Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Vladmir Putini

JF-Expert Member
Mar 22, 2022
777
1,439
Wakuu poleni kwa upambanaji.

Binafsi mimi kuna mda huwa nikitulizaga kichwa changu huwa naanza kujiuliza maswali mengi sana kuhusu mimi (binadamu) na ulimwengu kiujumla (Universe).

Maswali kama sisi (binadamu) ni kina nani,tumetoka wapi asili yetu, kwanini tupo (dhumuni la kuishi), mwisho wetu ama hatima yetu ni nini, Ulimwengu wa vitu je kama sayari, nyota, galaxies zimekuwepo vipi na nini hasa mwisho wake.

Hapo juu ni baadhi tu ya maswali ambayo huwa naiuliza sana akili yangu ikiwaga katika hali ya utulivu.

Lakini cha kusikitisha ni kwamba, katika maswali yote hayo ambayo huwa najiuliza, sijawahi kupata jibu la uhakika kuniridhisha kuhusu hayo maswali yangu.

Nimekuwa nikifanya bidii kubwa sana kupata majibu ya maswali yangu kupitia usomaji wa majarida au vitabu vihusuvyo historia,sayansi, dini na Falsafa lakini kote bado sijapata majibu ya kuniridhisha tofauti na kuambulia majibu ya kinadharia tu ambayo yana strength kiasi chake lakini pia yana weakness sehemu nyingi tu.

Na nikiri wazi tu kuwa katika usomaji wangu wa nadharia hizo zote (historia, sayansi, dini, falsafa) sehemu ambayo nimeanza kuiamini kunipa majibu ya maswali yangu ni kwenye DINI.

Nikiwa na maana nimeanza kuamini kwamba uwepo na sisi tuliohai na visivyo hai hapa ulimwenguni ni matokea ya Uumbaji ya nguvu kubwa sana inayoitwa MUNGU/ALLAH kama ambavyo dini nyingi zinaelezea nguvu hiyo.

Na leo maswali yangu yanajikita huko kwenye hiyo nguvu (Mungu) maana nimeanza kuiamini lakini pia kila nisomapo BIBLIA (mimi mkristo) inanipa maswali chungu nzima.

Sasa leo swali langu limejikita kwenye UKAMILIFU wa MUNGU.

Naombeni wasomaji mnielewe kuwa sina maana ya kukufuru (maana mara nyingi niulizapo maswali kuhusu MUNGU huwa naambiwa nakufuru) bali mimi nataka kujifunza zaidi kumuhusu huyu Mungu.

Dini nyingi (hasa Ukristo na uislamu) zimekuwa zikimwelezea Mungu kuwa ni Mkamilifu sana,mwenye nguvu nyingi sana, uwezo na akili zake hazichunguziki, hashindwi na chochote n.k.

Je hilo lina ukweli ? kupitia Biblia mimi nimeanza kudhani kwamba huenda kweli Mungu ana nguvu nyingi sana ila siyo zote, ana uwezo mkubwa sana ila siyo uwezo wote,ana maarifa mengi sana ila siyo maarifa yote, ana ukamilifu mwingi sana ila siyo ukamilifu wote n.k

Nasema haya ni kutokana na maswali yafuatayo :

1. Kama Mungu ana ukamilifu wote, kwanini sasa alimuumba malaika (Lucifer/shetani) alafu badae akaja kumuasi?
Kama Shetani/Lucifer aliasi maana yake ni kwamba Mungu alimuumba huyu kiumbe akiwa na madhaifu kadhaa na ndiyo maana alishindwa kuitii amri/mamlaka ya muumbaji wake.

Kama Mungu angelikuwa na ukamilifu wote, basi malaika wote wangelikuwa wameumbwa katika namna ya utii pekee, uasi usingetokea na huo uasi unadhihirisha kwamba Mungu aliwaumba hawa malaika wakiwa na udhaifu flani, hawakuwa na uimara wote.

2. Uumbaji wa Eva (Hawa) unaonesha kulikuwa na madhaifu pia.
Katika Biblia takatifu kwenye kitabu cha mwanzo, kuna mistari inaeleza kuwa "Mungu alimpa usingizi mzito Adam, alafu akabandua sehemu ya ubavu wake na kumfanya/kumuumba mwanamke (Hawa/Eva)".

Alafu Mungu akamwambia Adam kuwa huyu mwanamke atakuwa msaidizi wako

Lakini ni huyo huyo mwanamke ambae shetani (kwenye umbo la nyoka) alienda kumdanganya akachukua matunda ya mti walioambiwa asile yeye akala na akampelekea na mumewe (Adam) pia akala.

Lakini Mungu alivyomuuliza Adam kwanini umekula matunda ya mti ambao nilikwambia usile, Adam alijibu kuwa "Ni huyo mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea nikala".

Tukio hili linadhihirisha kuwa Mungu alimpa Adam msaidizi (Hawa) ambae ni dhaifu sana na ndiyo maana alisababisha dhambi ikaenda hadi kwa Adam.

Na huenda kama Mungu angelikuwa amempa Adam msaidizi imara asiye na madhaifu basi ile dhambi ya kula tunda ingeepukika.

Uko wapi sasa ukamilifu wote wa Mungu ikiwa aliweza kuwaumba malaika dhaifu (ambao walikuja kumuasi) na pia bado akampa Adam msaidizi dhaifu kabisa ambaye alisababisha dhambi imwendee hadi Adam?

Kwa leo naombeni comment zenu zinifunze kuhusu hilo tu (La ukamilifu wa Mungu) alafu mengine nitauliza siku nyingine, na mengine nitakuwa nauliza humo humo kwenye comments zenu.

NB: Naamini Mungu yupo, kutokana na baadhi ya vitu ninavyoviona ulimwenguni (hasa uumbaji/creation) ambapo kuna baadhi ya vitu hasa sayansi inakosa majibu ya kuridhisha, ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.

Karibuni mnifunze.
 
Wakuu poleni kwa upambanaji.

Binafsi mimi kuna mda huwa nikitulizaga kichwa changu huwa naanza kujiuliza maswali mengi sana kuhusu mimi (binadamu) na ulimwengu kiujumla (Universe).

Maswali kama sisi (binadamu) ni kina nani,tumetoka wapi asili yetu, kwanini tupo (dhumuni la kuishi), mwisho wetu ama hatima yetu ni nini, Ulimwengu wa vitu je kama sayari, nyota, galaxies zimekuwepo vipi na nini hasa mwisho wake.

Hapo juu ni baadhi tu ya maswali ambayo huwa naiuliza sana akili yangu ikiwaga katika hali ya utulivu.

Lakini cha kusikitisha ni kwamba, katika maswali yote hayo ambayo huwa najiuliza, sijawahi kupata jibu la uhakika kuniridhisha kuhusu hayo maswali yangu.

Nimekuwa nikifanya bidii kubwa sana kupata majibu ya maswali yangu kupitia usomaji wa majarida au vitabu vihusuvyo historia,sayansi, dini na Falsafa lakini kote bado sijapata majibu ya kuniridhisha tofauti na kuambulia majibu ya kinadharia tu ambayo yana strength kiasi chake lakini pia yana weakness sehemu nyingi tu.

Na nikiri wazi tu kuwa katika usomaji wangu wa nadharia hizo zote (historia, sayansi, dini, falsafa) sehemu ambayo nimeanza kuiamini kunipa majibu ya maswali yangu ni kwenye DINI.

Nikiwa na maana nimeanza kuamini kwamba uwepo na sisi tuliohai na visivyo hai hapa ulimwenguni ni matokea ya Uumbaji ya nguvu kubwa sana inayoitwa MUNGU/ALLAH kama ambavyo dini nyingi zinaelezea nguvu hiyo.

Na leo maswali yangu yanajikita huko kwenye hiyo nguvu (Mungu) maana nimeanza kuiamini lakini pia kila nisomapo BIBLIA (mimi mkristo) inanipa maswali chungu nzima.

Sasa leo swali langu limejikita kwenye UKAMILIFU wa MUNGU.

Naombeni wasomaji mnielewe kuwa sina maana ya kukufuru (maana mara nyingi niulizapo maswali kuhusu MUNGU huwa naambiwa nakufuru) bali mimi nataka kujifunza zaidi kumuhusu huyu Mungu.

Dini nyingi (hasa Ukristo na uislamu) zimekuwa zikimwelezea Mungu kuwa ni Mkamilifu sana,mwenye nguvu nyingi sana, uwezo na akili zake hazichunguziki, hashindwi na chochote n.k.

Je hilo lina ukweli ? kupitia Biblia mimi nimeanza kudhani kwamba huenda kweli Mungu ana nguvu nyingi sana ila siyo zote, ana uwezo mkubwa sana ila siyo uwezo wote,ana maarifa mengi sana ila siyo maarifa yote, ana ukamilifu mwingi sana ila siyo ukamilifu wote n.k

Nasema haya ni kutokana na maswali yafuatayo :

1. Kama Mungu ana ukamilifu wote, kwanini sasa alimuumba malaika (Lucifer/shetani) alafu badae akaja kumuasi?
Kama Shetani/Lucifer aliasi maana yake ni kwamba Mungu alimuumba huyu kiumbe akiwa na madhaifu kadhaa na ndiyo maana alishindwa kuitii amri/mamlaka ya muumbaji wake.

Kama Mungu angelikuwa na ukamilifu wote, basi malaika wote wangelikuwa wameumbwa katika namna ya utii pekee, uasi usingetokea na huo uasi unadhihirisha kwamba Mungu aliwaumba hawa malaika wakiwa na udhaifu flani, hawakuwa na uimara wote.

