Na mwezi huu uhutubie taifa tena, tumepata Medali

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,498
86,012
Juzi nimefurahi na kusikitika, hii ni baada ya TBC1 kutangaza kuwa mara baada ya taarifa ya habari Rais atahutubia taifa kufuatana na utaratibu wake wa "kuhutubia Taifa kila mwezi". Nilianza kushtuka kusikia neno hilo "kuhutubia Taifa kila mwezi" maana ni miezi kadhaa imepita sijamsikia. Taarifa ikaisha hakuna lolote hadi mida ya saa nne au tano hii kucheki ndio nakuta anahutubia.

Japokuwa hotuba yake haikuwa na jipya wala mvuto ila nilishangazwa na mambo kadhaa, moja; kwanini ahutubie Taifa muda huu ambapo tulikua tunaingia kwenye uchaguzi wa Igunga? pili, Ni suala la raisi kututangazia taifa zima kuwa kaenda kupokea medali ambayo ni heshima kwa Taifa. Hapa napo sikumwelewa kabisa raisi huyu.

Kwa Ufupi alipaswa kuzungumzia hali halisi ya nchi kiuchumi na kubwa suala la umeme, mfumuko wa bei, udini alioupalilia na mkakati gani kuhusu vijana wetu waliokosa mikopo huku wachache wakifaidi mikopo hio, lakini pia angetoa sababu za kueleweka kuhusu kucheleweshwa kwa salary za watumishi wake wa umma, tupo katika kipindi kigumu cha maisha so kutuambia suala la medali HAISAIDII hata kidogo maana kama ni medali tumezikosa kwenye michezo ambayo ndio ingekua sahihi kuzipata huko hizi za kisiasa ni upotevu wa muda na kuleweshwa madaraka ya kisiasa.

Swali langu ni hili; Je mwezi huu utahutubia tena? Kama ni kweli utaratibu wako wa "kuhutubia Taifa kila mwezi" basi uje na hoja zenye mashiko na maana kwa mustakabali wa taifa na sio usubiri hadi kuwe na events fulani fulani ili upate nafasi ya kuwatisha wananchi waichague CCM yako.
 
Sasa unataka ahutubie pale anapokuwa hana la kuongea? Kama kuna mafanikio unataka asiyasemee ili wengine tujueje? Hivi nyie mtakosoa hata maumbile ya kibinadamu kama vile kwenda haja!
 
Sasa unataka ahutubie pale anapokuwa hana la kuongea? Kama kuna mafanikio unataka asiyasemee ili wengine tujueje? Hivi nyie mtakosoa hata maumbile ya kibinadamu kama vile kwenda haja!

mafanikio?????????.............mafanikio gani hayo?
 
mkuu pole sana kwa kungoja hiyo risala! ukiiweka kwenye mlinganyo na hotuba haingii kabisa.
hiyo medal imesaidia nini katika suala zima la kuporomka kwa shilingi, kupanda kwa bei ya mafuta, tatizo la mgao wa umeme??????
jinga kabisa hii mutu!
 
hotuba ijayo atahutubia jinsi ccm ilivyopata ushindi wa kishindi huko igunga!! kwa sababu huwa hana la kuongea atleast atakuwa amepata la kuzungumzia. bullshit yan ananiboa huyu rais ****** anjua kucheza bao na kubadilisha wanawake! shenzi kabisa.......#$%&&()
 
Huwezi kaa mwezi mzima kama raisi ukakosa la kuongea, just a single day mambo mangapi yanatokea hapa nchini na yanahitaji mwongozo wa rais?? Alienda marekani akaomba neti wakampa, alafu wakampa tuzo kutokana na net walizompa, maana yake nini katika dulu za kisiasa!wenye uelewe mkubwa ndo watajua hila chafu na mbinu mbovu za hawa watu, na kama huna akili utapewa uenyekiti mikutano yote hata kama haikuusu make washajua huyu anapenda nini huku kapu lako linabomolewa! naye anacheka NA KUSEMA UKITAKA KULIWA KUBALIWA ULIWE KWELI??SISI TUNA TUMIA NINI KUFIKIRI???
 
Sasa unataka ahutubie pale anapokuwa hana la kuongea? Kama kuna mafanikio unataka asiyasemee ili wengine tujueje? Hivi nyie mtakosoa hata maumbile ya kibinadamu kama vile kwenda haja!

Wewe pamoja na Raisi wako wote ni weupe,mnaongea upupu tu sasa na wewe hapo umepost nini hicho?kilaza kabisa.
 
Huyu mtoto wa kada hivo ule wizi hawa ndo wadau so msimshangae anajua ukilaza wa kilaza!
 
Sina ugomvi na risala yake lakini alikua wapi siku zote? Hotuba ya kujisifia kupewa Medali? zitarudisha umeme? zitaleta sukari? itashusha bei ya mafuta? Je mwezi huu salary zitakuepo kweli? Ndio uongozi huo? Vipi madarasa mangapi yanaandaliwa au kuna mkakati gani kwajili ya watoto waliomaliza std 7 kujiunga na kidato cha kwanza mwakani? Rais? ana washauri au wezi?
 
Back
Top Bottom