GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,871
Naanza na ANGALIZO kuna wale ‘ Wapuuzi ‘ fulani ambao huwa wanadhani ninapokuja hapa na taarifa za Kuihusu Yanga SC yangu / yetu basi labda nakuwa ‘ nazusha ‘ tu au huwa pengine nakuwa na ‘ Agenda ‘ yangu binafsi na hata kuhisi kuwa natumika ‘ Kipropaganda ‘ Kuimaliza Yanga SC hasa hapa JamiiForums.
Kama kuna mwana Yanga SC naamini kabisa kuwa leo asubuhi alimsikia ‘ Mubashara ‘ kabisa Makamu Mwenyekiti wetu akizungumza kupitia Chombo cha Redio cha Efm katika Kipindi chao Kizuri cha ‘ Sports Headquarters ‘ na Kuitoa hii ‘ Kauli ‘ ya Kutia huruma ( ambayo naenda Kuinukuu hapa chini ) hasa kwa Wajumbe wa Shirikisho la Soka Barani Afrika ( CAF ) ambao leo Saa 2 za Usiku watakuwa ‘ wanazichagua ‘ Timu za Kucheza katika hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho ambalo Yanga SC imeangukia huko baada ya ‘ Kufurumushwa ‘ kwa Goli za Zawadi la Mchezaji wetu ‘ mbovu ‘ Makame.
“ Ni kweli kabisa Ndugu Mtangazaji kwamba leo mida ya Saa 2 Usiku Yanga SC tutajua tutacheza na nani ila naomba Mungu Yanga SC tupangiwe na Timu ambazo tutazimudu na naamini Mwenyezi Mungu atakuwa upande wetu “.
Nikisema kuwa Yanga SC kwa sasa hatuna Viongozi bali tuna ‘ Wahuni ‘ tupu muwe mnanielewa An Eagle sawa?
Na kuna ' Mtaalam ' wangu Mmoja amenitabiria na kusema kuwa Yanga SC yetu leo katika upangaji huo tunaendea ' Kuangukia ' kwa Timu kali na Kabambe za kutoka katika nchi hizi Tatu Kubwa Kimpira barani Afrika na ambazo hata Ulaya zimeshapeleka sana Wachezaji wake wengi wa Kulipwa hivyo ni kama tu vile Yanga SC ' tumeshatolewa ' huko na sasa tujikite zaidi katika Ligi ambayo na yenyewe pia kwa mwenendo wa Simba SC huko pia hatuna chetu labda tukibahatisha sana Kubeba Kombe mwaka huu basi ama litakuwa ni la Mapinduzi au la Kugombe Vyura wakubwa waliopatikana kwa Uwingi Klabuni Kwetu kutokana na hizi Mvua Kubwa zinazoendelea kwa sasa Jijini Dar es Salaam.
Nchi zenyewe ni:
Misri / Congo DR
Algeria / Cameroon
Tunisia / Nigeria
Kazi ipo mwaka huu na Yanga SC yetu Kudadadeki!
Kama kuna mwana Yanga SC naamini kabisa kuwa leo asubuhi alimsikia ‘ Mubashara ‘ kabisa Makamu Mwenyekiti wetu akizungumza kupitia Chombo cha Redio cha Efm katika Kipindi chao Kizuri cha ‘ Sports Headquarters ‘ na Kuitoa hii ‘ Kauli ‘ ya Kutia huruma ( ambayo naenda Kuinukuu hapa chini ) hasa kwa Wajumbe wa Shirikisho la Soka Barani Afrika ( CAF ) ambao leo Saa 2 za Usiku watakuwa ‘ wanazichagua ‘ Timu za Kucheza katika hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho ambalo Yanga SC imeangukia huko baada ya ‘ Kufurumushwa ‘ kwa Goli za Zawadi la Mchezaji wetu ‘ mbovu ‘ Makame.
“ Ni kweli kabisa Ndugu Mtangazaji kwamba leo mida ya Saa 2 Usiku Yanga SC tutajua tutacheza na nani ila naomba Mungu Yanga SC tupangiwe na Timu ambazo tutazimudu na naamini Mwenyezi Mungu atakuwa upande wetu “.
Nikisema kuwa Yanga SC kwa sasa hatuna Viongozi bali tuna ‘ Wahuni ‘ tupu muwe mnanielewa An Eagle sawa?
Na kuna ' Mtaalam ' wangu Mmoja amenitabiria na kusema kuwa Yanga SC yetu leo katika upangaji huo tunaendea ' Kuangukia ' kwa Timu kali na Kabambe za kutoka katika nchi hizi Tatu Kubwa Kimpira barani Afrika na ambazo hata Ulaya zimeshapeleka sana Wachezaji wake wengi wa Kulipwa hivyo ni kama tu vile Yanga SC ' tumeshatolewa ' huko na sasa tujikite zaidi katika Ligi ambayo na yenyewe pia kwa mwenendo wa Simba SC huko pia hatuna chetu labda tukibahatisha sana Kubeba Kombe mwaka huu basi ama litakuwa ni la Mapinduzi au la Kugombe Vyura wakubwa waliopatikana kwa Uwingi Klabuni Kwetu kutokana na hizi Mvua Kubwa zinazoendelea kwa sasa Jijini Dar es Salaam.
Nchi zenyewe ni:
Misri / Congo DR
Algeria / Cameroon
Tunisia / Nigeria
Kazi ipo mwaka huu na Yanga SC yetu Kudadadeki!