Waridi
JF-Expert Member
- Mar 30, 2008
- 1,025
- 171
Ndugu zangu watanzania,
Nchi yetu inakabiliwa na matatizo mengi kwa sasa kiasi kwamba inayumba sana na tusipoangalia itaanguka milele na haitapata kusimama tena.
Kama kuna mtu wa kuiokoa nchi yetu dhidi ya hatari hiyo,basi si mwingine bali sisi watanzania wenyewe. Huu ni wajibu mzito unaotukabili,ingekuwa heri basi tusiufanyie mzaha.
Miongoni mwa matatizo makubwa sana yanayotukabili ni hili la UFISADI.Yamkini tumekwisha anza kujaribu kupambana nalo lakini huenda silaha na mbinu tunazotumia kulikabili si muafaka kabisa.
Wataalam wa masuala ya kushughulikia matatizo,hususan matatizo ya kijamii wanapendekeza kwamba ili kuhakikisha kwamba tatizo linashughulikiwa ipasavyo hapana budi kutumia kile wanachokiita PROBLEM TREE ANALYSIS,yaani kulitambua na kulichambua tatizo kwa kuangalia matunda yake,majani yake,matawi yake,shina lake,mizizi yake mbali mbali na hasa mzizi wake mkuu-mzizi wa kati (TAPE ROOT),tena kwa kufika katika ncha ya mwisho kabisa ya huo mzizi mkuu. Naam,ukiisha kubainika huo mzizi mkuu,hakika siku utakapong'olewa,mti mzima utanyauka,si shina wala matawi wala majani yatakayobakia kijani kibichi.
Watanzania wenzangu,tumeujadili sana ufisadi(whatever this word means),yaani ubadhilifu,rushwa,ubinafsi na kujilimbikizia mali visivyo halali.Lakini je,tumekwisha kujiuliza na kutafuta u wapi mzizi mkuu wa dubwana hili,ili tuuchimbue tuondokane nalo?
Yamkini twaweza fikiri kwamba mzizi mkuu hapa ni CCM,well hoja hapo ikijengwa vizuri yawezekana ni kweli na hivyo dawa ya ufisadi ikawa ni kuing'oa CCM madarakani.Swali linalozuka tena hapo ni je, siku CCM iking'oka itakuwa kweli ndio mwisho wa ufisadi? Na kama jibu ni hapana...lets continue digging for the tape root.
Ndugu wananchi, kabla sijaja na nadharia yangu ya ninakodhani huko ndiko mzizi huo mkuu uliko, naomba mjadala...karibuni
Nchi yetu inakabiliwa na matatizo mengi kwa sasa kiasi kwamba inayumba sana na tusipoangalia itaanguka milele na haitapata kusimama tena.
Kama kuna mtu wa kuiokoa nchi yetu dhidi ya hatari hiyo,basi si mwingine bali sisi watanzania wenyewe. Huu ni wajibu mzito unaotukabili,ingekuwa heri basi tusiufanyie mzaha.
Miongoni mwa matatizo makubwa sana yanayotukabili ni hili la UFISADI.Yamkini tumekwisha anza kujaribu kupambana nalo lakini huenda silaha na mbinu tunazotumia kulikabili si muafaka kabisa.
Wataalam wa masuala ya kushughulikia matatizo,hususan matatizo ya kijamii wanapendekeza kwamba ili kuhakikisha kwamba tatizo linashughulikiwa ipasavyo hapana budi kutumia kile wanachokiita PROBLEM TREE ANALYSIS,yaani kulitambua na kulichambua tatizo kwa kuangalia matunda yake,majani yake,matawi yake,shina lake,mizizi yake mbali mbali na hasa mzizi wake mkuu-mzizi wa kati (TAPE ROOT),tena kwa kufika katika ncha ya mwisho kabisa ya huo mzizi mkuu. Naam,ukiisha kubainika huo mzizi mkuu,hakika siku utakapong'olewa,mti mzima utanyauka,si shina wala matawi wala majani yatakayobakia kijani kibichi.
Watanzania wenzangu,tumeujadili sana ufisadi(whatever this word means),yaani ubadhilifu,rushwa,ubinafsi na kujilimbikizia mali visivyo halali.Lakini je,tumekwisha kujiuliza na kutafuta u wapi mzizi mkuu wa dubwana hili,ili tuuchimbue tuondokane nalo?
Yamkini twaweza fikiri kwamba mzizi mkuu hapa ni CCM,well hoja hapo ikijengwa vizuri yawezekana ni kweli na hivyo dawa ya ufisadi ikawa ni kuing'oa CCM madarakani.Swali linalozuka tena hapo ni je, siku CCM iking'oka itakuwa kweli ndio mwisho wa ufisadi? Na kama jibu ni hapana...lets continue digging for the tape root.
Ndugu wananchi, kabla sijaja na nadharia yangu ya ninakodhani huko ndiko mzizi huo mkuu uliko, naomba mjadala...karibuni