Mzindakaya: Mbunge wa muda mrefu CV yake hii hapa

Mbunge wa Kwela, Dk Chrisant Mzindakaya amewashambulia wanaowatuhumu wenzao kuwa ni mafisadi kwa kusema kuwa nao ni mafisadi na wana roho mbaya.

Mbunge huyo pia amewatuhumu wanaomlaumu Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa kuwa wana roho za kishetani.

Mzindakaya amesema bungeni leo kuwa, wanaosema wenzao ni mafisadi wana roho za kifisadi na amehoji kwa nini wawaandame wenzao. “Na kwa nini wewe umezaliwa kuandama wenzako tu?” amehoji Mzindakaya wakati anachangia hoja ya bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2009/2010.

Amesema, watu hao wana roho mbaya, na wanajifanya wazuri kwa kuwa hawana moyo wa kuthubutu. “Binadamu ana kasoro moja, ukifanya mema kumi, ukakosea moja atafuta yote” amesema mbunge huyo katika kikao cha 11 cha mkutano wa 16 wa Bunge unaoendelea mjini Dodoma.
 
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alizaliwa Desemba 31, 1940. Kati ya mwaka 1960-1961 alijiunga Sekondari ya Bugerere nchini Uganda na kupata elimu ya sekondari; mwaka 1964-1965 alikuwa Afisa Maendeleo Msaidizi Wilaya ya Sumbawanga na mwaka 1963-1964 alijiunga Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru, Arusha


Hii CV haiko sawa Tarehe zinagongana
 
Jamani wana JF, mnashangaa nini wakati kila mwanasiasa sasa hivi anajiita DR? Kama Dr. Kingunge..., nk
 
sasa huo udaktari ni wa nini (wanyama, watu, falsafa, honoraria, au ni wakina [Maji marefu na Matunge]?). Manake sijaona kwenye andishi lako mahali alipotaja kupata chati cha huo udaktari!

Kuhusu maendelea yaliyotokea akiwa kiongozi ni machache mno. Shule 17 tu katika jimbo! Inanikumbusha miaka ya 90 ambapo K'njaro ilikuwa na sekondari karibia 100 ndani ya majimbo 6, sijui leo zitakuwa ngapi, manake kata nyingine zina shule hadi 6. Kiwango cha vijana wanaochaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari ni kidogo sana (27%) wakati mpango ni kuwa na zaidi ya 50% kwenda sekondary. Mwendo huu unaonyesha kuwa wananchi kwenye jimbo hili wameandaliwa kuendelea kuwa wakulima wadogo wadogo tu!

Ametaja barabara zilizojengwa, ila hakusema ni kwa kiwango gani, kwani hata wanavijiji hufanyia matengenezo barabara zao, lakini hazipitiki kwa muda wote!

Sijaona alipozungumzia suala la afya, maji, makazi ndani ya jimbo lake. Hivi ni viashiria vya maendeleo! Watu wanaweza kuwa wanavuna lakini wanaendelea kulala kwenye vibanda vya nyasi, kunywa kangara na kimpumu na kusubiri msimu mwingine wa kilimo ufike.
Miaka ya zamani kulikuwa na kozi zilikuwa zinatolewa na Eastern Block ikiongozwa na USSR zilizokuwa hata za miezi sita katika nyanja za propaganga, espionage na mambo ya siasa ambazo wengi wa wahitimu walipomaliza walijiita madokta. Lakini nahisi sio madokta wale wa kusoma kutibu au wa level ya Phd. Ni madokta wa mambo mambo kama wanayoyafanya
 
Miaka ya zamani kulikuwa na kozi zilikuwa zinatolewa na Eastern Block ikiongozwa na USSR zilizokuwa hata za miezi sita katika nyanja za propaganga, espionage na mambo ya siasa ambazo wengi wa wahitimu walipomaliza walijiita madokta. Lakini nahisi sio madokta wale wa kusoma kutibu au wa level ya Phd. Ni madokta wa mambo mambo kama wanayoyafanya

Jamani, huyu ba'mkwe anatoka ktk ukoo wawindaji na alizoeshwa kula nyama sasa kipindi ile amepelekwa uganda kusoma middle school alishindwa kuvumilia walau hata kumaliza mhula wa kwanza kwakuwa maisha ya kula matoke hakuzoea na akaamua kutoroka na kurudi nyumbani ufipa.

Basi ndo akawa kondakta wa mabasi (Enzi hizo yalijukana kama SAIDI BUS SERVICES) yalokuwa yakimilikiwa na waarabu yakiwa yakipiga ruti kati ya Ufipa na mji wa mpakani na nchi ya zambia.

Zaidi ya hapo hakuna elimu yeyote ya maana aliyosomea, umaarufu wa kisiasa alipata kwakuwa marehemu babaake alikuwa akiwatibu viongozi wakubwa wa inji hii, na huo ubunge amekuwa akiupata kwa njia mabalimbali za kibabe, mlungula pia akisaidiwa na kuogopwa kwa ndumba. Kwa kifupi jimbo lake liko nyuma sana kimaendeleo!

Huo udaktari alipewa mwanzoni mwa miaka ya 2000 na chuo kimoja cha kidini cha kule marekani tena sherehe ya kutunikiwa aliiandaa yeye mwenyewe pale ufipa na kumgharimia mwakilishi wa chuo hicho usafiri na malazi ili kuwaonesha wanachi wa jimbo lake jinsi gani alivyo msomi, anadai eti wamarekani walimpatia udakatari kwa kuthamini mchango wake wa kuleta maendeleo Tanzania. waalikwa wa graduation hiyo waliongozwa na "kaka yake" bwana John Malecela pamoja na Askofu wa dini moja kubwa...

Suala la kukataliwa Mzumbe ni kweli, kisa ni yeye mwenyewe akiwa mkuu wa mkoa wa Morogoro kwenda chuo cha kilimo Sokoine na kuamuru tena kwa nguvu wampatie matrekta yao walokuwa wakitumia kufundishia ili aende akatimize azma yake ya kilimo kazi huku akiwalimia vigogo mashamba makubwa bure badala ya kuleta maendeleo yalokusudiwa.

Ikumbukwe, baadhi ya wanabodi ya Sokoine walikuwa wakitokea Mzumbe basi mwamba huyu akajisahau na kujaribu kujiunga na shule ili ajiendeleze ndo akakumbana na mkasa huo wa kunyimwa!!! naamini kabisa pamoja na kwamba hakuwa na sifa za kujiunga, wangeweza mkubalia asome lakini alikuwa tayari ameshawauzi waacademia!!!

Nawakilisha.
 
jamani eeh mkoa wa Rukwa ukipaa na ungo unaweza kuwa clarified dr mtake msitake,au mnataka wote muwe vipofu hapa?nijibu moja...mb...........rr
 
Mzindakaya alifukuzwa Mzumbe kwa sababu alifoji, udaktari pia ni forgery. Miaka 44 hakuna cha maana. Sasa amekuwa mtetezi mkubwa wa Mkapa baada ya kupewa bilion 9 za kuanzisha kiwanda cha kusindika nyama Rukwa
mhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh! ndiyo maana siku hizi maana hana sumu tena kama alivyo kuwa zamani...
 
I like Mzindakaya, he knows how to make things happen! Tangu 1965 hadi leo na huenda hata kesho, tunahitaji calibre ya watu kama hawa na wala siyo maneno-maneno.

Haya wasomi wekeni changamoto zenu nanyi hapa mme-achive nini tangu mlipomaliza shule hadi sasa?
 
Je, huyu Bwana Crisant Majiyatanga Mzindakaya hajawahi kuwa Waziri mdogo wa Uchukuzi hapo awali? Pengine hili lilitokea wakati akiwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara:

Mafaili ya TAKUKURU ya wakati huo yana kisa kwamba Bwana Crisant Majiyatanga Mzindakaya alichukua vifaa vya ujenzi wa nyumba yake na kuvisafirisha kwa lori la serikali kutoka Dar mpaka Sumbawanga! Wengine walitia hofu kuwa huenda baadhi ya vifaa hivyo vilikuwa ni mali ya serikali! Nyerere aliyajua hayo na baadaye kamtimua Bwana Crisant Majiyatanga Mzindakaya, mbali ya majambo yake mengine yasiyo ya ki-maadili!
 
I like Mzindakaya, he knows how to make things happen! Tangu 1965 hadi leo na huenda hata kesho, tunahitaji calibre ya watu kama hawa na wala siyo maneno-maneno.

Haya wasomi wekeni changamoto zenu nanyi hapa mme-achive nini tangu mlipomaliza shule hadi sasa?
Ni kweli kuna mambo mengi ameyafanya mazuri na tunahitaji kuwa na watu wengi wa aina yake ndani ya mfumo wa utawala. Mfano alisaidia sana kubadili tabia za waluguru za kucheza ngoma toka juma tatu mpaka jumapili kwa kuwalazimisha kulima mashamba na kupiga marufuku ngoma hizo katikati ya wiki.Nasikia hata Kigoma alijitahidi sana kupigania kilimo. Lakini kinachojadiliwa hapa ni kweli yeye ni Dokta?
 
Je, huyu Bwana Crisant Majiyatanga Mzindakaya hajawahi kuwa Waziri mdogo wa Uchukuzi hapo awali? Pengine hili lilitokea wakati akiwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara:

Mafaili ya TAKUKURU ya wakati huo yana kisa kwamba Bwana Crisant Majiyatanga Mzindakaya alichukua vifaa vya ujenzi wa nyumba yake na kuvisafirisha kwa lori la serikali kutoka Dar mpaka Sumbawanga! Wengine walitia hofu kuwa huenda baadhi ya vifaa hivyo vilikuwa ni mali ya serikali! Nyerere aliyajua hayo na baadaye kamtimua Bwana Crisant Majiyatanga Mzindakaya, mbali ya majambo yake mengine yasiyo ya ki-maadili!
Kumbe........
 
Alizaliwa Desemba 31, 1940. Kati ya mwaka 1960-1961 alijiunga Sekondari ya Bugerere nchini Uganda na kupata elimu ya sekondari; mwaka 1964-1965 alikuwa Afisa Maendeleo Msaidizi Wilaya ya Sumbawanga na mwaka 1963-1964 alijiunga Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru, Arusha ambako alitunukiwa cheti.
Kutokana na 'kiu' ya kupata elimu, Dk Mzindakaya aliwahi kujiunga Chuo cha Maendeleo ya Uongozi Mzumbe (IDM) hivi sasa Chuo Kikuu Mzumbe na kufukuzwa kwamba hakuwa na sifa.
Kama nakumbuka vizuri aliyekuwa mkuu wa baraza la Mzumbe alikuwa Marehemu Amon Nsekela
 
RIP. Chrisant mzindakaya Maji ya Tanga nukumbuka 2010 ulituuliza swali kwamba walio hai na walio kufa wengi wepi.tulipokujibu walio kufa ukasema basi umeshashinda ubunge kwakuwa wafu watakuchagua

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
Mzindakaya alifukuzwa Mzumbe kwa sababu alifoji, udaktari pia ni forgery. Miaka 44 hakuna cha maana. Sasa amekuwa mtetezi mkubwa wa Mkapa baada ya kupewa bilion 9 za kuanzisha kiwanda cha kusindika nyama Rukwa
Na deni hill bado Anadaiwa Kiwanda hakifanyi kazi
 
Back
Top Bottom