Mzimu wa Sombetini wamtafuna Godbless Lema

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,921
31,161
Bwana Godbless Lema ameendelea kuandamwa na kashfa ya kumnadi Diwani wa CCM Sombetini Bwana A Mawazo katika uchaguzi mdogo.Bwana Lema mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Arusha mjini amejikuta akishindwa kutoa majibu ya kuridhisha wapiga kura ni sababu zipi zilimfanya amfanyie kampeni Bwana A Mawazo mwana CCM na kumwacha mgombea udiwani wa CHADEMA,CUF na TLP ?.Ikumbukwe Bwana Mawazo alikuwa diwani wa TLP kabla ya kujiunga na CCM.

Mkutano wa Dr W Slaa Mbauda ulibakia kama karata pekee ya kumwokoa Lema dhidi ya kashfa ya kuuza ubunge mwaka 2005 na kumfanyia kampeni Mawazo lakini bado hakuweza kujitoa kwenye kashfa hizo na hata Dr Slaa ilielekea alikuwa akijua dhambi yake.Alimtaka awe makini kwani anaweza kumtosa ???????.



Wagombea udiwani wa CHADEMA wameonekana kuwa na nguvu zaidi ya mgombea ubunge hasa baada ya mkutano wa Dr W Slaa.Madiwani wa kata za Kimandulu,Elerai na Moshono wameendelea kuvutia wapiga kura wengi kuliko mwanzo,Bwana Lema amekuwa akitegemea kubebwa na madiwani wa kata hizo zaidi tofauti na mwanzo wa kampeni zake madiwani walikuwa wakimtegemea zaidi ili kuwafikia wapiga kura wengi.


CCM inafanya vizuri kata ya Kati ilipo ngome kuu ya Mama batilda,mkutano wake maeneo ya St Thomas Hospital ulivutia watu wengi sana huku mgombea udiwani wa kata ya kati akiwa na uhakika wa kushinda kata hiyo.


TLP inaringia kata ya Sokoni 1,Sombetini,Lemara na Ungalimited.wapiga debe wa TLP wanatumia udhaifu wa Bwana Lema hasa kitendo chake cha kumpigia debe mgombea wa CCM.
 
Bwana Godbless Lema ameendelea kuandamwa na kashfa ya kumnadi Diwani wa CCM Sombetini Bwana A Mawazo katika uchaguzi mdogo.Bwana Lema mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Arusha mjini amejikuta akishindwa kutoa majibu ya kuridhisha wapiga kura ni sababu zipi zilimfanya amfanyie kampeni Bwana A Mawazo mwana CCM na kumwacha mgombea udiwani wa CHADEMA,CUF na TLP ?.Ikumbukwe Bwana Mawazo alikuwa diwani wa TLP kabla ya kujiunga na CCM.

Mkutano wa Dr W Slaa Mbauda ulibakia kama karata pekee ya kumwokoa Lema dhidi ya kashfa ya kuuza ubunge mwaka 2005 na kumfanyia kampeni Mawazo lakini bado hakuweza kujitoa kwenye kashfa hizo na hata Dr Slaa ilielekea alikuwa akijua dhambi yake.Alimtaka awe makini kwani anaweza kumtosa ???????.



Wagombea udiwani wa CHADEMA wameonekana kuwa na nguvu zaidi ya mgombea ubunge hasa baada ya mkutano wa Dr W Slaa.Madiwani wa kata za Kimandulu,Elerai na Moshono wameendelea kuvutia wapiga kura wengi kuliko mwanzo,Bwana Lema amekuwa akitegemea kubebwa na madiwani wa kata hizo zaidi tofauti na mwanzo wa kampeni zake madiwani walikuwa wakimtegemea zaidi ili kuwafikia wapiga kura wengi.


CCM inafanya vizuri kata ya Kati ilipo ngome kuu ya Mama batilda,mkutano wake maeneo ya St Thomas Hospital ulivutia watu wengi sana huku mgombea udiwani wa kata ya kati akiwa na uhakika wa kushinda kata hiyo.


TLP inaringia kata ya Sokoni 1,Sombetini,Lemara na Ungalimited.wapiga debe wa TLP wanatumia udhaifu wa Bwana Lema hasa kitendo chake cha kumpigia debe mgombea wa CCM.

Hao wanaomhoji au kutaka kujadili maamuzi binafsi ya Ndg Godbless Lema wanakiuka Uhuru wake maoni, hayo ndio mawazo mgandfo ya KiCCM tunayoyapiga vita na kutaka mabadiliko. Kama Ndg Godbless anaamini kuwa mgombea wa CCM anafaa yako huru kumfanyi kampeni bila ya kipingamizi chochote. Mfano hai ni 1995, pale Hayati Mwalimu Nyerere alipokuwa anamnadi Mgombea Urais kwa tiketi ya ccm Benjamin Mkapa na alipofika Jimbo la Musoma Mjini na kukuta CCM imempitisha Ndg Emmanuel Mogoti kama mgombea Ubunge. Kwa kuwa alikuwa na tuhuma za kufilisi ushirika, Mwalimu aliishia kumnadi Benjamin Mkapa na katika nafasiu ya ubunge akatangaza hadharani katika mkutano huo kuwa atampigia kura mgombea wa NNCR mageuzi Balozi Paul Ndobo badala ya mgombea wa CCM.

Matokeo yake wananchi wa jimbo hilo wakamchagua mgombea wa NCCR Mageuzi katika jimbo hilo.

Hivyo hakuna ubaya wowote mtu wa chama kimoja kumpigia debe wa chama kingine. Tuache mawazo mgando ya KiCCM.
 
Hao wanaomhoji au kutaka kujadili maamuzi binafsi ya Ndg Godbless Lema wanakiuka Uhuru wake maoni, hayo ndio mawazo mgandfo ya KiCCM tunayoyapiga vita na kutaka mabadiliko. Kama Ndg Godbless anaamini kuwa mgombea wa CCM anafaa yako huru kumfanyi kampeni bila ya kipingamizi chochote. Mfano hai ni 1995, pale Hayati Mwalimu Nyerere alipokuwa anamnadi Mgombea Urais kwa tiketi ya ccm Benjamin Mkapa na alipofika Jimbo la Musoma Mjini na kukuta CCM imempitisha Ndg Emmanuel Mogoti kama mgombea Ubunge. Kwa kuwa alikuwa na tuhuma za kufilisi ushirika, Mwalimu aliishia kumnadi Benjamin Mkapa na katika nafasiu ya ubunge akatangaza hadharani katika mkutano huo kuwa atampigia kura mgombea wa NNCR mageuzi Balozi Paul Ndobo badala ya mgombea wa CCM.

Matokeo yake wananchi wa jimbo hilo wakamchagua mgombea wa NCCR Mageuzi katika jimbo hilo.

Hivyo hakuna ubaya wowote mtu wa chama kimoja kumpigia debe wa chama kingine. Tuache mawazo mgando ya KiCCM.

Heshima kwako jatropha,

Ni kweli Mwl Nyerere alimpigia kura Balozi Paul ndobo wa NCCR Magezi na kumwacha mwanaCCM mwenzake Emanuel Magoti.Pengine Rais J Kikwete alitakiwa ajifunze hili wakati alipoenda Rombo angejinadi mwenyewe na ikiwezeka ampigie debe mgombea safi bila kujali chama watu wenye akili nzuri tungemwelewa.

