Mzumbe University SACCOS ni jipu

Evarm

JF-Expert Member
Aug 30, 2010
1,932
1,398
Habari zenu wakuu,

Tunaomba Viongozi wa Chuo Kikuu Mzumbe wa SACCOS (MU SACCOS) mlipe wafanyakazi wenu waliostaafu na waliohama hapo chuoni. Hiki ni chuo cha viongozi lakini hamna hata Uongozi bora na kujali watu mliofanya nao kazi au waliostaafu kwa kuwalipa hela zao kwa wakati za SACCOS.

Mimi binafsi nina zaidi ya miezi kadhaa sijalipwa wala kurudishiwa hela zangu ninazodai hapo SACCOS, nimekuwa nikizungushwa sana kulipwa hela zangu na hao viongozi wa MU SACCOS, mnachokifanya sio sawa kabisa.

Nilifuata taratibu zenu zote kwa kuandika barua kwenye uongozi huo, lakini kila ukiwapigia simu viongozi wa MU SACCOS wanasema hawana hela na hawajui watalipa lini. Hakika hii inatuvunja sana moyo na hata kuleta chuki juu yenu.

Tunaomba wafanyakazi wa Chuo Kikuu Mzumbe muwafikishie ujumbe wenzenu wote hapo. Nafahamu mpo humu wengi tu.

Wenu,

Evarm
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom