizani kifo ni kusinzia eeh!!!
Nasikia wanamgogoro na mkewe karibu wataachana kisa hawezi tena mapenzi na mkewe
wee muongo Roma kabarikiwa na mke wewe. Mdada yani anampenda sana roma hata kwenye instagram. Yule ni mke mwema kwa roma kutoka kwa bwana
 
Ni takribani miezi miwili sasa inakatika huku kukiwa na ukimya wa kushangaza kutoka vyombo vya usalama kuhusu kilichowatokea ROMA na wenzie,mimi kama raia wa nchi hii imeumizwa na kusikitishwa sana na ukimya huu kuliko hata tukio lenyewe la utekaji,haiwezekani raia wanatekwa wanaenda kuteswa vibaya halafu tukio hilo lipite kama hakujatokea kitu inasikitisha sana.

Nimesikitishwa pia na kimya cha waziri wa habari kwa jinsi picha yake inavyonijia siku akiwa kwenye press conference ya ROMA akionekana kana kwamba ana uchungu na ameguswa sana na tukio hilo kumbe alikuwa anatuachezea bongo muvi,inasikitisha sana
Hata mkuu wa mkoa aliyehakikisha vyombo vya dola vinafannya juu chini kuhakikisha ndugu zetu watanzania wenzetu wanapatikana wakiwa wazima nae pia hana hata habari kama vile hili jambo halikumgusa,KWELI!?

vyombo vya usalama viko kimya,mwezi wa pili huu unakaribia lakini hakuna findings wala update yoyote mpaka sasa,hii inaleta picha mbaya kwamba raia sasa hatuko salama ndani ya nchi yetu kama ni kweli watu wanaweza wakafanya mambo ya kutisha kiasi hicho halafu wakapotelea GIZANI.huu ni muendelezo wa matukio ambayo serikali haiyapatii ufumbuzi kama matukio yanayotokea huko KIBITI,tukio la kupotea BEN SANANE,matukio haya yanaichafua serikali kwamba imeshindwa kuchukua hatua au serikali inapuuzia UHAI wa RAIA wake na pia inapuuzia haki ya sisi wananchi kujulishwa kuhusu usalama wetu.kwa hali hii halafu anatokea mtu anakuhubiria kuhusu UZALENDO,kweli!?
ROMA yupo hai kwa nini usimuulize kimemtokea nini?
Ndio maana shule mnafeli kwa wingi kutokana na ugoi goi wa akili,muathirika yupo hai,aulizwe yeye alipatwa na nini badala ya kuisakama serikali
 
ROMA yupo hai kwa nini usimuulize kimemtokea nini?
Ndio maana shule mnafeli kwa wingi kutokana na ugoi goi wa akili,muathirika yupo hai,aulizwe yeye alipatwa na nini badala ya kuisakama serikali
dah!hongera sana wewe uliefaulu shule.
 
ROMA yupo hai kwa nini usimuulize kimemtokea nini?
Ndio maana shule mnafeli kwa wingi kutokana na ugoi goi wa akili,muathirika yupo hai,aulizwe yeye alipatwa na nini badala ya kuisakama serikali
kwa hio ww unaeitetea serikali umefaulu shule? chet unacho? maana mwenzako bashite anaulizwa chet chake analia lia tu. wewe kwan ni msemaji wa serekal? goi goi plus
 
kwa hio ww unaeitetea serikali umefaulu shule? chet unacho? maana mwenzako bashite anaulizwa chet chake analia lia tu. wewe kwan ni msemaji wa serekal? goi goi plus
Nikuoneshe cheti kwani wewe muajiri wangu?
 
Back
Top Bottom