Lilemekisande
Member
- Apr 14, 2012
- 5
- 0
Ndugu zangu wana jamii,mimi ni Mtanzania ambaye nasikitishwa sana habari ya kila siku kwa Watanzania kunyanyasika katika nchi yetu,Habari hii ni kutoka Mirerani Mkoa wa Manyara Wilaya ya Simanjiro katika kijiji cha Naisinyai ambako ndipo ilipo kampuni ya uchimbaji madini ya Tanzanite iitwayo Tanzanite One Mining LTD.Kuna mzungu mmoja ni mwajiliwa wa kampuni hiyo aitwae Collin mnamo mwaka kati ya 2003 mpaka 2005 aliwahi kumpiga risasi kijana mmoja na kumuua kisa eti alikuwa andandia gari lililokuwa limebeba udongo uliotoka mgodini,kesi hii ilizungushwa zungushwa tu na huyo mzungu akakimbilia kwao South africa,alikaa huko kwa muda na mara tena akarudi na kuendelea na kazi,watu walijiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu,hilo likawa limepita.Ila ajabu nyingine tena amerudia tabia yake ya kupiga watu risasi.Ni kama siku 5 au 7 zimepita amefanya tena tukio hilola kupiga vijana wa huku Mirerani kwa risasi na vijana hao inasemekana waliingia kwenye mgodi wao bila ruhusa basi yeye akachukua jukumu la kuanza kurusha risasi kwa watu hao,sasa mimi swali langu ni kwamba hivi serikali yetu iko kweli kwa ajili ya watanzania au kwa ajili ya wawekezaji wakorofi kama hawa,jamani mimi nimemaliza ila naomba nanyi mtoe mawazo yenu.