Na plan ya kuwa na e-commerce website ya mkoa mmoja tu

Mapensho star

JF-Expert Member
Jun 30, 2016
3,052
4,074
Kuna hii fursa ambayo nimekuwa na lengo la kuifanya mda mrefu
kuna jambo ambalo linanisukuma kuanzisha hii e-commerce website sababu kubwa ni kuongezeka kwa watumiaji wa internet
nilijaribu kuanzisha siku zilizopita lakini nilipata changamoto ya promotion kuifanya iwe brand
nikashindwa kufanya promotion kama wanayoitumia wenzangu bajeti yangu ni ndogo
Ila sasa nimekuja na wazo hili kutengeneza website ambayo itawakutanisha wauzaji na wanunuzi wa mkoa mmoja
nataka niweke nguvu kwa mkoa mmoja
sasa ata hivyo nimekuja kuomba ushauri kwa ambao wana e-commerce au wanauzoefu na hili

ni njia zipi zinaweza kunisaidia kwa bajeti ndogo kuifanya e-commerce iwe brand kwa mkoa mmoja
 
Wazo zuri mkuu,

1. Lenga kwenye majiji kwakuwa watumiaji wa mitandao ni wengi
2. Bidhaa zitakazo kuwa humo ziwe za kuwelenga vijana zaidi kwakuwa wao ndio watumiaji wakubwa wa mitandao
3. Umeuliza ni njia ipi utumie kutangaza web yako iwe ya mkoa mmoja, tumia radio za mikoa. Kuna baadhi ya mikoa kuna radio ambazo hazishiki mikoa mingine

Maswali:
1. Bidhaa atakuwa anauza nani? wewe au member ndio watakuwa wanaweka bidhaa zao kama ebay
2. Unaposema budget ndogo ni sh ngapi? ili mtu aweze kukusaidia kimawazo utangaze katika njia ambayo inaendana na budget yako
 
Hilo wazo , ninalo muda sana , changamoto kubwa watu bado wanaamini kufanya mambo manualy, wengi wanajua ku google tu
 
Wazo zuri mkuu,

1. Lenga kwenye majiji kwakuwa watumiaji wa mitandao ni wengi
2. Bidhaa zitakazo kuwa humo ziwe za kuwelenga vijana zaidi kwakuwa wao ndio watumiaji wakubwa wa mitandao
3. Umeuliza ni njia ipi utumie kutangaza web yako iwe ya mkoa mmoja, tumia radio za mikoa. Kuna baadhi ya mikoa kuna radio ambazo hazishiki mikoa mingine

Maswali:
1. Bidhaa atakuwa anauza nani? wewe au member ndio watakuwa wanaweka bidhaa zao kama ebay
2. Unaposema budget ndogo ni sh ngapi? ili mtu aweze kukusaidia kimawazo utangaze katika njia ambayo inaendana na budget yako
Asante kaka kwa ushauri wako
kwa kunisaidia hili kulenga kwenye majiji nimepata kitu
mimi napenda iwe kama ebay au alibaba
nimesema na bajeti ndogo sababu nimeona njia wanazotumia wenzangu kufanya promotion ni tv station sijui gharama za kutangaza kwenye tv

ila radio na social media naweza nikafanya promotion japo sijui kama itakuwa inaweza niletea impact kubwa kuwa brand nianze kuwatoza wanaoweka bidhaa au nipate wadhamini
 
Guud idea. Ila hapo kuna changamoto sana. Wew unamkutanisha buyer na seller. Je unaweza vipi ku track transactions. Na utajuaje kama mteja na muuzaj wamfanya biashara. Maana naona ww utakuwa unapokea claims za wateja ambao hujafanya nao transactions.
 
Wazo hili ninalo tangu september,2017.
na nakaribia kulitekeleza, sasa isiwe tupo mkoa mmoja.
 
Wazo hili ninalo tangu september,2017.
na nakaribia kulitekeleza, sasa isiwe tupo mkoa mmoja.
 
Back
Top Bottom