Nirejee kwa Bwana Godbless Lema hakuwa na sababu za kufanya hivyo inajulikana Bwana Mawazo alijitoa TLP kwasababu za rushwa ya nyumba,gari na fedha.Sababu pekee anayoitoa Bwana Lema ni urafiki !!!!!!.
 
heshima kwako jatropha,

ni kweli mwl nyerere alimpigia kura balozi paul ndobo wa nccr magezi na kumwacha mwanaccm mwenzake emanuel magoti.pengine rais j kikwete alitakiwa ajifunze hili wakati alipoenda rombo angejinadi mwenyewe na ikiwezeka ampigie debe mgombea safi bila kujali chama watu wenye akili nzuri tungemwelewa.

nirejee kwa bwana godbless lema hakuwa na sababu za kufanya hivyo inajulikana bwana mawazo alijitoa tlp kwasababu za rushwa ya nyumba,gari na fedha.sababu pekee anayoitoa bwana lema ni urafiki !!!!!!.

lakini ukumbuke kuwa hizo nituhuma tu na hazijathibitishwa. Ni vyema kama tuhuma hizi zina ukweli wowote ndg godbless lema aulizwe maswali kuhsinana tuhuma hizo katika mikutano yake ya kampeni.
 
Mkuu Ngongo, nimefuatilia kidogo unavyomwandama huyu Lema wa Chadema na kwa hali ya kawaida sijui lengo lako hasa ni nini. Kwa vyovyote vile hii yako wazungu wanaiita obsession na wanikumbusha mwana JF mwingine anavyomwandama mdogo wetu Regia - wakati mwingine inakuwa vigumu sana kuwaelewa watu wengine.
 
Heshima kwako jatropha,

Ni kweli Mwl Nyerere alimpigia kura Balozi Paul ndobo wa NCCR Magezi na kumwacha mwanaCCM mwenzake Emanuel Magoti.Pengine Rais J Kikwete alitakiwa ajifunze hili wakati alipoenda Rombo angejinadi mwenyewe na ikiwezeka ampigie debe mgombea safi bila kujali chama watu wenye akili nzuri tungemwelewa.

Nirejee kwa Bwana Godbless Lema hakuwa na sababu za kufanya hivyo inajulikana Bwana Mawazo alijitoa TLP kwasababu za rushwa ya nyumba,gari na fedha.Sababu pekee anayoitoa Bwana Lema ni urafiki !!!!!!.
Mimi naona unajaribu kuwapotosha wana JF lakini huwezi kufanikiwa huyo mgombea wa TLP unaempigia kampeni hakubaliki hapa Arusha huko sombetini nakujua si kama unavyosema na watu wengi wanaikubali CHADEMA Kwa ujumla sijui hiyo research ya Lema kuteswa na mzimu wa Sombetini hebu niambie ni sombetini ipi hasa maana naona unachuki binafsi na Lema...Hizo sababu za kumuunga mkono mgombe wa chama CCM alizijibu...Alitoa sababu mbili pamoja nakuomba msamaha naamini ulikuwepo siku ya mkutano ulizisikia ila unajaribu kupotosha ndiyo maana siku hiyo ulikaa kimya hukuongelea chochote.... kuhusu kuuza ubunge alikanusha namini ulimsikia pia....huwezi kuuza ubunge kwa mil 30 sawa na mshahara wa miezi mitatu kwa taaarifa yako Lema hata CCM wana mkubali hasa kambi ya Mrema
 
Unajua Mkuu Ngongo inakuwa taabu watu kukuamini kwani tangu mwanzo umeonekana hauko upande wa Lema
 
lakini ukumbuke kuwa hizo nituhuma tu na hazijathibitishwa. Ni vyema kama tuhuma hizi zina ukweli wowote ndg godbless lema aulizwe maswali kuhsinana tuhuma hizo katika mikutano yake ya kampeni.

Heshima kwako Jatropha,

Mkuu wangu Godbless Lema alimfanyia kampeni Aliphonce Mawazo kampeni huko Sombeti mimi mwenyewe nilishuhudia kwa hiyo hizi si tuhuma ni ukweli na utabaki doa kubwa la kisiasa upende usipende.Kwa taarifa yako Godbless Lema kwenye mkutano wake wa kampeni kata ya Sekei jana aliwaomba radhi wananchi waliokuja kumsikiliza unaweza kuuliza vyanzo vingine ili kujiridhisha.nguvu ya CHADEMA sasa ipo kwa wagombea udiwani ambao wanjitahidi kumsafisha kwa wapiga kura.

Godbless Lema asingejiingiza kwenye mitego ya CCM mwaka huu asingekuwa na sababu ya kufanya kampeni kwani alishinda uchaguzi wa mwaka 2005 lakini kwa kutojua tayari alikuwa na mtaji mzuri akakubali kurubuniwa.

Wa JF najua upo ugonjwa wa ajabu hapa jamvini kila wakati tunataka kusoma habari nzuri za CHADEMA ! ikitokea habari mbaya tunatafuta njia za kitoto kukataa ukweli.
 

"Wagombea udiwani wa CHADEMA wameonekana kuwa na nguvu zaidi ya mgombea ubunge hasa baada ya mkutano wa Dr W Slaa.Madiwani wa kata za Kimandulu,Elerai na Moshono wameendelea kuvutia wapiga kura wengi kuliko mwanzo,Bwana Lema amekuwa akitegemea kubebwa na madiwani wa kata hizo zaidi tofauti na mwanzo wa kampeni zake madiwani walikuwa wakimtegemea zaidi ili kuwafikia wapiga kura wengi.
"



Ujumbe huu una migongano..............Inakuwaje Dr. Slaa awabebe madiwani lakini asimbembe Mbunge wakeeeeeeeeeeeee?

Aidha anawabeba wote au la hasha...........Nina wasiwasi taarifa hii yalenga kumpigia debe Dr. batildaaaaaaaaaaaa
 
Mkuu Ngongo, nimefuatilia kidogo unavyomwandama huyu Lema wa Chadema na kwa hali ya kawaida sijui lengo lako hasa ni nini. Kwa vyovyote vile hii yako wazungu wanaiita obsession na wanikumbusha mwana JF mwingine anavyomwandama mdogo wetu Regia - wakati mwingine inakuwa vigumu sana kuwaelewa watu wengine.

Heshima kwako Mag3,

Mkuu Simwandami Lema kwasababu za kutunga ila nataka ukweli ufahamike mapema najua iko siku mtakuja tafuta rejea hapa JF.Ikiwa Lema atachaguliwa nitafurahi kwasababu namba ya wapinzani itaongezeka lakini simpiganaji wa kweli.Kashindwa kusimamia jambo dogo sana je akiwa mbunge masuala makubwa kama mikataba mibovu ya madini,wizi na matumizi mabaya ya fedha za umma ataweza ??????.
 
Mimi naona unajaribu kuwapotosha wana JF lakini huwezi kufanikiwa huyo mgombea wa TLP unaempigia kampeni hakubaliki hapa Arusha huko sombetini nakujua si kama unavyosema na watu wengi wanaikubali CHADEMA Kwa ujumla sijui hiyo research ya Lema kuteswa na mzimu wa Sombetini hebu niambie ni sombetini ipi hasa maana naona unachuki binafsi na Lema...Hizo sababu za kumuunga mkono mgombe wa chama CCM alizijibu...Alitoa sababu mbili pamoja nakuomba msamaha naamini ulikuwepo siku ya mkutano ulizisikia ila unajaribu kupotosha ndiyo maana siku hiyo ulikaa kimya hukuongelea chochote.... kuhusu kuuza ubunge alikanusha namini ulimsikia pia....huwezi kuuza ubunge kwa mil 30 sawa na mshahara wa miezi mitatu kwa taaarifa yako Lema hata CCM wana mkubali hasa kambi ya Mrema

Heshima kwako Crashwise,

Wakaazi wa wengi wa Kata ya Sombetini walishuhudia Lema akimpigia debe mgombea udiwani wa CCM
Bwana Mawazo hawahitaji kuambiwa au kusikia kutoka kwa mtu yoyote walimwona na sasa wanamshangaa.Ni kweli nina chuki kubwa na Lema baada ya kutusaliti wanamageuzi na sasa anakuja kudanganya umma kwamba ni mwanamageuzi wa kweli wakati ukweli unajulikana.Sababu za kumpigia mgombea wa CCM ulizikubali kama ulizikubali tafadhali jitazame upya pengine haya mageuzi tunayojadili umeyadandia tu.
 
Unajua Mkuu Ngongo inakuwa taabu watu kukuamini kwani tangu mwanzo umeonekana hauko upande wa Lema

Heshima kwako Ndege ya Uchumi,

Ni kweli tangu mwanzo sikuwa upande wa Lema.Mwaka 2005 nilikuwa namuunga mkono Lema kwa hali na mali nilishiriki kuchangia kampeni fedha za mafuta,picha na nk.

Mwaka 2010 simuungi mkono Lema kwasababu aliondoa kesi mahakamani bila kumshirikisha mtu yoyote.alitoweka kwa muda baada ya kufuta kesi aliporejea aliulizwa sababu za kuondoa kesi mahakamani hakuwa na majibu alipobanwa zaidi akaishia kuondoka yeye na Mawazo Aliphonce diwani wa TLP Sombetini.Bwana Lema mwaka 2005 alikuwa akimiliki VW bito mbovu baada ya kufuta kesi alianza kupata maendeleo ya haraka haraka [1] Noah mpya new model[2] RVR mpya [3] Baloon[4] Nyumba.Majibu ya utetezi gazeti la mwanahalisi 15/09/20010 anadai hakuwa na tsh 5 milioni za kuendesha kesi sasa jiulize magari na nyumba anayomiliki yana thamani gani ?.Ikiwa tunachukia A Chenge,E Lowassa,Karamagi na B Mramba kutufisadi lakini hatuoni ufisadi wa wanaojita wapiganaji feki hakika Tanzania itaendelea kuogelea kwenye dimbwi la umaskini miaka nenda miaka rudi.


Mkuu NU nimekuwa mshiriki mkubwa wa siasa za upinzani tangu enzi za Makongoro Nyerere,nazijua siasa na wanasiasa.Sifungwi na uanachama wa vyama vya siasa napenda kuangalia sifa ya mtu na si chama.Tulimchagua Makongoro Nyerere kwa kuangalia chama badala ya kutazama sifa ya mtu [tulimweka pembeni Mzee E Mtei].Miaka kumi na tano imepita tangu wana Arusha tufanye kosa ambalo mpaka leo tunaendelea kubeba lawama.Hakika mimi si mmojawapo wa watu wanashabikia chama kwa kuangalia mambo kijuju.

Mkuu NU nimeelekeza nguvu zangu Arumeru Magharibi yupo Bwana Ole Kisambu anagombea kwa mara ya pili mwaka 2005 alimsumbua sana Mollel wa CCM.Namsaidia Ole Kisambu kwasababu ana msimamo madhubuti,ni mwadilifu,hanunuliki wala haongeki.

Nasisitiza tena na tena sifungwi na chama chochote[isipokuwa CCM] naangalia mgombea makini,mwenye elimu nzuri,mwadilifu,mbunifu na mwenyekipaji.
 

"Wagombea udiwani wa CHADEMA wameonekana kuwa na nguvu zaidi ya mgombea ubunge hasa baada ya mkutano wa Dr W Slaa.Madiwani wa kata za Kimandulu,Elerai na Moshono wameendelea kuvutia wapiga kura wengi kuliko mwanzo,Bwana Lema amekuwa akitegemea kubebwa na madiwani wa kata hizo zaidi tofauti na mwanzo wa kampeni zake madiwani walikuwa wakimtegemea zaidi ili kuwafikia wapiga kura wengi.
"



Ujumbe huu una migongano..............Inakuwaje Dr. Slaa awabebe madiwani lakini asimbembe Mbunge wakeeeeeeeeeeeee?