2. Uumbaji wa Eva (Hawa) unaonesha kulikuwa na madhaifu pia.
Katika Biblia takatifu kwenye kitabu cha mwanzo, kuna mistari inaeleza kuwa "Mungu alimpa usingizi mzito Adam, alafu akabandua sehemu ya ubavu wake na kumfanya/kumuumba mwanamke (Hawa/Eva)".

Alafu Mungu akamwambia Adam kuwa huyu mwanamke atakuwa msaidizi wako

Lakini ni huyo huyo mwanamke ambae shetani (kwenye umbo la nyoka) alienda kumdanganya akachukua matunda ya mti walioambiwa asile yeye akala na akampelekea na mumewe (Adam) pia akala.

Lakini Mungu alivyomuuliza Adam kwanini umekula matunda ya mti ambao nilikwambia usile, Adam alijibu kuwa "Ni huyo mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea nikala".

Tukio hili linadhihirisha kuwa Mungu alimpa Adam msaidizi (Hawa) ambae ni dhaifu sana na ndiyo maana alisababisha dhambi ikaenda hadi kwa Adam.

Na huenda kama Mungu angelikuwa amempa Adam msaidizi imara asiye na madhaifu basi ile dhambi ya kula tunda ingeepukika.

Uko wapi sasa ukamilifu wote wa Mungu ikiwa aliweza kuwaumba malaika dhaifu (ambao walikuja kumuasi) na pia bado akampa Adam msaidizi dhaifu kabisa ambaye alisababisha dhambi imwendee hadi Adam?

Kwa leo naombeni comment zenu zinifunze kuhusu hilo tu (La ukamilifu wa Mungu) alafu mengine nitauliza siku nyingine, na mengine nitakuwa nauliza humo humo kwenye comments zenu.

NB: Naamini Mungu yupo, kutokana na baadhi ya vitu ninavyoviona ulimwenguni (hasa uumbaji/creation) ambapo kuna baadhi ya vitu hasa sayansi inakosa majibu ya kuridhisha, ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.

Karibuni mnifunze.
Ukiangalia kwa ukaribu upande wa dini ulikua na ni mpango wa mwanadamu kuutafuta ukweli ama nguvu ambayo ni kubwa kuliko sisi.
Sasa katika hizo harakati za kutafuta kila mmoja kaja na nadharia tofauti kulingana na exPerience yake.

Ukiangalia kwa ukaribu zaidi ni kwamba dini unaweza kua ulikua ni mpango mzuri zaidi labda wa kujiunganisha na huyo alie mkubwa kuliko sisi, lakini kilichotokea na kinachotokea ule ambao ukweli ulioanza kuonekana au umewahi kupatwa umebadilishwa kila mmoja akiserve interest anazozijua yeye.

So kuelewa vizuri ni bora kuanza kujitizama kuanzia ndani (look within) I'm uta-experience kwa namna tofauti na kuachana na hizi stori stori zingine.
 
Tunaamini hivyo kwasababu kuna vitu hatujavijua bado!! Sifa za Mungu alizopewa Ktk vitabu haziendani na uhalisia!..
Mkuu fikra zetu zinaathiriwa na mazingira yetu.. sitakupa jibu la Mungu yupo au hayupo ila jibu nalokupa ni kuwa ulimwengu unasheria za kushangaza sana tukijazigundua ndo zaidi tutaelewa kuhusu Mungu!.. hatujui vingi kuhusu ulimwengu ndio maana tunapwayapwaya hata ktk kumuelezea Mungu kwani hatumjui bado.
 
Ukiangalia kwa ukaribu upande wa dini ulikua na ni mpango wa mwanadamu kuutafuta ukweli ama nguvu ambayo ni kubwa kuliko sisi.
Sasa katika hizo harakati za kutafuta kila mmoja kaja na nadharia tofauti kulingana na exPerience yake.

Ukiangalia kwa ukaribu zaidi ni kwamba dini unaweza kua ulikua ni mpango mzuri zaidi labda wa kujiunganisha na huyo alie mkubwa kuliko sisi, lakini kilichotokea na kinachotokea ule ambao ukweli ulioanza kuonekana au umewahi kupatwa umebadilishwa kila mmoja akiserve interest anazozijua yeye.

So kuelewa vizuri ni bora kuanza kujitizama kuanzia ndani (look within) I'm uta-experience kwa namna tofauti na kuachana na hizi stori stori zingine.

By the way dini inaweza isiwe suala la kubwa kwangu.

Lakini ni kwamba, nikisoma nadharia zingine hasa sayansi ya AUSTRONOMY inanifanya mimi kwa mawazo yangu mwenyewe ni conclude tu kusema Mungu yupo.

Mfano : katika sayansi ya anga za juu (Austronomy) ni kwamba kila kitu kilichoko angani kinazunguka (every object in the universe is moving or is in motion).

Ni kama na maana kwamba Dunia inazunguka,Mwezi unazunguka,Sayari zote zinazunguka,Jua linazunguka,Galaxy (mkusanyiko wa nyota) zinazunguka,Black holes zina zunguka n.k

Yaani kifupi ni kwamba hakuna kitu hata kimoja ambacho kimo hewani kimesimama wima tu hakizunguki,every object is in motion.

Lakini sasa kinachonishangaza, kwenye hii tasnia ni kwamba "ulimwengu unazunguka kwa kufata kanuni maalum".

Yaani unavyoviona angani vyote vinazunguka kwa kufata system/formula ama mfumo maalum na ndiyo maana huoni vikigongana hovyo wakati ukiangalia ni kama viko shaghala paghala (bila mpangailio).

Isingekuwa hivi vitu viko kwenye mfumo maalum basi dunia yetu hii ingeshagogwa na vitu vingine vikubwa sana angani na ingeshasambaratika muda tu.

Coz kwenye anga kuna vitu vikubwa sana ambavyo ukifananisha na Dunia, Dunia itaonekana kama kipande cha kokoto tu.

Hivyo basi, universe kuwa katika mpangalio maalum na kufata kanuni , ndiyo kunanifanya nipate wazo kuwa "Lazima kutakuwa na fundi aliyedizaini hivi vitu na kuviongoza (kama remote controller).

Trust me huu ulimwengu usingekuwa na fundi maalum wa kuungoza basi vitu angani vingekuwa vinagongana kila dakika hata dunia sasahivi isingekuwepo ingeshafanywa kifusi mda.

Sasa huyo fundi ndiye nimekuja kudhani kwamba ndiyo atakuwa huyo Mungu anaesemwa kwenye vitabu vya dini.

Lakini sasa nimeenda na kwenye vitabu vya dini, sifa anazopewa nikilinganisha na matukio ya baadhi ya vitu humo humo kwenye vitabu vya dini, naona kabisa vinakosa ushirikiano/haviendani.

Nimeamua nikupe mfano mmoja tu wa AUSTRONOMY, ila ukitaka mwingine pia nitakupa
 
Hapo naona unamfikiria Mungu kama binadamu.

Ila kwa Mungu dunia iko sawa kabisa na anavyotaka yeye, ila wewe ndo unafikiri hayo yote yaliyo tokea yako nje ya uwezo wake.

Ngoja nikuulize

1.Kwa nini tunaweka watu 22 uwanjani washindane kuingiza mpira golini kwa kutumia miguu.

Mbona asiingia tu mtu mmoja akabeba mpira na mkono akaugiza golini?


2.Umewahi kucheza gemu rahisi? Lilikua linaboa eeeh?



Mpaka happy Kuna kitu umegundua au bado.
 
Tunaamini hivyo kwasababu kuna vitu hatujavijua bado!! Sifa za Mungu alizopewa Ktk vitabu haziendani na uhalisia!..
Mkuu fikra zetu zinaathiriwa na mazingira yetu.. sitakupa jibu la Mungu yupo au hayupo ila jibu nalokupa ni kuwa ulimwengu unasheria za kushangaza sana tukijazigundua ndo zaidi tutaelewa kuhusu Mungu!.. hatujui vingi kuhusu ulimwengu ndio maana tunapwayapwaya hata ktk kumuelezea Mungu kwani hatumjui bado.

Nakubaliana na wewe kabisa.

Na mimi nikwambie tu kuwa mimi binafsi naamini kuna nguvu ipo inayouongoza huu ulimwengu, labda tuseme hiyo nguvu ndiyo tuipe jina la Mungu.

Na tukishaipa jina la Mungu, maana ya ukitaka kuijua zaidi hiyo nguvu ni lazima uende kwenye vitabu vya Dini ndiko utakakopata maelezo kumuhusu.


Lakini sasa nimeenda huko, nimesoma maandiko ya huko, sifa anazopewa huyo Mungu, zinaniachia maswali chungu nzima na kuanza kuhoji kuhusu uwezo/maarifa/ukamilifu wake
 
Hapo naona unamfikiria Mungu kama binadamu.

Ila kwa Mungu dunia iko sawa kabisa na anavyotaka yeye, ila wewe ndo unafikiri hayo yote yaliyo tokea yako nje ya uwezo wake.

Ngoja nikuulize

1.Kwa nini tunaweka watu 22 uwanjani washindane kuingiza mpira golini kwa kutumia miguu.

Mbona asiingia tu mtu mmoja akabeba mpira na mkono akaugiza golini?


2.Umewahi kucheza gemu rahisi? Lilikua linaboa eeeh?



