Na Raia Mwema nalo....

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,927
Habari za kuaminika zinasema kuwa gazeti la Rai Mwema linatarajiwa kumuomba Radhi Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz kufuatia makala iliyotoka kwenye gazeti hilo wiki chache zilizopita.

Bw. Rostam alitoa tishio la kuchukua hatua za kisheria dhidi ya gazeti hilo wakati ule ule alipotoa tishio la kushtaki gazeti la MwanaHalisi. Hata hivyo, wachunguzi wa mambo mbalimbali wamegawanyika kama uamuzi wa kumuomba radhi ni sahihi au wangesubiri aende mahakamani kwanza.

Bw. Rosam anadai kuwa aliandikwa vibaya na kuchafuliwa hadhi na heshima yake na gazeti hilo katika makala iliyoandikwa na Bw. Joseph Mihangwa toleo la April 2 na maendelezo yake kwenye April 9.

Hata hivyo, Bw. Rostam hakuchachamalia makala iliyoandikwa na Lula wa Ndali Mwananzela yenye kichwa cha habari "Sipendi Rostam atisike Kiberiti Bungeni". Makala hiyo ilijibiwa wiki moja baadaye na mtu ajiitaye "Joseph Wambura" katika makala yake "Tusimdharau, Rostam hatikisi kiberiti".
 
Habari za kuaminika zinasema kuwa gazeti la Rai Mwema linatarajiwa kumuomba Radhi Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz kufuatia makala iliyotoka kwenye gazeti hilo wiki chache zilizopita.

Bw. Rostam alitoa tishio la kuchukua hatua za kisheria dhidi ya gazeti hilo wakati ule ule alipotoa tishio la kushtaki gazeti la MwanaHalisi. Hata hivyo, wachunguzi wa mambo mbalimbali wamegawanyika kama uamuzi wa kumuomba radhi ni sahihi au wangesubiri aende mahakamani kwanza.

Bw. Rosam anadai kuwa aliandikwa vibaya na kuchafuliwa hadhi na heshima yake na gazeti hilo katika makala iliyoandikwa na Bw. Joseph Mihangwa toleo la April 2 na maendelezo yake kwenye April 9.

Hata hivyo, Bw. Rostam hakuchachamalia makala iliyoandikwa na Lula wa Ndali Mwananzela yenye kichwa cha habari "Sipendi Rostam atisike Kiberiti Bungeni". Makala hiyo ilijibiwa wiki moja baadaye na mtu ajiitaye "Joseph Wambura" katika makala yake "Tusimdharau, Rostam hatikisi kiberiti".



Wacha tuone .Kumbe sasa MwanaHalisi ni kidume zaidi .Ulimwengu kaogopa nini ? Wacha kwanza tuone matendo ndipo tuanze debate hapa .
 
Waliogawanyika kuhusu usahihi wa kuomba radhi ni watu wa nje au ndani ya raia mwema?
 
Wacha tuone .Kumbe sasa MwanaHalisi ni kidume zaidi .Ulimwengu kaogopa nini ? Wacha kwanza tuone matendo ndipo tuanze debate hapa .

Lunyungu,

Hapa hakuna cha ukidume au nini, ni suala la kama walichoandika wanaamini ni sahihi au la. Kama raiamwema wamegundua wameandika habari ambayo ina makosa, naamini wana wajibu wa kuomba msamaha hata kama mhusika ni fisadi.

Hivyo hivyo kwa Mwanahalisi kama wanaamini walichoandika ni sahihi, sioni kwanini wababaike na kuomba msamaha?

Gazeti wanatakiwa wa report habari na sio ku kutengeneza habari.
 
its called libel. the paper might find itself very insolvent when it comes to paying this man.... On sound legal advise watakuwa wameona makosa yao... its not a matter of opinion or fact but rather evidence of allegations, lack of which leads to the Claimant winning the suit and Mwanahalisi paying over 3Billion. its the LAW.hehehehe. I love it.
 
wachunguzi wa nje... sijui ndani kukoje.

Tusubiri tuone gazeti lao la wiki hii kama litaandika chochote kuhusiana na hili. Kwa maoni yangu wanastahili kuutumia ushahidi mbali mbali dhidi ya tuhuma za RA pamoja na ule wa ripoti ya Mwakyembe kuhusiana na ufisadi wa Richmond ili kupambana naye ili afichue yale aliyotaka kuzungumza bungeni na akakataliwa.
 
Kama hawajapewa barua ya kutakiwa kuomba msamaha na Rostam, ni vema wakachapisha kwa hiari yao usasahihi sehemu anayolalamikia na kuomba radhi kwa kukosea kuchapisha, bila kusubiri kulazimishwa kuomba msamaha kama wanajua hilo kosa lao. Then baada ya hapo wammng'ang'anie kidhani kumwandika Rostam na deal zake mpaka wamnyake tena sawasawa.




____________________________
 
Kama hawajapewa barua ya kutakiwa kuomba msamaha na Rostam, ni vema wakachapisha kwa hiari yao usasahihi sehemu anayolalamikia na kuomba radhi kwa kukosea kuchapisha, bila kusubiri kulazimishwa kuomba msamaha kama wanajua hilo kosa lao. Then baada ya hapo wammng'ang'anie kidhani kumwandika Rostam na deal zake mpaka wamnyake tena sawasawa.




____________________________

Wakipata wakili mzuri kama Lissu wanaweza kuamua kutoomba msamaha na kuigeuza hii kesi kuwa ya RA badala ya Raia Mwema na ushahidi uko belele na wanaweza kuwaita wajumbe wa kamati hiyo kama mashahidi wa kutetea walichoandika dhidi ya RA. Halafu wakamchokonoa ili tujue ni kipi alichotaka kusema bungeni na kamati ya CCM bungeni ikamkataza kufanya hivyo.
 
hapo patam sijui itakuaje???Lakinikwa nini atumie ubavu kuombwa msamaha??!! kwa nini asiende na ushahidi wake pale Idara ya Habari?? Then hayo magazeti ndio yamue kumuomba msamaha?? Hivi anafikiri ni kitu gani Wa-Tanzania kwa sasa hawajui dhidi yake?? Ameshidwa kupambana na wbabe wenzake (CCM MAFISADI) sasa naona anaalizia hsira zake kwenye magazeti mbayo ki mantiki bado machanga..anyways, Kazi ipo
 
makanjanja wasitumie nafasi ya kutuhimiwa viongozi kwa ufisadi na kuandika pumba.

mtu anaelikoroga kwa makusudi ni jukumu lake alinywe

si busara kuhumhukumu mtu kwa hisia.

ikiwa ra anaona kama hajafanyiwa haki na aende na makanjanja na wao wajiandae kama ni wa kweli.



ufisadi ni pamoja kuwalisha wananchi habari zisizona uhakika tupambane na aina zote za ufisadi
 
Wakipata wakili mzuri kama Lissu wanaweza kuamua kutoomba msamaha na kuigeuza hii kesi kuwa ya RA badala ya Raia Mwema na ushahidi uko belele na wanaweza kuwaita wajumbe wa kamati hiyo kama mashahidi wa kutetea walichoandika dhidi ya RA. Halafu wakamchokonoa ili tujue ni kipi alichotaka kusema bungeni na kamati ya CCM bungeni ikamkataza kufanya hivyo.


Hivi Lissu amewahi kushinda kesi gani kubwa? Mimi nimemsikia zaidi kwenye siasa kuliko kwenye sheria. Anyone with his data?




___________________________
 
Hivi Lissu amewahi kushinda kesi gani kubwa? Mimi nimemsikia zaidi kwenye siasa kuliko kwenye sheria. Anyone with his data?




___________________________


Yatakushinda! Tundu Antipas Lissu ni mwanasheria wa mazingira aliyebobea anayefahamika ndani na nje ya Tanzania. Hebu google search jina lake tu utapata habari zake.

Asha
 
Yatakushinda! Tundu Antipas Lissu ni mwanasheria wa mazingira aliyebobea anayefahamika ndani na nje ya Tanzania. Hebu google search jina lake tu utapata habari zake.

Asha



Asha,
Naona unakuwa na shida kidogo na postings zangu. Mimi nimeuliza tu swali kwa nia njema kabisa ya kujua naona wewe ukadakia kishari-shari.

Mimi ninavyojua ni kuwa Tundu ni mwanasheria wa mambo ya mazingira, maana nakumbuka alitajwa tajwa sana wakati wa kesi ya Buliyankulu. Lakini sijui kabisa kesi zake na ku-google kesi za TZ ni kumnyima mtu haki yake maana hazitakuwepo zote if at all kama zitakuwepo. Ninachotaka ni kufahamu ni kuwa, ingawa yeye amejikita zaidi kwenye mazingira, labda pia ni kibaka kwenye criminal na civil law ambayo hapa ndio inayohitajika. Ndio maana nilitaka mtu anayemfahamu vema atueleze otherwise, akina kibenea wanahitaji watu kama akina Marando n.k. I hope umenielewa na pia umeelewa kuwa kwenye sheria nako kuna ku-speshalaizi. Tuendelee na mjadala wetu kiuungwana.



___________________________
 
Asalamu alaykum.

Kama kilichondikwa ni cha kweli basi sioni kama kuna haja ya kuanza kubabaika kwa kuomba radhi.
muhimu kusimamia ukweli lakini kama waliaondika hawana uhakika na wamezua basi kuomba radhi ni must na ni uungwana maana kumzulia mtu sio vizuri na ni makosa kimaadili kumchafua mtu katika jamii.
 
Asha,
Naona unakuwa na shida kidogo na postings zangu. Mimi nimeuliza tu swali kwa nia njema kabisa ya kujua naona wewe ukadakia kishari-shari.

Mimi ninavyojua ni kuwa Tundu ni mwanasheria wa mambo ya mazingira, maana nakumbuka alitajwa tajwa sana wakati wa kesi ya Buliyankulu. Lakini sijui kabisa kesi zake na ku-google kesi za TZ ni kumnyima mtu haki yake maana hazitakuwepo zote if at all kama zitakuwepo. Ninachotaka ni kufahamu ni kuwa, ingawa yeye amejikita zaidi kwenye mazingira, labda pia ni kibaka kwenye criminal na civil law ambayo hapa ndio inayohitajika. Ndio maana nilitaka mtu anayemfahamu vema atueleze otherwise, akina kibenea wanahitaji watu kama akina Marando n.k. I hope umenielewa na pia umeelewa kuwa kwenye sheria nako kuna ku-speshalaizi. Tuendelee na mjadala wetu kiuungwana.



___________________________

Kwani umeajiri mtu wa kukufanyia research hapa? Fanya research mwenyewe ......grrrrrrr
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom