Na Sisi tuwasusie madaktari kuwapa huduma

tatizo viongozi wenu dhaifu wamewaambukiza udhaifu wa kufikiri.we never said kada yetu ni superior to other kadas kama una ona kuna umuhimu wa kutugomea madaktari then do it sio ukae kwenye keyboard na kuandika pumba.take action in what u believe in,that s what we are doing
 
Hawa MaDR wanadai upuuzi mbona hawawasemei ma-Medical wa vijijini Manesi au Wanajeshi? Nashauri waache kazi kwa amani kwani wanaviji-Dispensary na kutoa mimba.
Hivi bajeti ya Wizara ya Fedha imepita sasa tumee wapi? Au @ MGONJWA ALIPE 100,000/ kundidikisha jina/ Daftari? Mm bbaunga mkono madaktari walaaniwe luucgga ya kususiwa


Laana yako dhidi ya madaktari ikurudie kifuani mwako na uzao wako mara mia na kesho usukumizwe kwenye tanuru la moto. Mfumo tulio nao sasa si wa kusemeana kila mtu anabeba msalaba wake mwenyewe. Ndiyo maana walio nacho wanajiongezea na kuwakaba wengine. Bila shaka hujawahi kuugua wewe ukachungulia kaburi. Hujaona wagonjwa wa maradhi yanayoambukiza wakihudumiwa na hawa madaktari ambao wewe unawalaani. Mchango wako ni nini kwa nchi na wananchi wa nchi hii hata ujipe haki ya kulaani madaktari wanaodai haki yao?
Kwa taarifa yako nchi za wenye akili madaktari hawagomi kwa kuwa wenye akili hawa wanajua kuwa wakiumia (kama mwalimu wa sayansi aliyepelekwa Kairuki) wakiwa kazini na madaktari wamegoma hawatatibiwa. Badala yake kada nyingine za wafanyakazi ndizo zinagoma kwa niaba ya madaktari. Wewe ulitaka waendelee kuonewa? Kama wewe unapenda kuonewa ni shauri lako. Pili ni jukumu la serikali tena serikali peke yake kutoa huduma za afya na wala sio madaktari. Hao ndio wanaostahili lawama na kwa kweli laana zote za Watanzania kwa kutokosesha matibabu. Ndiyo maana hao FISI-WENU hawakosi kujisifu kwa kujenda dispensari katika kampeni zao. Ni majukumu yao. Sijawahi kuona hoja dhaifu kama yako mkuu. Unafadhaisha kuonekana kwenye jukwaa kama hili. Wewe hakika ni great sinker- unazamisha jukwaa!
 
Nije kwa madaktari, hata mkigoma miaka yote, seriki ya CCM haitawalipa hata siku moja mishahara mnayodai, nani kwadanganya CCM inaweza kuwalipa Sh. 3.5 Millioni kwa mwezi na marupurupu mengine? Kwanza mlichemka, mnadai pesa nyingi sana kwa wakati mmoja, sijui nani aliwashauri, mlipenda sifa za kuitwa Drs, fanyeni kazi yenu!
Halafu ikifika 2015 mtavishwa Magwanda ya Kijani na kupiga kura huku mnashangilia! SUBIRINI 2015 NA MCHUKUE MAAMUZI MAZITO, MTAKUWA KAMA WAALIMU MSIPOANGALIA.

Mkuu hoja yako dhidi ya madaktari inaudhi na dhaifu kupita maelezo. Hivi kweli great thinker unapenda kutuaminisha kuwa madaktari walisomea utaalam huo kwa vile tu wanapenda kuitwa madaktari, LOL! Kama ndicho kigezo ulichotumia kuusaka utaalam ulio nao ni aibu. Hawa ni watu waliojitolea sehemu kubwa sana ya maisha yao kusoma masomo magumu (unabisha? wewe yalikushinda na wivu unakupata). Sio masomo tu lakini pia wanaishi maisha magumu ambapo wakati wowote wanaweza kujikuta wako kazini (angalia kunapotokea dharula au maafa). Siku zote wako kwenye hatari ya kuambukizwa magonjwa yote hatari ambayo unaweza kuyafikiria duniani. Huko ni kujitoa kwa ajili ya kuhudumia na wala si kutaka jina la udaktari.
Wanajamvi, mtoa hoja aseme kama yuko tayari kwa shilingi hizo milioni tatu na nusu aende Muhimbili kwa mwezi mmoja tu. Wala yeye asitibu maana si daktari, aambatane tu na madaktari katika shughuli zao. Wakiwahudumia wagonjwa naye awepo usiku na mchana. Zamu naye apewe na ile nyumba ya dakatari aliyepanga Malambamawili ahamie huko ili aje Muhimbili kila siku kwa daladala. Akutane na wagonjwa na kifua kikuu, ukimwi, kipindupindu, kimeta, vidonda vilivyooza (vinacyotoa usaha na harufu mbaya), na magonjwa yanayofanan na hayo. Halafu aje aeleze jukwaa kama hizo fedha zinatosha. Kwanini tuandikie mate wakati wino umesheheni.
 
Jamani wadau kwa jinsi hali ilivyo kama wao wamekataa kutupa huduma na sisi tuwasusie kuwapa huduma kama wao wanavyofanya kwa jamii. Wahasibu wasiwalipe mshahara yao na hata huduma nyingine pia tuwatose. Tusiwafundishe watoto wao hata wakija na hela yao na huduma nyinginezo...mgogoro wauletao wanaoumia ni watanzania maskini na sip viongozi wa serikali. Mgogoro huu Pinda. Hawa ghasia.Mwinyi aathiriki nao n.k

Waalimu tutagoma kuwapa madaktari huduma kwa mshahara ganu tunaopata?
 
Mkuu hoja yako dhidi ya madaktari inaudhi na dhaifu kupita maelezo. Hivi kweli great thinker unapenda kutuaminisha kuwa madaktari walisomea utaalam huo kwa vile tu wanapenda kuitwa madaktari, LOL! Kama ndicho kigezo ulichotumia kuusaka utaalam ulio nao ni aibu. Hawa ni watu waliojitolea sehemu kubwa sana ya maisha yao kusoma masomo magumu (unabisha? wewe yalikushinda na wivu unakupata). Sio masomo tu lakini pia wanaishi maisha magumu ambapo wakati wowote wanaweza kujikuta wako kazini (angalia kunapotokea dharula au maafa). Siku zote wako kwenye hatari ya kuambukizwa magonjwa yote hatari ambayo unaweza kuyafikiria duniani. Huko ni kujitoa kwa ajili ya kuhudumia na wala si kutaka jina la udaktari.
Wanajamvi, mtoa hoja aseme kama yuko tayari kwa shilingi hizo milioni tatu na nusu aende Muhimbili kwa mwezi mmoja tu. Wala yeye asitibu maana si daktari, aambatane tu na madaktari katika shughuli zao. Wakiwahudumia wagonjwa naye awepo usiku na mchana. Zamu naye apewe na ile nyumba ya dakatari aliyepanga Malambamawili ahamie huko ili aje Muhimbili kila siku kwa daladala. Akutane na wagonjwa na kifua kikuu, ukimwi, kipindupindu, kimeta, vidonda vilivyooza (vinacyotoa usaha na harufu mbaya), na magonjwa yanayofanan na hayo. Halafu aje aeleze jukwaa kama hizo fedha zinatosha. Kwanini tuandikie mate wakati wino umesheheni.


Mkuu, elewa kwamba siyo kila hoja ya mtu lazima mtu mwingine aone ni nzuri au mbaya. Hoja yangu kwako itakuwa dhaifu lakini kwa wengine siyo dhaifu! Na kwa taarifa yako sijawahi hata kufikiria maishani nisome huo udaktari. Unataka kuniambia sisi tuliosoma Engineering (Civil) ni masomo rahisi? Kipimo cha urahisi ni nini? Aliyesoma Geology nae kasoma masomo rahisi. Nakubaliana na wewe kuwa lazima watu walipwe kulingana na ugumu wa kazi. Point ni kwamba, kani kada nyingine serikalini zinalipwa mishahara mikubwa? Kwa taarifa yako, hata MD wa kawaida Hospitali za Binafsi mshahara wake hauzidi 1.5 M kama unabisha lete hoja. Nikuulize kitu kimoja cha msingi sana. NI KADA ZIPI ZINAZOFANYA KAZI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU? NI MADAKTARI PEKE YAO? KWANI POLISI, WAALIMU NA KADA NYINGINE HIZO HAZINA MAISHA MAGUMU? KAMA WEWE NI DAKTARI BASI ELEWA KUWA SULUHISHO NI KUITOA SERIKALI YA MAGAMBA NA SI VINGINEVYO. MTANDELEA KULIA TU KAMA MTAENDELEA KUWACHAGUA CCM. NGOJA NIENDE ZANGU KWA PROJECTS ZANGU, MJASIRIAMALI MIMI, NAONA UNANIPOTEZEA MUDA TU NA HASIRA ZAKO!
 
Kanywe zile dawa za ugonjwa wa akili ninazokupa kila mwezi ukalale maana naona kale kaugonjwa kanataka kuibuka! Teh teh By the way zinaitwa Haloperidol!!!

Wewe ndo mgonjwa wa akili ambae unashangilia watu kufa kwa sababu ya madai ya pesa! Huoni hata aibu kutoa haya mambo. Dr. Ulimboka kabigwa na kupelekwa Emergency hakuna mtu zaidi ya DR. Mwafongo, na kapelekwa MOI!. Sasa piga picha kama ni mama yako au baba yako ndo yuko katika hali hiyo ni nani angemtibu. Nahisi wewe ni DR. na ulikula kiapo, then hii inaigia akilili? Naunga mkono madai na si kwa mgomo, SHAME ON YOU! NA BAADA YA MUDA RUDINI JAMVINI MTUELEZE KAMA HIZO PESA MTAKAZOLIPWA ZITARUDISHA UHAI WA WALIOKUFA! ELIMU YENU HAIJAWASAIDIA, SAWASA TU NA MAGAMBA!
 
Aaah, umegundua eeh, hata mie nilitaka kumueleza hivyo hivyo, kumbe na ww huwa unamtibu?!


Wewe ndo mgonjwa wa akili ambae unashangilia watu kufa kwa sababu ya madai ya pesa! Huoni hata aibu kutoa haya mambo. Dr. Ulimboka kabigwa na kupelekwa Emergency hakuna mtu zaidi ya DR. Mwafongo, na kapelekwa MOI!. Sasa piga picha kama ni mama yako au baba yako ndo yuko katika hali hiyo ni nani angemtibu.

Nahisi wewe ni DR. na ulikula kiapo, then hii inaigia akilili? Naunga mkono madai na si kwa mgomo, SHAME ON YOU!
NA BAADA YA MUDA RUDINI JAMVINI MTUELEZE KAMA HIZO PESA MATAKAZOLIPWA ZITARUDISHA UHAI WA WALIOKUFA! ELIMU YENU HAIJAWASAIDIA, SAWASA TU NA MAGAMBA!
 
Katika hili Madaktari waendelee hadi wananchi washituke, watu wa reli huwa wanagoma wakati wasafiri wameshakata tiketi na hapo ndipo wakubwa huwa wanashituliwa na kelele za wasafiri, katika hili mtuhimiwa wa kwanza ni serikali na itashituka pale tu wananchi watakapoamka na kuanza kupaza sauti zao, hili la kulaumu madkatari hatuwatendei haki kabisa, wananchodai ni pamoja na huduma bora kwa hao watu maskini ambao hawana uwezo, sasa ukiwatuhumu tuu ni sawa na kuwa dhaifu
 
Back
Top Bottom