Mpaka happy Kuna kitu umegundua au bado.
Kwanza nikuweke sawa kuwa, mimi simfikirii Mungu kuwa sawa na binadamu.

Nimesema kuwa Mungu ana uwezo mwingi,akili nyingi,maarifa.mengi,ukamilifu mwingi ila kati vyote hivyo anavyo katika hali ya wingi na siyo katika hali ya ukamilifu wote (100%) ama ya kutokuwa na kikomo

Nasema hayo sija- Qoute kokote ila nimesema ni kutokana na jinsi anavyojipambanua yeye ndani ya vitabu vyake vitakatifu (rejea mifano miwili ya maswali niliyatolea mfano kwenye uzi).

Mungu angelikuwa na sifa zote hizo za ukamilifu basi hizo kasoro zilizojitokeza (zikapelekea dhambi) zingeweza kuepukika iwapo uumbaji huo angeufanya katika ukamilifu.

Zingatia kwamba, sijaribu kumkosoa/kumsahihisha Mungu katika uumbaji wake bali nataka tu kujua kwanini itokee hivo wakati yeye ana ukamilifu wote na uwezo wake hauna kikomo ?

Labda mnambie kama hizo kasoro aliziumba kwa maksudi kwa sababu anazozijua mwenyewe hapo nitawaelewa ila mkiendelea kunambia aliumba katika ukamilifu wote, hapo nitaendelea kuwauliza maswali yasiyoisha.

Mfano wako wa mpira kuwa na wachezaji 22 na kushindana kuingiza goli kwa miguuu.

Huu mfano kumbuka ni wa kanuni (sheria za kibinadamu ambazo tumeziweka wenyewe) na mara kwa mara hufanyiwa marekebisho kulingana za uhitaji.

Mfano sasahivi wanafikiria kupunguza dakika za kucheza ziwe 40 kwa kila kipindi badala ya 45.

Kwa hiyo hizi ni kanuni ambazo tumweziweka na tunazibadilisha muda wowote tutakaotaka
 
Kwanza nikuweke sawa kuwa, mimi simfikirii Mungu kuwa sawa na binadamu.

Nimesema kuwa Mungu ana uwezo mwingi,akili nyingi,maarifa.mengi,ukamilifu mwingi ila kati vyote hivyo anavyo katika hali ya wingi na siyo katika hali ya ukamilifu wote (100%) ama ya kutokuwa na kikomo

Nasema hayo sija- Qoute kokote ila nimesema ni kutokana na jinsi anavyojipambanua yeye ndani ya vitabu vyake vitakatifu (rejea mifano miwili ya maswali niliyatolea mfano kwenye uzi).

Mungu angelikuwa na sifa zote hizo za ukamilifu basi hizo kasoro zilizojitokeza (zikapelekea dhambi) zingeweza kuepukika iwapo uumbaji huo angeufanya katika ukamilifu.

Zingatia kwamba, sijaribu kumkosoa/kumsahihisha Mungu katika uumbaji wake bali nataka tu kujua kwanini itokee hivo wakati yeye ana ukamilifu wote na uwezo wake hauna kikomo ?

Labda mnambie kama hizo kasoro aliziumba kwa maksudi kwa sababu anazozijua mwenyewe hapo nitawaelewa ila mkiendelea kunambia aliumba katika ukamilifu wote, hapo nitaendelea kuwauliza maswali yasiyoisha.

Mfano wako wa mpira kuwa na wachezaji 22 na kushindana kuingiza goli kwa miguuu.

Huu mfano kumbuka ni wa kanuni (sheria za kibinadamu ambazo tumeziweka wenyewe) na mara kwa mara hufanyiwa marekebisho kulingana za uhitaji.

Mfano sasahivi wanafikiria kupunguza dakika za kucheza ziwe 40 kwa kila kipindi badala ya 45.

Kwa hiyo hizi ni kanuni ambazo tumweziweka na tunazibadilisha muda wowote tutakaotaka
Najaribu kukujengea picha fulani kupitia hiyo mifano ebu jaribu kufikiri zaidi na maanisha Nini?
 
Najaribu kukujengea picha fulani kupitia hiyo mifano ebu jaribu kufikiri zaidi na maanisha Nini?
Jaribu kufafanua au toa mifano mingine.

Ila nilichoelewa ni kwamba Mungu ametuweka tuishi ndani ya sheria zake (mfano sheria za mchezo wa soccer) alafu mchezaji akivunja sheria hizo maana yake ataadhibiwa kwa mujibu wa kosa lake (sawa na sisi kumtenda dhambi Mungu).
 
Mkuu napendekeza usome kitabu HOW DID LIFE GET HERE BY CREATION OR EVOLUTION.
Humo hata hayo ya shetani alitoka wapi yanajibiwa .
Utakipata free kwenye online library WOL.JW.ORG nenda kwenye section ya vitabu.
 
Jaribu kufafanua au toa mifano mingine.

Ila nilichoelewa ni kwamba Mungu ametuweka tuishi ndani ya sheria zake (mfano sheria za mchezo wa soccer) alafu mchezaji akivunja sheria hizo maana yake ataadhibiwa kwa mujibu wa kosa lake (sawa na sisi kumtenda dhambi Mungu).
Namaanisha kadili wachezaji wanavyochua vikali ndio furaha ya mashabiki


Jinsi mechi inavyozidi kua ngumu zaidi ndivyo inavyozidi kuwa tamu zaidi

Try to think in different angles.


Au imagine uko na wanao wanne, ukawambia nataka niwape challenge Mimi naenda kujificha
Ila atakae niona ntampa zawadi.

Ukaenda kujificha mahali ambapo wewe unawaona vizuri wanavyo hangaika . Kukutafuta

Na wewe huwezi fanyachochote kuwasaidia kwa sababu it's a challenge ulioamua wewe licha ya kuwa unao uwezo huo

Mpaka hapo umegundua nini kumuhusu Huyu Mungu.
 
Mkuu napendekeza usome kitabu HOW DID LIFE GET HERE BY CREATION OR EVOLUTION.
Humo hata hayo ya shetani alitoka wapi yanajibiwa .
Utakipata free kwenye online library WOL.JW.ORG nenda kwenye section ya vitabu.
Mkuu asante sana, nitaki down load nikisome.

Lakini issue kama shetani alitoka wapi kwangu siyo issue labda kama atakuwa ameelezewa katika muktadha tofauti na Biblia.

Maana katika biblia inamwelezea shetani kuwa miongoni mwa malaika wa Mungu na kama ni miongoni mwa malaika wa Mungu maana yake ni kwamba Mungi ndiye aliyemuumba mana yeye (Mungu) ndiye muumbaji wa vyote kwa mujibu wa biblia.

Kwa hiyo mimi issue siyo shetani kutoka wapi, ila issue ni uasi wake kwa muumba wake ambao huo uasi labda ulisababisha na kuumbwa bila ukamilifu flani, kama aliumbwa bila ukamilifu flani inakuwaje sasa Muumbaji/Mungu tunamwita ni mkamilifu wa vyote hajawahi kukosea ?.

Ila I promise hicho kitabu nitakisoma
 
Huwezi kutumia mind kuelezea ukuu wa Mungu,since iko limited mnoo. Kitu pekee unacho weza kuelezea ni kile ulicho experience. You have to go beyond the Egoic Mind ili umtambue Mungu.
Mkuu Egoic mind ikoje ebu nifafanulie kidogo.

Lakini pia nikuulize swali fupi : Kama Mungu ndiye aliyetuumba na kutupa akili/maarifa haya, unadhani alukuwa hajui kuwa kuna siku binadamu tutajiuliza maswali kama haya kumuhusu ?
 
Namaanisha kadili wachezaji wanavyochua vikali ndio furaha ya mashabiki


Jinsi mechi inavyozidi kua ngumu zaidi ndivyo inavyozidi kuwa tamu zaidi

Try to think in different angles.


Au imagine uko na wanao wanne, ukawambia nataka niwape challenge Mimi naenda kujificha
Ila atakae niona ntampa zawadi.

Ukaenda kujificha mahali ambapo wewe unawaona vizuri wanavyo hangaika . Kukutafuta

Na wewe huwezi fanyachochote kuwasaidia kwa sababu it's a challenge ulioamua wewe licha ya kuwa unao uwezo huo

Mpaka hapo umegundua nini kumuhusu Huyu Mungu.

Mpaka hapo nimegundua kwamba "Mungu hayo madhaifu aliyomuumba nayo Lucifer/Muasi pamoja na ya Eva (aliyedanganywa na huyo muasi) alikuwa anayatambua fika na alifanya hivo maksudi japo uwezo wa kutoyaumba hayo madhaifu alikuwa nayo ila aliwaumba nayo maksudi.

Nambie kama nipo sahihi hapo ama laah..

Kama nipo sahihi utanambia nikuulize swali moja muhimu sana
 
Mpaka hapo nimegundua kwamba "Mungu hayo madhaifu aliyomuumba nayo Lucifer/Muasi pamoja na ya Eva (aliyedanganywa na huyo muasi) alikuwa anayatambua fika na alifanya hivo maksudi japo uwezo wa kutayaumba hayo madhaifu alikuwa nayo ila aliwaumba nayo maksudi.

Nambie kama nipo sahihi hapo ama laah..

Kama nipo sahihi utanambia nikuulize swali moja muhimu sana
Uko sahihi kabisa uliza
 
Wakuu poleni kwa upambanaji.

Binafsi mimi kuna mda huwa nikitulizaga kichwa changu huwa naanza kujiuliza maswali mengi sana kuhusu mimi (binadamu) na ulimwengu kiujumla (Universe).

