Mzozo wa Yanga SC na ENDA Tour: Yanga yatakiwa kulipa milioni 200 au kupelekwa FIFA

ngulukizi

JF-Expert Member
Oct 10, 2018
510
1,431
Yanga SC imeingia katika mzozo na Kampuni ya uwakala wa mechi inayojulikana kama ENDA TOUR ambayo inatambulika na FIFA, kwa KUKIUKA MAKUBALIANO ya kimkataba.

Yanga inasemekana waliingia mkataba na Kampuni hiyo ili iandaliwe kambi ya mazoezi na mechi wakati huu wa maandalizi ya msimu (Pre-season).

Kambi ilipangwa kuwa nchini UTURUKI kwenye Jimbo la Kocael kitongoji cha Kartepe kwenye Hotel ya GREEN PARK, na mtu waliekuwa wanawasiliana nae anaitwa ABDULFATAH FAD.

Kambi ilikuwa ianze tarehe 15/7 /2022 mpaka taerehe 4/8/2022 ikichukua watu 50 wa Yanga ambao ni pamoja na wachezaji, benchi la ufundi na viongozi.

Kwa mujibu wa mkataba kama Yanga wangeamua kuachana na kambi hiyo siku 10 kabla ya tarehe 15/7/2022 wangelazinika kulipa 20% ya malipo yote waliyokubalina ya Dola za Marekani 87,000/ ($87,000) ambayo ni zaidi ya 200,000,000/=

Lakini kama wakiamua kughairisha ndani ya siku 9 kabla ya tarehe 15/7/2022 wanalazimika kulipa 100% ya dola 87,000/=

Yanga kupitia kwa CEO wao SENZO MBATHA wameandika barua pepe leo tarehe 14/7/2022 wakieleza kugahirisha kambi hiyo ya Uturuki.

Sababu ikiwa ni ratiba ngumu waliyopokea kutoka Bodi ya Ligi. Akaomba msamaha kwa usumbufu utakaojitokeza.

Senzo alijibiwa kwa kuulizwa kwanini anaghairishaje safari leo ilihali timu nyingine waliyoingia nayo mkataba inakuja kesho, tarehe 15/7.

Pia anakumbuka kwamba wana mkataba ambao unasema ukighairisha kambi zikiwa zimebaki siku 9 kabla ya siku unayotakiwa kuwa kambini unapaswa kulipia 100% ya malipo na kuamliwa KULIPA hiyo pesa ndani ya wiki hii.

Taarifa zinasema ENDA TOUR wanajiandaa kuleta malalamiko TFF kabla ya kwenda FIFA kama ilivyo ada.

BIN KAZUMARI (The voice of the voiceless)C/P
 
Yanga SC imeingia katika mzozo na Kampuni ya uwakala wa mechi inayojulikana kama ENDA TOUR ambayo inatambulika na FIFA, kwa KUKIUKA MAKUBALIANO ya kimkataba
Mimi nikafikiri labda yanga imeshindwa kulipa hizo gharama kumbe ni hekaya za abunwasi tu zinaendelea hapa, M.200 ni kitu gani kwa mfano mbele ya GSM?

Mkataba Kama ulikuwepo utafuatwa kwa mujibu wa sheria za mikataba kwaiyo sioni cha ajabu hapo, Kama yanga ingegoma kulipa ndo ingekuwa shida sasa sijaona mahala ambapo iyo statiment imesema yanga kagoma kulipa
 
Mimi nikafikiri labda yanga imeshindwa kulipa hizo gharama kumbe ni hekaya za abunwasi tu zinaendelea hapa, M.200 ni kitu gani kwa mfano mbele ya GSM? Mkataba Kama ulikuwepo utafuatwa kwa mujibu wa sheria za mikataba kwaiyo sioni cha ajabu hapo, Kama yanga ingegoma kulipa ndo ingekuwa shida sasa sijaona mahala ambapo iyo statiment imesema yanga kagoma kulipa
Mkataba ili kufutwa
Pande zote mbili lazima zikubaliane
( Mutual agreement)

Kama hili ni la kweli ndani ya klabu kuna watu wanaihujumu kwa njia moja au nyingine lazima kwenye kila jambo kuwepo na foreseen event
Ilikupunguza gharama zisizo na ulazima
 
Jemedari Said sijui ana nini na Yanga! Ndiyo huyu huyu kwa chuki zake binafsi alisababisha Metacha Mnata kuachwa na Yanga msimu uliopita, baada ya kumjaza upepo na hivyo kumtoa mchezoni!

Ana nini huyu jamaa na timu ya wananchi?
Lakini swala la kuahirishwa kwa pre-season yenu Turkey ni la ukweli au uongo? Sasa wewe badala ya kujadili alichoreport Jemedari, wewe unaanza kum-attack personally.

 
Ismail Aden Rage alikuwa sahihi kuhusu Umbumbumbu wa hawa makolo

Jambo wala hali make sense hata kidogo
 
Ila kuna uongo mwingine hata kama sijasoma sheria huwezi nidanganya tangu lini mambo ya timu kuweka kambi yakapekwa FIFA.

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Ni bora umekiri mwenyewe kuwa hujui chochote kuhusu sheria kabla haujaropoka hilo swali, shughuli zote za kimpira kati level inayotambulika na mamlaka husika basi zitakuwa chini ya guidelines za FIFA.
 
Back
Top Bottom