Aidha anawabeba wote au la hasha...........Nina wasiwasi taarifa hii yalenga kumpigia debe Dr. batildaaaaaaaaaaaa

Heshima kwako Rutashubanyuma,

Kwanza soma post #6 ya Mkuu crashwise.Naomba tujiulize kidogo tuache ushabiki mandazi.Lema alipata jukwaa zuri ambalo Bwana Lyimo wa TLP na Dr Batilda wa CCM wangelipata wangelitumia kuwaeleza wapiga kura watawafanyia nini lakini jukwaa hilo Lema kabahatika kulipata anashia kutoa utetezi na kuomba msamahaa.Wakuu tujaribu kuwaheshimu watanzania kidogo tunapiga kelele Muungwana kumnadi Mramba,Lowassa na Chenge kwakuwa tunajua wametufanyia nini lakini hatutaki kupiga kelele uoza wa Lema kisa anagombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA ?.Mwl Nyerere aliwahi kumpigia kura mgombea ubunge wa NCCR Mageuzi na kumwacha mgombea wa CCM kwakuwa alikuwa na kashfa ya kutoa rushwa.Namsoma sana Mwl Nyerere natamani angekuwa hai pengine huu upuuzi tunaouona sasa ungepata msemaji makini.

 
Bwana Godbless Lema ameendelea kuandamwa na kashfa ya kumnadi Diwani wa CCM Sombetini Bwana A Mawazo katika uchaguzi mdogo.Bwana Lema mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Arusha mjini amejikuta akishindwa kutoa majibu ya kuridhisha wapiga kura ni sababu zipi zilimfanya amfanyie kampeni Bwana A Mawazo mwana CCM na kumwacha mgombea udiwani wa CHADEMA,CUF na TLP ?.Ikumbukwe Bwana Mawazo alikuwa diwani wa TLP kabla ya kujiunga na CCM.

Mkutano wa Dr W Slaa Mbauda ulibakia kama karata pekee ya kumwokoa Lema dhidi ya kashfa ya kuuza ubunge mwaka 2005 na kumfanyia kampeni Mawazo lakini bado hakuweza kujitoa kwenye kashfa hizo na hata Dr Slaa ilielekea alikuwa akijua dhambi yake.Alimtaka awe makini kwani anaweza kumtosa ???????.



Wagombea udiwani wa CHADEMA wameonekana kuwa na nguvu zaidi ya mgombea ubunge hasa baada ya mkutano wa Dr W Slaa.Madiwani wa kata za Kimandulu,Elerai na Moshono wameendelea kuvutia wapiga kura wengi kuliko mwanzo,Bwana Lema amekuwa akitegemea kubebwa na madiwani wa kata hizo zaidi tofauti na mwanzo wa kampeni zake madiwani walikuwa wakimtegemea zaidi ili kuwafikia wapiga kura wengi.


CCM inafanya vizuri kata ya Kati ilipo ngome kuu ya Mama batilda,mkutano wake maeneo ya St Thomas Hospital ulivutia watu wengi sana huku mgombea udiwani wa kata ya kati akiwa na uhakika wa kushinda kata hiyo.


TLP inaringia kata ya Sokoni 1,Sombetini,Lemara na Ungalimited.wapiga debe wa TLP wanatumia udhaifu wa Bwana Lema hasa kitendo chake cha kumpigia debe mgombea wa CCM.

Lema kamchukuwa mawazo wake ..bado unapenda isoma hii habari tena au unatamani ifuta..?

Naona mzimu wa Sombetini unakurudia.
 
Mimi ni mwana cdm kitendo cha lema sio kibaya kama ameona anafaa mwacheni ampigie situnajenga nchi moja? au?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom