Mzungu Mweusi: Masihi/Mwokozi wa Maskini wa Afrika?

Companero

Platinum Member
Jul 12, 2008
5,605
1,704
Tuliwalaumu sana. Tuliwasema sana. Tuliwakejeli sana.

Tukasema wana kasumba. Tukadai hawakumbuki wanakotoka. Tukasisitiza ni vibaraka.

Lakini leo wanafanya mambo makubwa huko Ulaya na Marikani. Leo hii wanatumika kuleta maendeleo ya Wazungu. Licha ya mafanikio yao yote huko bado huku Afrika hali ni mbaya sana mpaka imebidi tutunge maneno mapya - kama vile Kufulia - ili kuelezea jinsi sisi watu ambao Frantz Fanon alituita 'Les damnes de la Terre', yaani, 'The Wretched of the Earth' au 'Viumbe Waliolaanika Ulimwenguni', tulivyopigika kama hii picha hapo inavyodhihirisha.

58806_tired_woman_tmb.jpg


Je, wakati sasa umefika kukubali hawa Wazungu Weusi watutawale ile tuondokane na ile laana ya Nyani Ngabu ya 'Miafrika Ndivyo Tulivyo'? Je, saa ya wokovu wa Mwafrika imefika kupitia Masihi ambaye ni 'Black Skin White Mask', kama alivyokejeliwa na Frantz Fanon? Je, wakati ni huu wa kuirejea hali inayokejeliwa kizalendo hapo chini na Nabii wetu aliyeshindwa kutufikisha kwenye Nchi ya Ahadi ya 'Egalite' yenye asali na maziwa kwa ajili ya watu wote?

"Some of us, particularly those of us who acquired a European type of education, set ourselves out to prove to our colonial rulers that we had become ‘civilized'; and by that we meant that we had abandoned everything connected with our own past and learnt to imitate only Europeans ways. Our young men's ambition was not to become well educated Africans, but to become Black Europeans! Indeed, at one time it was a complement rather than an insult to call a man who imitated the Europeans a ‘Black European'" - Julius Kambarage a.k.a ex- Black European Julius Cambridge
 
Last edited:
Companero,
Shida ya huyu mzungu mweusi ni kwamba he is self hating. Hana self confidence.
Utawezaje kuwa na vision ya kuwaendeleza wenzako kama wewe mwenyewe hujiamini? Tulikuwa na rais ambaye aliamini kabisa kuwa Watanzania hawawezi. Kaburu tu ndiye anayeweza. Tumeona matokeo ya sera zake. Tusirudi huko.
 
Companero,
Shida ya huyu mzungu mweusi ni kwamba he is self hating. Hana self confidence.
Utawezaje kuwa na vision ya kuwaendeleza wenzako kama wewe mwenyewe hujiamini? Tulikuwa na rais ambaye aliamini kabisa kuwa Watanzania hawawezi. Kaburu tu ndiye anayeweza. Tumeona matokeo ya sera zake. Tusirudi huko.


Jasusi:

Uwa namlaumu babu Nyerere, lakini katika vitu vyote ambavyo namshukuru ni kunipa self confidence.

Watu wanamtukuza kwa kuwapeleka shule bure, lakini self confidence huna, hakuna kitakachofanyika.

Watanzania wanatetemeka kuambiwa East Africa Integration.
 
Companero,
Mkuu hii hadithi ni ndefu sana na hakika inahitaji kurasa nyingi sana kuijadili.
MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO ni mchanganyiko wa mengi sana na hakika wingi wake unatokana na ULIMBUKENI...
Maendeleo ya mtu mweusi yanatokana na kuiga.. Na kibaya zaidi ni kwamba tunakwenda jifunza kuendesha gari wakati uwezo wa kununua hilo gari hatuna. Tunakwenda shule jifunza Uinjinia wakati hata kufua chuma hatuwezi... kwa maana kwamba hata kama tunataka kutengeneza baiskeli basi hicho chuma tunatashindwa kukipata..na kibaya zaidi ni kwamba tumeshindwa kutumia elimu hiyo ktk mazingira yetu, mathlan hatuna chuma au uwezo wa kufua chuma basi tutengeneze hata baiskeli ya mianzi, Hatuwezi..
Mkuu wangu hata Bajaj tunaagiza, gari ambazo zinakwenda kwa kutumia motor tu tumeshindwa kuunda tunaagiza Bajaj toka India...Hizi huko India hutengenezwa mtaani kama mafundi seremala wa pale Keko!..
Na kibaya zaidi tunategemea mabadiliko ya toka kwa viongozi wetu ambao ni MALIMBUKENI kama sisi..sote sisi tunataka kuwa Black European tukifuata nyayo walizopitia wazungu wakati hiustoria ya nchi zetu ni tofauti kabisa. Tumeshindwa kujifunza toka kwao toka utumwa, kutawaliwa hadi ukoloni mamboleo.

Mkuu tuliingizw utumwa kwa sababu sisi (wabantu) ni WAKULIMA hodari.. Na mfano huo bado upo hadi leo hiii.. Huku Canada kuna mashamba ya mvinyo na kazi za misitu. Huko mshikaji watu wanaoonyesha maajabu ni Wabantu.. Kina Yah man (Jamaika)Warundi, Wakongo na Machinga wapo wamejaa tele tena wanaichapa kazi utafikiri hakuna kesho na wanalipwa vizuri sana, lakini njoo nyumbani mkuilima ndiye mtu wa mwisho pamoja na kwamba tunapiga kelele kila siku kwamba Watumwa ndio waliojenga uchumi wa nchi hizo..

Baada ya utumwa mzungu alifanya nini?... alianzisha kilimo ndani ya nchi zetu wenyewe na mazao yetu kusafirishwa nchi zao kwa hiyo hawakuwa haja tena ya kuja fuata watumwa.. tukaletewa mbegu za kila aina toka humu humu Afrika na kwa ujinga wetu hadi leo hii tunaamini Mjarumani ndiye alituletea Mhogo, chakula cheap na rahisi wakati yeye mjarumani hana asili na mhogo..mjarumani hali, wala hatakula mhogo maishani mwake.
Tunashindwa kujiuliza na kuelewa huyo Mjarumani aliutoa wapi mhogo na kwa sababu gani kutuletea sisi wakati akichukua kahawa na Pamba yetu...Ndipo tunaporudi pale pale waliposema wahenga..USIPOFAHAMU UNAKOTOKA HUTAJUA UNAKOKWENDA..

Hivyo mbio zetu zoote hizi hatufahamu tunakwenda wapi.. Na kati ya ULIMBUKENI mkubwa duniani ni huu wa mwafrika kutofahamu anakwenda wapi na kibaya zaidi tunajaribu sana kufikiria njia ya kwenda wakati hatufahamu tulikotoka - tunakumbuka tu mateso na adha zilizotupata.
 
Julius,
Mkuu wala usiogope.. hali hiyo haiwezi kukuta kwa sababu hapo bibie anafikiria mengine kabisaaaaa, hakulala vizuri usiku uliopita!. kwa hiyo msitake kutafsiri picha kwa mtazamo wa magharibi..Njaa ndio imemkuza iweje iwe hoja kwake, tenga limejaa mihogo ana shida gani!..
 
Je, 'Wazungu Weusi' wataweza kutuongoza, kutatawala na kutusimamia ili tuache hizi tabia ambazo zinasemekana ni za 'Miafrika ndivyo ilivyo' na eti ambazo ndizo zinafanya tuwe na maendeleo duni ukilinganisha na 'Wazungu Weupe'?

YANAYO TUFANYA TUWE WASWAHILI...

1.Unamwita mtu usiyemjua(wala kukutana nae kabla) aunt au anco.


2.Asilimia 90 ya CD pamoja na cassete za muziki ulizonazo nyumbani ni feki (sio original copies).


3.Stoo yako imejaa vitu (makorokoro) kwa kuwa hutupi kwa kuamini kuwa ipo siku utayahitaji kwa mfano karpet ukilitoa hulitupi n.k.


4.Una machupa ya maji matupu ya shampoo perfume pamoja na vipodozi vingine umeweka tuu wala huna shughuli navyo.

5.Watoto wako wote wana majina ya utani mfano babu ali,chidi,mamu,dida n.k.

6.Hakuna mtu katika familia yako anayetoa taarifa kwako anapo kuja kukutembelea mfano kaka,shangazi n.k.

7.Mifuko yako imejaa vitu kama vile vijiti vya kusafishia meno,tissue n.k ulivyochukua sehemu kama vile mgahawani.

8.Mama yako ana migogoro na ndugu na hawazungumzi kwa muda wa siku 10 au zaidi.


9.Hupigi simu isipokuwa katika muda ambao gharama za kupiga ni nafuu(mfano usiku sana ) na mara nyingi huwa una beep tu.


10.Ulipokua mdogo nguo unazonunuliwa pamoja na viatu ni vikubwa mara mbili ili uweze kuvivaa muda mrefu zaidi.

11.Wakati ukisafiri na ndege unabeba mzigo wa uzito mkubwa kuliko inavyoruhusiwa.


12.Unapomsaidia mtu na akafanikiwa basi utakuwa unasema kama sio mimi asingekuwa vile yule.
 
Je, 'Wazungu Weusi' wataweza kutuongoza, kutatawala na kutusimamia ili tuache hizi tabia ambazo zinasemekana ni za 'Miafrika ndivyo ilivyo' na eti ambazo ndizo zinafanya tuwe na maendeleo duni ukilinganisha na 'Wazungu Weupe'?

YANAYO TUFANYA TUWE WASWAHILI...

1.Unamwita mtu usiyemjua(wala kukutana nae kabla) aunt au anco.

2.Asilimia 90 ya CD pamoja na cassete za muziki ulizonazo nyumbani ni feki (sio original copies).

3.Stoo yako imejaa vitu (makorokoro) kwa kuwa hutupi kwa kuamini kuwa ipo siku utayahitaji kwa mfano karpet ukilitoa hulitupi n.k.

4.Una machupa ya maji matupu ya shampoo perfume pamoja na vipodozi vingine umeweka tuu wala huna shughuli navyo.

5.Watoto wako wote wana majina ya utani mfano babu ali,chidi,mamu,dida n.k.

6.Hakuna mtu katika familia yako anayetoa taarifa kwako anapo kuja kukutembelea mfano kaka,shangazi n.k.

7.Mifuko yako imejaa vitu kama vile vijiti vya kusafishia meno,tissue n.k ulivyochukua sehemu kama vile mgahawani.

8.Mama yako ana migogoro na ndugu na hawazungumzi kwa muda wa siku 10 au zaidi.

9.Hupigi simu isipokuwa katika muda ambao gharama za kupiga ni nafuu(mfano usiku sana ) na mara nyingi huwa una beep tu.

10.Ulipokua mdogo nguo unazonunuliwa pamoja na viatu ni vikubwa mara mbili ili uweze kuvivaa muda mrefu zaidi.

11.Wakati ukisafiri na ndege unabeba mzigo wa uzito mkubwa kuliko inavyoruhusiwa.

12.Unapomsaidia mtu na akafanikiwa basi utakuwa unasema kama sio mimi asingekuwa vile yule.

Lakini mkuu wangu hii tabia hata wahindi, wachiina na waspanish wanayo iweje uwe uswahili?..
Labda mimi nikupe tafsiri ya NDIVYO TULIVYO..
 
Wakuu jana nilikuwa naongea na Mzungu mmoja wa Afrika Kusini aliniambia kuwa kuna mambo madogo sana yanayotakiwa kubadilishwa kwenye vichwa vya watu weusi, ambavyo kama ikipatikana formula ya kuvibadilisha kuna uwezekano mkubwa waafrika wakawa na maendelep makubwa sana. Amepinga kuwa weusi hawana akili, ametoa evidence zake kuwa ukiwaweka weusi kufanya kazi na whites wanaperfomr better kuliko hata whites.
Amesema kuna mawili makubwa. La kwanza ni uaminifu, amesema wengi si waaminifu, wadokozi na wezi wakubwa. La pili ambalo anaona ni kubwa zaidi ni kuwa weusi tuna lack togetherness au kujiita sisi. Sikuelewa sana pointi yake lakini alikuwa anazungumzia sana kitu kama collectiveness, obectiveness na subjectiveness. anasema sisi ni wabinafsi sana ndio maana wazungu 20 wanaweza kuwatawa waafrika 100, lakini waafrika 1000 hawawezi kuwatawala hata wazungu watano.
Nyani Ngabu, hii sijawahi kuisikia vizuri ukiweza naona utufafanulie vizuri lakini nadhani alisema kitu cha kweli kabisa. Hasa nilipokuwa najaribu ku-relate na hali halisi ya hapa Tanzania. Naona mtu yuko radhi auze watanzania wenzake kwa ajili ya visenti kutoka kwa Rostam. Ndio maana Rostam ana easy ride ya kuiendesha serikali na watanzania wote.
 
NDIVYO TULIVYO = LIMBUKENI

Historia
Tuliuzwa kwa shanga wakati wa Utumwa, tukapewa mhogo na mahindi wakachukua kahawa, Pamba na katani, Leo tunapewa elimu na afya wakichukua dhahabu na ardhi yetu -
- Conclusion priorities zetu ndizo hafifu..hivyo tumepoteza kabisa vitu muhimu au niseme zana za ujenzi wa maendeleo.
1. Tumepoteza Uhuru wetu kifupi hatufahamu kwa nini tulipigania Uhuru..kama kuna mtu anaweza kunambia na akakubalika na kijiwe hiki - namkaribisha!

2. Tumepoteza tamaduni zetu, na pasipo sababu ya msingi hakuna anayezitaka tena.
3. Hatukubali makosa, hata kama yapo basi kuna mkono wa mtu (mchawi).

4. Hatuna imani baina yetu, na ukiweka imani utapigwa changa la macho.
5. Tunasoma ili kuajiriwa na sii kutoa ajira...malengo hafifu.
6. Hatuna common goal, kila jumuiya ya Watanzania ni lazima haikubaliki na wote.
7. Maradhi, Umaskini na Ujinga ni maswala ya Aibu..hayafai kujadiliwa isipokuwa dini, Ukabila, rangi na ubaguzi mwingine ndio umepewa nafasi kubwa ya maisha yetu.
8. na kubwa zaidi ya yote.. UNAFIKI!
 
Njaa ni hoja kwa sababu haizoeleki! Raha inazoeleka lakini njaa...mmmhhh....hapana bana.
Usiseme hivyo mwenzako nimepiga mwezi mzima wa Ramadhani na bado naongezea sita! ukiwa ktk swaumu unaweza sana kufikiri na IQ inapanda utashangaa..trust me!
Penye nia kuna njia maanake wenzetu wamejifunza mengi kutokana na shida...
 
Usiseme hivyo mwenzako nimepiga mwezi mzima wa Ramadhani na bado naongezea sita!
Penye nia kuna njia maanake wenzetu wamejifunza mengi kutokana na shida...

Hebu acha hizo Bob. Wewe mwezi mzima ulikuwa unafuturu na ulikuwa inashindilia kisawasawa. Na hiyo ilikuwa mwezi tu. Kwa wenzako hiyo ni daily occurence.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom