Na haya ndio maajabu ya viongozi wetu

mr pipa

JF-Expert Member
Jul 26, 2021
2,299
4,820
Ni vitu gani ambavyo viongozi wetu walifanya nyuma ila pale unapo kumbuka unabaki na mshangao na kujiuliza maswali yasio na majibu

Mimi nakumbuka mwaka fulani nipo kijijini kwetu kulikuwa na tatizo la maji baada ya wananchi kulalamika sana akaja kiongozi mmoja hivi na kusema amesikia kilio cha wananchi na kuwahaidi kutatua tatizo lile linalowasumbua wananchi

Ni kweli baada ya muda wakaja watu wa kuchimba visima pale kijijini hiyo kampuni ikachimba visima kama 16 hivi na mwisho wa siku vile visima vilitoa maji mwezi na hali kulejea kama zaman

Kilicho niacha kwenye mshangao ni kwamba katika hicho hicho kijiji kama kilomita 2 kunachazo kikubwa tu cha maji kwanini wametumia gharama kubwa kuchimba vile visima na pesa kupotea

Asee kila nikikumbuka hili nastaajabika sana

Hebu tueleze kitu gani ambacho kimefanywa na kiongozi wako kinakuacha njia panda

2025 hatutaki mje na ahadi za barabara na mashule tumewachoka miaka sitini yote bado mna ahadi hizo hizo oneni aibu

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
Kumfukuzwa mtu kazi kisa mashine kuleta majibu tofauti mana umeweka kitu kisichojulikana kwenye mashine.
 
Back
Top Bottom