commited
JF-Expert Member
- Feb 27, 2012
- 1,626
- 870
Ndugu zangu leo 17/09/2012 nilikuwa naangalia taarifa ya habari ya kutoka itv saa 2.00 usiku. Kuna taarifa moja iliyokuwa inaelezea jinsi mbuga yetu ya serengeti ilivyobarikiwa wanyama wengisana (simba 3000, fisi 7500, nyumbu takribani 5000 na nk ambayo ni idadi kubwa sana isiyoweza patikana katika nchi yoyote ile duniani), na pia ikawa inaeleza kuwa katika watalii woote 800,000 wanaoingia nchini kwetu kila mwaka , mbuga hii hutembelewa na watalii wapatao 500,000.
Mjadala wangu uanaanzia hapa, kwa kuangalia sehemu moja tu ya utalii na nikalinganisha na tatizo dogo tu la ukosefu wa madawati katika shule zetu za msingi (zaidi) na sekondari.Nikachulia matharani hao watalii 500,000 tu wa mwaka mmoja kila mmoja alipe kiingilio cha tsh 50,000 tu kuingia mbuga hii ukizidisha hapo utapata (watalii 500,000 x tsh 50,000/= 25,000,000,000/= mapato ya mwaka mmoja tu).
Nikajiuliza hivi gharama ya kutengeneza dawati mmoja tu ni shillingi ngapi, nikasema matharani iwe 50,000/= nikajiuliza tena je kwasasa tuna jumla ya watoto wangapi waliopo shule zetu za misingi nchi nzima nikasema iwe 500,000 (mtanisamehe kama ni takwimu ndogo)kwa hiyo gharama ya kutengeneza madawati 500,000 ya watoto wetu woote wa shule ya msingi itakuwa 500,000/= x 50,000 wanafunzi =25,000,000,000/= (ambayo ni sawa na mapato ya mwaka mmoja tu ya mbuga mmoja tu ya serengeti iliyotembelewa na watalii 500,000).
Je imekuwaje hadi leo tunazaidi ya miaka 50 hata nusu ya tatizo hili hatujalimaza, je ni kweli tunakimbizana kuendelea kama wengine??? kama wenzetu wako dunia ya kwanza na sisi bado tuko dunia ya tatu (tena ni nchi ya 3 kwa kuombaomba baada ya afrighanstan na iraq)
Je ni lini tutafika huko katika listi ya dunia ya kwanza???
Je tunamikakati gani ya kufikia hukokaribuni ndugu zangu kwa majadiliano, mataniwia radhi kwa mahali popote nilipo kosea takwimu, lakini lengo langu ni kuonyesha ni kwa vipi kama tuna fursa kama hii lakini hatuzitumii kutatua matatizo yetu ikiwa tuna kila kitu leo tz ni ya 3 barani africa kwa ku export nje dhahabu, tunakila kitu achilia mbali gesi, na makaa ya mawe na kadhalika.
JK aliwahi kusema hata yeye hajui kwanini tz ni maskini lakini hapa leo muda huu katika kipindi cha dk 45 ITV Mzee malecela anasema chanzo kikubwa cha umaskini wa tz ni ukosefu wa mtaji,,,, karibuni
Mjadala wangu uanaanzia hapa, kwa kuangalia sehemu moja tu ya utalii na nikalinganisha na tatizo dogo tu la ukosefu wa madawati katika shule zetu za msingi (zaidi) na sekondari.Nikachulia matharani hao watalii 500,000 tu wa mwaka mmoja kila mmoja alipe kiingilio cha tsh 50,000 tu kuingia mbuga hii ukizidisha hapo utapata (watalii 500,000 x tsh 50,000/= 25,000,000,000/= mapato ya mwaka mmoja tu).
Nikajiuliza hivi gharama ya kutengeneza dawati mmoja tu ni shillingi ngapi, nikasema matharani iwe 50,000/= nikajiuliza tena je kwasasa tuna jumla ya watoto wangapi waliopo shule zetu za misingi nchi nzima nikasema iwe 500,000 (mtanisamehe kama ni takwimu ndogo)kwa hiyo gharama ya kutengeneza madawati 500,000 ya watoto wetu woote wa shule ya msingi itakuwa 500,000/= x 50,000 wanafunzi =25,000,000,000/= (ambayo ni sawa na mapato ya mwaka mmoja tu ya mbuga mmoja tu ya serengeti iliyotembelewa na watalii 500,000).
Je imekuwaje hadi leo tunazaidi ya miaka 50 hata nusu ya tatizo hili hatujalimaza, je ni kweli tunakimbizana kuendelea kama wengine??? kama wenzetu wako dunia ya kwanza na sisi bado tuko dunia ya tatu (tena ni nchi ya 3 kwa kuombaomba baada ya afrighanstan na iraq)
Je ni lini tutafika huko katika listi ya dunia ya kwanza???
Je tunamikakati gani ya kufikia hukokaribuni ndugu zangu kwa majadiliano, mataniwia radhi kwa mahali popote nilipo kosea takwimu, lakini lengo langu ni kuonyesha ni kwa vipi kama tuna fursa kama hii lakini hatuzitumii kutatua matatizo yetu ikiwa tuna kila kitu leo tz ni ya 3 barani africa kwa ku export nje dhahabu, tunakila kitu achilia mbali gesi, na makaa ya mawe na kadhalika.
JK aliwahi kusema hata yeye hajui kwanini tz ni maskini lakini hapa leo muda huu katika kipindi cha dk 45 ITV Mzee malecela anasema chanzo kikubwa cha umaskini wa tz ni ukosefu wa mtaji,,,, karibuni