Mzindakaya naye ataka serikali imsafishe Mkapa

Mpita Njia

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
6,997
1,163
Yulembunge machacha (enzi zake) wa Kwela, Chrisant Mzindakaya, ameitaka serikali kutoa kauli haraka iwezekanavyo kuhusiana na tuhuma zinazomkabili Benjamin Mkapa.
Amesema leo Bungeni kuwa Mkapa anasakamwa wakati ni mtu si tu mwenye sifa katika anga za kimataifa, bali amelifanyia mambo makubwa taifa hili.
Ameshangazwa na wabunge ambao nao wamejiunga katika orodha ya watu wanaomsema vibaya rais huyo akisema kuwa wanajifedhehesha kwani hata ukumbi wa bunge ambamo wanakaa na kujadili mambo kadha umejengwa kutokana na juhudi za mkapa.
 
what crap! kwa kuwa mkapa kajenga bunge ndo iweje?
mbona watanzania tumezowea sana viongozi wetu kutokufanya wajibu wao mpaka wakifanya sisi tunaona maajabu! kisha kiongozi alofanya jema moja tu anageuka malaika!
aibu kwa mbunge kutoa maneno kama hayo
 
Nilivyomsoma katikati ya mistari, nadhani Mzindakaya anarusha madongo dhidi ya baadhi ya watu serikali kuwa wana njama za kumchafua Mkapa kwa sababu anashangaa ni sehemu gani duniani ambako kiongozi mkuu wa nchi mstaafu anaweza kuchafuliwa kiasi hiki na serikali ikaendelea kukaa kimya?
 
Uyu nae si alipewa mkopo wa bilioni kadhaa alafu BOT wakamdhamini enzi za mkapa au anazani tumesahau?
Sio ukumbi wa bunge tuu ata uwanja wa taifa haijalishi!
 
Nilivyomsoma katikati ya mistari, nadhani Mzindakaya anarusha madongo dhidi ya baadhi ya watu serikali kuwa wana njama za kumchafua Mkapa kwa sababu anashangaa ni sehemu gani duniani ambako kiongozi mkuu wa nchi mstaafu anaweza kuchafuliwa kiasi hiki na serikali ikaendelea kukaa kimya?

Mkapa ana ofisi yake, ana wasaidizi wake wanaolipwa na serikali, ana watumishi n.k yeye mwenyewe ni mwandishi wa habari, ana uwezo wa kusema na anajua lugha... kama yeye mwenyewe hataki kujisafisha kwa kuwa mkweli na muwazi, hakuna serikali yoyote duniani itakayomsafisha.

Mtu unapojichafua usitegemee mtu mwingine akumwagie maji kujisafisha wakati unaona mto!
 
Yulembunge machacha (enzi zake) wa Kwela, Chrisant Mzindakaya, ameitaka serikali kutoa kauli haraka iwezekanavyo kuhusiana na tuhuma zinazomkabili Benjamin Mkapa.
Amesema leo Bungeni kuwa Mkapa anasakamwa wakati ni mtu si tu mwenye sifa katika anga za kimataifa, bali amelifanyia mambo makubwa taifa hili.
Ameshangazwa na wabunge ambao nao wamejiunga katika orodha ya watu wanaomsema vibaya rais huyo akisema kuwa wanajifedhehesha kwani hata ukumbi wa bunge ambamo wanakaa na kujadili mambo kadha umejengwa kutokana na juhudi za mkapa.

Credibility ya Mzindakaya iko kwenye vumbi .... yeye aendelee kula fedha alizokopa kizengwe huku akihesabu siku zake za kuwa huru kabla ya kufikishwa kwenye vyombo vya sheria
 
Yulembunge machacha (enzi zake) wa Kwela, Chrisant Mzindakaya, ameitaka serikali kutoa kauli haraka iwezekanavyo kuhusiana na tuhuma zinazomkabili Benjamin Mkapa.
Amesema leo Bungeni kuwa Mkapa anasakamwa wakati ni mtu si tu mwenye sifa katika anga za kimataifa, bali amelifanyia mambo makubwa taifa hili.
Ameshangazwa na wabunge ambao nao wamejiunga katika orodha ya watu wanaomsema vibaya rais huyo akisema kuwa wanajifedhehesha kwani hata ukumbi wa bunge ambamo wanakaa na kujadili mambo kadha umejengwa kutokana na juhudi za mkapa.


Kwa hiyo ukijenga bunge tena kwa pesa za Watanzania walipa kodi hata ukifanya ufisadi basi wewe umezewe tu!!! Mzindakaya ni fisadi mwingine aliyefilisika kimawazo.
 
Yule Mzee mimi personal kanichefua mno.
Alikua anaongea kama anawaambia watoto wake nyumbani kwake,watoto amabo hawajuu what is right or wrong.
Anapaswa yeye na hao waliomtuma kusema maneneo yale wajue kwamba Tumebadilika(watanzania) sio wale wa enzi zile wakipindi kile chake Ignorant, illiteracy and most of all fearfully.
Mzee not any mor...........,ile system yenu tunai-crash haina nafasi tena wakati huu.Mwizi/Wezi tunawajua na wachapakazi tuna wajua.
Just a little quastion for you Mzee Mzindakaya...........Hivi Mugabe amekuaje...?anajari kweli maswahi ya watu wake na taifa lake.......?
Si ndio yeye aliye jienga misingi ya Rhodesea (Zimbabwe) kutoka kwa wakoloni...Itakuja kua Mkapa,....?ambaye amekuta nchii hii safi.

Please Mzee wangu...bora ustahafu kwa heshima au else your down fall will be very bad bora atleast you remain with that little diginity you still have.

Just a thought this for my fellow JF members dont you think its time kwa wabunge wetu wewe wanaangaliwa miaka ya kustahafu.....maana imeandikwa kwenye vitabu vya dini umri ukiwa mkubwa binadamu ana kua kama mtoto?
 
Eti Nani???
Mzindakaya?
Huyu lazima ajikombe kwa waliomkopesha/kumpa mabilioni bila sababu. Hapo alipo kama atang'ang'aniwa kulipa deni la kiwanda chake cha nyama, ni sawa na hukumu ya maisha yake maana hicho kiwanda! Looo! sidhani kama kilifanyiwa uchambuzi kabla ya kuanzishwa.

It is a total loss. Kiwanda kikubwa hakuna kazi yoyote. Alizoea kupewa madaraka sasa anajifunza biashara kwa hali ngumu sana!

Eti anapanda magari yanayosafirisha nyama kwenda nje ya nchi ili asiibiwe!!
Heee! :)
 
Jamani tuwe macho. Makundi yote ya mafisadi sasa wamejiunga na kukabiliana nasi. HII NI VITA tusichukulie mzaaha. It is serious. Tusijikute wanatugawa na kutuchanganya. Angalieni sana. Kuna kesi kama tano zinatarajiwa kufikishwa mahakamani na zote hakuna hata moja ambayo haimgusi Mkapa na ndio maana wanataka Hosea aondoke kabla hajazifikisha hizo kesi mahakamani, maana wameshaandaa mtu wao. Pamoja na matatizo yake ya Richmond, Hosea sasa anachapa kazi kwa maelekezo ya JK na kwamba hakuna atakayepona. Mramba, Yona, Chenge, etc. Nyingine kwa kuwa hazijawa public tusubiri
 
mzee wetu mzindakaya: "zamani kusingalipo elimu, mvi zilihesabika kama busara, sasa elimu ingalipo kamwe mvi si kigezo cha busara tena.....shaban robert
 
Jamami jengo la Bunge limejengwa na pension funds nne (NSSF, PPF, PSPF na LAPF) through a joint company called Pension Properties Ltd. Hawa jamaa wamefinance hiyo project kwa 100% ingawa kwa bond ya serikali (14% bond nadhani). Na serikali (serikali hii) nadhani imeshaanza kulipa hiyo bond. Sasa huyu mzee anapokuja na kumsafisha mkapa na hoja dhaifu kulikoni!!!!!!!! Nakumbuka mkapa alienda kufungua biashara ya Mzindakaya (Machinjioya Kisasa) huko sumbawanga na akamsifu sanaa huyu mzimdakaya. Pia ni huyuhuyu mzindakaya alimtetea sana Balali na BoT mwaka jana tu. Huyu bwana baada ya kuchafuka katika ufisadi hana ujasiri tena! Naye ni fisadi. Apuuzwe!
 
Yulembunge machacha (enzi zake) wa Kwela, Chrisant Mzindakaya, ameitaka serikali kutoa kauli haraka iwezekanavyo kuhusiana na tuhuma zinazomkabili Benjamin Mkapa.
Amesema leo Bungeni kuwa Mkapa anasakamwa wakati ni mtu si tu mwenye sifa katika anga za kimataifa, bali amelifanyia mambo makubwa taifa hili.
Ameshangazwa na wabunge ambao nao wamejiunga katika orodha ya watu wanaomsema vibaya rais huyo akisema kuwa wanajifedhehesha kwani hata ukumbi wa bunge ambamo wanakaa na kujadili mambo kadha umejengwa kutokana na juhudi za mkapa.

Huyu naye kaishiwa baada ya kuchota mapesa BOT na kujenga kiwanda cha nyama kule Sumbawanga,akajiroga kabisa.
Mkapa alipata hela wapi za kujenga ukumbi wa bunge?Hizo ni pesa za mifuko ya jamii ambayo ni mali ya wananchi
 
Unajua mzindakaya naye anatafuta sehemu ya kujisafisha kama sio kuficha madhambi yeye naye ameshiriki kuyatenda. Haiwezekani watu wachache wakawa juu ya sheria kiasi hiki...nafikiri katika dunia ni TZ pekee ambapo watuhumiwa wakubwa tu ndo hupata nafasi ya kuishi vizuri eti waachwe kwani mchango wao ni mkubwa katika nchi. Ukiangalia falsafa ambayo tunaijenga ni 'iba ipasavyo kisha utapata maisha bora iba kidogo segerea huikwepi'. Hivi hawa watu say polisi, PCCB etc wanastahili kuwepo? Je hakuna haja kweli ya kubadilisha katiba yetu na kuwapa nafasi kwa hizi dola kutekeleza majukumu yao kwa uhuru kabisa?
 
Yulembunge machacha (enzi zake) wa Kwela, Chrisant Mzindakaya, ameitaka serikali kutoa kauli haraka iwezekanavyo kuhusiana na tuhuma zinazomkabili Benjamin Mkapa.
Amesema leo Bungeni kuwa Mkapa anasakamwa wakati ni mtu si tu mwenye sifa katika anga za kimataifa, bali amelifanyia mambo makubwa taifa hili.
Ameshangazwa na wabunge ambao nao wamejiunga katika orodha ya watu wanaomsema vibaya rais huyo akisema kuwa wanajifedhehesha kwani hata ukumbi wa bunge ambamo wanakaa na kujadili mambo kadha umejengwa kutokana na juhudi za mkapa.


Kweli mfa maji hakosi kutapatapa. Hata watapetape vipi moto lazima uwawakie.
 
Kweli hii ni hasara kabisa!

Mzindakaya na wegine...hawana kina chochote cha uhalisia. Hili ni tatizo kubwa. hawana miguu ya kusimamia pekee yao. Ni wasaliti ambao siku zao zinahesabika.

Bunge limekuwa genge la leo kukubali hiki..na kesho kukukiruka...simply wanaanagalia upepo...

..Muda huohuo alipokuwa anaongea huo upupu...alimrushia kijembe Mwakyembe...Eti atulie...kwani kamati ya RD sio yake na niya bunge...so hawezi kuja na kuisemea ...etc
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom