Na mgao huu..... Crank box inakufaa

futikamba

JF-Expert Member
Jan 18, 2010
243
13
Wapendwa JF,

Mgao wa umeme hapa nyumbani sasa umerudi. Napenda kuwakumbusha kwamba promotion ya crank box bado ipo valid hadi tar 30.11.2010. Ni Tshs: 15,000/= tu!!

Crank box ni jenereta ndogo ya mkono yenye uwezo wa kuwasha taa 3 za LED.
Haitumii mafuta ya taa, haitumii betri, haitumii umeme wa jua au wa tanesco kuchaji. Teknolojia yake ni rahisi sana! Inatumia Dynamo kutengeneza nishati na kuhifadhi nishati hiyo kwenye capacitor. Ili kuichaji crank box, unazungusha tu kamkono kake kwa dakika moja tu na unaweza kupata mwanga kwa muda usiopungua masaa mawili.
eco_crank_box.jpg
Je unatambua umuhimu wake wakati wa dharura?​

Tunza Mazingira & Jali afya yako - Usiwashe mishumaa, kibatari na chemli.
Sevu Pesa yako - Usinunue betri wala mafuta ya taa kwa kila siku utakayohitaji mwanga wa dharura.

CRANK BOX KWA MWANGA BORA NA WA KUDUMU.
Waranti ya mwaka mmoja.
Kadirio la maisha ni miaka kumi ya matumizi ya kila siku


Tupo Mbezi Beach - Samaki Opposite na Barabara ya kwendea Masana Hospital, Karibu na hoteli ya Gates of Paradise.
Tanzania Home Power Systems.
 
Hakuna za kufua upepo maana mimi bwana bora nilale giza lakini nisilale kwenye joto
 
Hizo taa 3 inazowasha zipo separate au ziko kwenye unit moja?. Maana yangu ni kuwa hiyo crank box ndio taa na generator au ni vitu viwili tofauti?
 
Hizo taa 3 inazowasha zipo separate au ziko kwenye unit moja?. Maana yangu ni kuwa hiyo crank box ndio taa na generator au ni vitu viwili tofauti?

Hizo taa 3 zinakuwa separate, unaweza kuziweka sehemu tofauti kwani package inakuja na vifaa vitakavyokuwazesha ku fix hizo taa include wire and screws.
 
Deal nzuri hii na jinsi tulivyo hoi kwa mgao, haya weka email hapa tuweze kufuatilia. Ina maana biashara yenyewe mpaka Mbezi Beach?
 
Hizo taa 3 zinakuwa separate, unaweza kuziweka sehemu tofauti kwani package inakuja na vifaa vitakavyokuwazesha ku fix hizo taa include wire and screws.
Wakuu nimeelewa kwa nini hawa jamaa wamekuwa kimya hata baada ya watu kuonyesha interest na hii bidhaa, tofauti na alivyobainisha ndugu niliyem-quote hivi vitu vyote vipo katika unit moja. Ni kama kusema torch ya dinamo, ila tu ina taa 3 na unaweza install mahali kwa ajili ya mwanga na usalama.
Unajua ilibidi nifuatilie baada ya kuona kimya kimezidi na hii ingeweza kutupunguzia ukali wa mgao, maana wengine tunaishi eneo ambalo huu tena si mgao ila ni kukosa kabisa umeme. Tango mgao umeanza tunapata wastani wa masaa 3 tu kwa siku, nayo ni kuanzia saa 11 jioni aidha mpaka saa 2 au ikizidi saa 4 usiku.
Sasa baada ya kuona hili tangazo nikaona kama mkombozi vile, hata hivyo bado ni za muhimu nitawatafuta. Kwa wale watakaopenda email yao ni tanhompowersys@gmail.com.
 
Kwa hiyo kila baada ya masaa 2 inabidi uamke kuzungusha kamkono ili iendelee kukupatia umeme? Kuna maeneo wengine tunapenda taa iwake muda mrefu zaidi ya hayo masaa 2.
 
itakuwa ni taa ya kichina tuu
Habari za masiku wakuu!?
Napenda kuwahakikishia kwamba taa hizi si za kichina kabisa. Ni product ya The Nedherlands. Na kuhusu ufanyaji wake wa kazi Naona Shedafa hapo amenisaidia kunyoosha maelezo. Ndio, ni unit moja inayokuja na full installation package.

Promotion imeongezwa wadau. Mwisho ni tar 31.12.2010. Na kwa walio mbali na DSM tupigie simu kupitia 0715 997688 au e-mail: tanhompowersys@gmail.com kwa mawasiliano zaidi.
 
Back
Top Bottom