Maswali kama sisi (binadamu) ni kina nani,tumetoka wapi asili yetu, kwanini tupo (dhumuni la kuishi), mwisho wetu ama hatima yetu ni nini, Ulimwengu wa vitu je kama sayari, nyota, galaxies zimekuwepo vipi na nini hasa mwisho wake.

Hapo juu ni baadhi tu ya maswali ambayo huwa naiuliza sana akili yangu ikiwaga katika hali ya utulivu.

Lakini cha kusikitisha ni kwamba, katika maswali yote hayo ambayo huwa najiuliza, sijawahi kupata jibu la uhakika kuniridhisha kuhusu hayo maswali yangu.

Nimekuwa nikifanya bidii kubwa sana kupata majibu ya maswali yangu kupitia usomaji wa majarida au vitabu vihusuvyo historia,sayansi, dini na Falsafa lakini kote bado sijapata majibu ya kuniridhisha tofauti na kuambulia majibu ya kinadharia tu ambayo yana strength kiasi chake lakini pia yana weakness sehemu nyingi tu.

Na nikiri wazi tu kuwa katika usomaji wangu wa nadharia hizo zote (historia, sayansi, dini, falsafa) sehemu ambayo nimeanza kuiamini kunipa majibu ya maswali yangu ni kwenye DINI.

Nikiwa na maana nimeanza kuamini kwamba uwepo na sisi tuliohai na visivyo hai hapa ulimwenguni ni matokea ya Uumbaji ya nguvu kubwa sana inayoitwa MUNGU/ALLAH kama ambavyo dini nyingi zinaelezea nguvu hiyo.

Na leo maswali yangu yanajikita huko kwenye hiyo nguvu (Mungu) maana nimeanza kuiamini lakini pia kila nisomapo BIBLIA (mimi mkristo) inanipa maswali chungu nzima.

Sasa leo swali langu limejikita kwenye UKAMILIFU wa MUNGU.

Naombeni wasomaji mnielewe kuwa sina maana ya kukufuru (maana mara nyingi niulizapo maswali kuhusu MUNGU huwa naambiwa nakufuru) bali mimi nataka kujifunza zaidi kumuhusu huyu Mungu.

Dini nyingi (hasa Ukristo na uislamu) zimekuwa zikimwelezea Mungu kuwa ni Mkamilifu sana,mwenye nguvu nyingi sana, uwezo na akili zake hazichunguziki, hashindwi na chochote n.k.

Je hilo lina ukweli ? kupitia Biblia mimi nimeanza kudhani kwamba huenda kweli Mungu ana nguvu nyingi sana ila siyo zote, ana uwezo mkubwa sana ila siyo uwezo wote,ana maarifa mengi sana ila siyo maarifa yote, ana ukamilifu mwingi sana ila siyo ukamilifu wote n.k

Nasema haya ni kutokana na maswali yafuatayo :

1. Kama Mungu ana ukamilifu wote, kwanini sasa alimuumba malaika (Lucifer/shetani) alafu badae akaja kumuasi?
Kama Shetani/Lucifer aliasi maana yake ni kwamba Mungu alimuumba huyu kiumbe akiwa na madhaifu kadhaa na ndiyo maana alishindwa kuitii amri/mamlaka ya muumbaji wake.

Kama Mungu angelikuwa na ukamilifu wote, basi malaika wote wangelikuwa wameumbwa katika namna ya utii pekee, uasi usingetokea na huo uasi unadhihirisha kwamba Mungu aliwaumba hawa malaika wakiwa na udhaifu flani, hawakuwa na uimara wote.

2. Uumbaji wa Eva (Hawa) unaonesha kulikuwa na madhaifu pia.
Katika Biblia takatifu kwenye kitabu cha mwanzo, kuna mistari inaeleza kuwa "Mungu alimpa usingizi mzito Adam, alafu akabandua sehemu ya ubavu wake na kumfanya/kumuumba mwanamke (Hawa/Eva)".

Alafu Mungu akamwambia Adam kuwa huyu mwanamke atakuwa msaidizi wako

Lakini ni huyo huyo mwanamke ambae shetani (kwenye umbo la nyoka) alienda kumdanganya akachukua matunda ya mti walioambiwa asile yeye akala na akampelekea na mumewe (Adam) pia akala.

Lakini Mungu alivyomuuliza Adam kwanini umekula matunda ya mti ambao nilikwambia usile, Adam alijibu kuwa "Ni huyo mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea nikala".

Tukio hili linadhihirisha kuwa Mungu alimpa Adam msaidizi (Hawa) ambae ni dhaifu sana na ndiyo maana alisababisha dhambi ikaenda hadi kwa Adam.

Na huenda kama Mungu angelikuwa amempa Adam msaidizi imara asiye na madhaifu basi ile dhambi ya kula tunda ingeepukika.

Uko wapi sasa ukamilifu wote wa Mungu ikiwa aliweza kuwaumba malaika dhaifu (ambao walikuja kumuasi) na pia bado akampa Adam msaidizi dhaifu kabisa ambaye alisababisha dhambi imwendee hadi Adam?

Kwa leo naombeni comment zenu zinifunze kuhusu hilo tu (La ukamilifu wa Mungu) alafu mengine nitauliza siku nyingine, na mengine nitakuwa nauliza humo humo kwenye comments zenu.

NB: Naamini Mungu yupo, kutokana na baadhi ya vitu ninavyoviona ulimwenguni (hasa uumbaji/creation) ambapo kuna baadhi ya vitu hasa sayansi inakosa majibu ya kuridhisha, ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.

Karibuni mnifunze.
Mkuu

Ni KWELI super natural power AMBAYO waliamua kuiita Mungu IPO/yupo!


Kinachsikitisha ni kwamba:-


Africa maarifa kumhusu yaliletwa karne ya 18,ina maana waafrica waliishi miaka 1800 bila kujua Mungu wala Dini hizi za ukristo na uislam na SASA tuna miaka 223 TANGU tumfaham MUNGU wa kigeni tuliyeletewa maarifa yake!!!
NB
2023-1800=223 miaka ya maarifa ya Mungu mpya!!


Ni HIVYO tu mkuu anzia hapo kutafakari kwamba maisha ya baby zetu yalikuaje kuanzia mwaka 0 HADI 1800!!?

Tafakari!
 
Uko sahihi kabisa uliza
Kama Mungu alimuumba Lucifer na madhaifu flani Labda ambayo yalimfanya ashindwe kuwa mtiifu automatically mpaka akaasi, Sasa huoni kuwa hukumu (ya jehanam) aliyopewa shetani na waasi wenzie itakuwa ya uonevu ?

Yaani wewe muumbaji, umekiumba kiumbe ambacho unajua kuwa kina udhaifu flani, na huo udhaifu umeuweka kwa maksudi kwake, na unajua kabisa huo udhaifu uliouweka kwake utam sababishia afanye kosa flani,alafu wewe muumbaji uje umuhukumu tena adhabu kali kwa kosa ambalo ni matokeo ya udhaifu wa maksudi wakati wa uumbaji, we huoni kuwa hiyo hukumu utakayomuhukumu kwa kosa hilo itakuwa ni uonevu wa wazi kabisa ?

The same theory apply to Eva, Alijua kabisa ameemumba Eva na madhaifu ambayo yalipelekea akaingia kwenye udanganyifu wa Nyoka akafanya dhambi, alafu uwahukumu Adam na Eva kwa matokeo ya udhaifu ulioweka ndani yao, that means wewe muumabaji utakuwa mwonevu wa kiwango cha juu sana
 
Mkuu

Ni KWELI super natural power AMBAYO waliamua kuiita Mungu IPO/yupo!


Kinachsikitisha ni kwamba:-


Africa maarifa kumhusu yaliletwa karne ya 18,ina maana waafrica waliishi miaka 1800 bila kujua Mungu wala Dini hizi za ukristo na uislam na SASA tuna miaka 223 TANGU tumfaham MUNGU wa kigeni tuliyeletewa maarifa yake!!!
NB
2023-1800=223 miaka ya maarifa ya Mungu mpya!!


Ni HIVYO tu mkuu anzia hapo kutafakari kwamba maisha ya baby zetu yalikuaje kuanzia mwaka 0 HADI 1800!!?

Tafakari!
Kwa kweli hilo ni jambo lingine la msingi kabisa ambalo linahitaji ufafanuzi wake kutoka kwa hawa wanaojiita wanathiolojia wa Mungu Mpya.

Na inabidi waje hapa waelezee.

Lakini kabla hiyo imani ya Mungu mpya kuletwa, historia inaonesha kuwa Mababu zetu (Waafrica Weusi) walikuwa na imani zao kabla hata hizo za Mungu mpya kuletwa.

Na imani hizo za kale za Mababu zetu, zimekuja kuitwa kuwa ni za kimizimu/kishetani.

Lakini ninachoshangaa ni kwamba hizo imani inaonekana zilikuwa zinawasaidia, yaani walikuwa wakiomba chochote kwenye mizimu yao walikuwa wanapata.

Lakini baada ya kuwasili kwa Imani za Mungu mpya (aliyeletwa na wakoloni) ikaonekana hiyo imani ya mababu zetu ilikuwa ni kichawi na ni haramu/chukizo kwa Mungu.

Sasa mimi nauliza, wale mababu zetu waliokufa kabla ya kuwasili kwa imani za Mungu mpya, hukumu yao siku ya kiama itakuwaje ?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom