Abdalah Abdulrahman
JF-Expert Member
- Aug 29, 2019
- 222
- 201
Baadhi ya viongozi wa siasa huwatumia wananchi kama inavyotumika karatasi ya chooni (toilet paper) au mshumaa kwa malengo ya kuwasaidia kusafisha mabaya yao,kuwasafishia njia,kuwapa mwaga huku wakiwaacha wanachama wao wakiteketea.
Ninasema hivyo kwani ni Chadema iliyowadanganya wanachama wake wadeki na kutandika kanga barabarani ili wabunge na madiwani pamoja na mgombea wao wa uraisi apite kipindi cha uchaguzi,baada ya uchaguzi manufaa yote waliyopata ya ongezeko la ruzuku,mfuko wa jimbo,mafao,mikopo nakadhalika, hakuna hata kitu kimoja wanachama waliambulia,maeneo waliyoyaongoza viongozi hawa yamebakia hayana maendeleo kwa ubinafsi wao wa kuangalia maslahi yao na ya familia zao kwanza.Ni viongozi wa Chadema waliowashawishi wanachama wao waandamane na kuwapiga mawe polisi,waliokamatwa hakuna hata kiongozi mmoja wa chama alieenda kuwatembela na kuangalia familia zao.
Mifano hii na mingine inaturejesha katika kisa hiki cha uchungu cha kupotea kwa maisha ya ndugu yetu Aquilina katika vurugu zilizoanzishwa na wafuasi wa Chadema. Baada ya kufariki kwa binti Aquilina,serikali ilichukua jukumu la kuusitiri mwili wa marehemu na kuwafariji wazazi na walezi wa Aquilina.Hakuna kiongozi yeyete wa Chadema ambaye aliwahi kufika katika familia ya marehemu na hakuna pesa au mchango wowote aliyowahi kupelekwa kwenye familia ya marehemu.Michango iliyochangwa kwa ajili ya zoezi hili iliishia kwa viongozi wachache ndani ya Chama.
Bado haifahamiki kuwa ni waandamanaji wa Chadema walimuua binti huyu pale walipokuwa wakiwarushia mawe polisi,risasi iliyotoka kwa mwandamanaji mwenye silaha au ni risasi iliyotoka kwa polisi ndio ilimuua binti huyu.Ukweli utafahamika tu,lakini tufahamu kuwa nafsi yeyote inayouliwa kwa dhuluma haiondoki bila kuacha athari kwa wale walioidhulumu.Hivyo basi mzimu wa kifo cha Aqulina pamoja na utekaji wa wanachama ndani ya Chadema unaolenga kujinufaisha kwa watu wachache kisiasa utaendelea kuwasumbua viongozi wa Chadema mpaka watakapotubu juu ya dhambi hii na zingine wanazowafanyia Watanzania.Hii inadhihirika katika hoja zifuatazo:-
1. Kushindwa kwenye chaguzi za marudio na za serikali za mitaa
Chadema imeendelea kudhoofika kama sio kufa katika maeneo ya mijini ambapo ilikuwa na nguvu kupitia UKAWA,hii inadhhirika kutokana na matokeo ya chaguzi za marudio katika maeneo mbalimbali ambazo wananchi wamechagua viongozi wa Chama cha Mapinduzi(CCM) kwa zaidi ya asilimia 90% .Chadema pia imeendela kupoteza mvuto kwa wanachama wake wachache kwa kitendo cha kususia uchaguzi wa serikali za mitaa.Wanachama wameingiwa na wasiwasi na kupelekea kutojiandikisha na wale wengi waliojiandikisha kuazimia kutorudia tena makosa ya kuwachagua viongozi ambao ni wabinafsi wasio na uzalendo na nchi yao.
2. Zomea zomea ya Viongozi wa Chadema
Haikuwahi kutokea mpasuko uliopelekea wanachama kuzomea viongozi wao ndani ya chama,hasa kiongozi mkubwa kama Mwenyekiti wa chama.Hii inaendelea kudhibitisha mzimu wa Aquilini unawatafuna viongozi kutokana na zomea zomea zinazoendelea katika mikutano ya Chadema.Ni hivi karibuni tu Mh Freeman Mboe alizomewa na wanachama wake katika jimbo lake huko Hai wakimtaka aeleze alichowafanyia wananchi katika kipindi cha miaka 5 ya uongozi wake,na baada ya kushindwa kueleza akahairisha mkutano.
3. Mkosi ya kunusurika kufungwa
Ilibakia alimanusra viongozi wote wa Chadema kwenda jela kutokana na kutiwa hatiani kwa jinai waliyoifanya.Chadema ilitumia tukio hili kujinufaisha na kutenda makosa mengine kama kutakatisha fedha nakadhalika.Tukio hili limeacha dowa kuwa kwani mchakato mzima wa ukusanyaji wa pesa hizi uligubikwa na usiri mkubwa wenye nia ovu ya kupiga hela na kutakatisha pesa chafu.
4. Mkosi inayopelekea kuvunjika viungo
Baada ya wanachama wa chadema kufanyafujo ndani ya Gereza kwa kutaka Mwenyekiti kutolewa bila kufuata utaratibu huku wakimiminia askari magereza matusi kama walivyo wamiminia askari polisi siku ya hukumu ya kesi ya viongozi wa chadema,ilitokea sintofahamu ambyo ilisababisha kuumia kwa viongozi hawa wa chma.Baadhi ya watu waliokuwepo katika eneo la tukio wanasema Halima mdee pamoja na Ester Bulaya waliangukiwa na kundi la wanachama waliokuwa wakiwakimbia askari magereza.
5. Kukusanya wanachama wao ili wawauwe kwa Korona
Mwenyekiti wa Chadema Mh Freeman Mboe anawahadaa wanachama wake kukusanyika licha ya kuwepo kwa ugonjwa wa Korona amabo unapinga mikusanyiko.Lengo kuu ni kuleta taharuki ya maambukizi mapya kwa Watanzania ili waweze kukusanya michango ya misiba kwa ajili ya kampeni za mwaka huu.
Chadema kama chama kinatakiwa kujitahmini juu ya kutumia damu za watu kufikia malengo yao ya kisiasa.Seriakali inatakiwa kuhakikisha kila jambo wanalofanya Chadema lina mustakabali mwema na nchi,sivyo kutumia kila rasilimali iliyopo kulizuia kwa manufaa ya nchi
Mungu ibariki Tanzania
Ninasema hivyo kwani ni Chadema iliyowadanganya wanachama wake wadeki na kutandika kanga barabarani ili wabunge na madiwani pamoja na mgombea wao wa uraisi apite kipindi cha uchaguzi,baada ya uchaguzi manufaa yote waliyopata ya ongezeko la ruzuku,mfuko wa jimbo,mafao,mikopo nakadhalika, hakuna hata kitu kimoja wanachama waliambulia,maeneo waliyoyaongoza viongozi hawa yamebakia hayana maendeleo kwa ubinafsi wao wa kuangalia maslahi yao na ya familia zao kwanza.Ni viongozi wa Chadema waliowashawishi wanachama wao waandamane na kuwapiga mawe polisi,waliokamatwa hakuna hata kiongozi mmoja wa chama alieenda kuwatembela na kuangalia familia zao.
Mifano hii na mingine inaturejesha katika kisa hiki cha uchungu cha kupotea kwa maisha ya ndugu yetu Aquilina katika vurugu zilizoanzishwa na wafuasi wa Chadema. Baada ya kufariki kwa binti Aquilina,serikali ilichukua jukumu la kuusitiri mwili wa marehemu na kuwafariji wazazi na walezi wa Aquilina.Hakuna kiongozi yeyete wa Chadema ambaye aliwahi kufika katika familia ya marehemu na hakuna pesa au mchango wowote aliyowahi kupelekwa kwenye familia ya marehemu.Michango iliyochangwa kwa ajili ya zoezi hili iliishia kwa viongozi wachache ndani ya Chama.
Bado haifahamiki kuwa ni waandamanaji wa Chadema walimuua binti huyu pale walipokuwa wakiwarushia mawe polisi,risasi iliyotoka kwa mwandamanaji mwenye silaha au ni risasi iliyotoka kwa polisi ndio ilimuua binti huyu.Ukweli utafahamika tu,lakini tufahamu kuwa nafsi yeyote inayouliwa kwa dhuluma haiondoki bila kuacha athari kwa wale walioidhulumu.Hivyo basi mzimu wa kifo cha Aqulina pamoja na utekaji wa wanachama ndani ya Chadema unaolenga kujinufaisha kwa watu wachache kisiasa utaendelea kuwasumbua viongozi wa Chadema mpaka watakapotubu juu ya dhambi hii na zingine wanazowafanyia Watanzania.Hii inadhihirika katika hoja zifuatazo:-
1. Kushindwa kwenye chaguzi za marudio na za serikali za mitaa
Chadema imeendelea kudhoofika kama sio kufa katika maeneo ya mijini ambapo ilikuwa na nguvu kupitia UKAWA,hii inadhhirika kutokana na matokeo ya chaguzi za marudio katika maeneo mbalimbali ambazo wananchi wamechagua viongozi wa Chama cha Mapinduzi(CCM) kwa zaidi ya asilimia 90% .Chadema pia imeendela kupoteza mvuto kwa wanachama wake wachache kwa kitendo cha kususia uchaguzi wa serikali za mitaa.Wanachama wameingiwa na wasiwasi na kupelekea kutojiandikisha na wale wengi waliojiandikisha kuazimia kutorudia tena makosa ya kuwachagua viongozi ambao ni wabinafsi wasio na uzalendo na nchi yao.
2. Zomea zomea ya Viongozi wa Chadema
Haikuwahi kutokea mpasuko uliopelekea wanachama kuzomea viongozi wao ndani ya chama,hasa kiongozi mkubwa kama Mwenyekiti wa chama.Hii inaendelea kudhibitisha mzimu wa Aquilini unawatafuna viongozi kutokana na zomea zomea zinazoendelea katika mikutano ya Chadema.Ni hivi karibuni tu Mh Freeman Mboe alizomewa na wanachama wake katika jimbo lake huko Hai wakimtaka aeleze alichowafanyia wananchi katika kipindi cha miaka 5 ya uongozi wake,na baada ya kushindwa kueleza akahairisha mkutano.
3. Mkosi ya kunusurika kufungwa
Ilibakia alimanusra viongozi wote wa Chadema kwenda jela kutokana na kutiwa hatiani kwa jinai waliyoifanya.Chadema ilitumia tukio hili kujinufaisha na kutenda makosa mengine kama kutakatisha fedha nakadhalika.Tukio hili limeacha dowa kuwa kwani mchakato mzima wa ukusanyaji wa pesa hizi uligubikwa na usiri mkubwa wenye nia ovu ya kupiga hela na kutakatisha pesa chafu.
4. Mkosi inayopelekea kuvunjika viungo
Baada ya wanachama wa chadema kufanyafujo ndani ya Gereza kwa kutaka Mwenyekiti kutolewa bila kufuata utaratibu huku wakimiminia askari magereza matusi kama walivyo wamiminia askari polisi siku ya hukumu ya kesi ya viongozi wa chadema,ilitokea sintofahamu ambyo ilisababisha kuumia kwa viongozi hawa wa chma.Baadhi ya watu waliokuwepo katika eneo la tukio wanasema Halima mdee pamoja na Ester Bulaya waliangukiwa na kundi la wanachama waliokuwa wakiwakimbia askari magereza.
5. Kukusanya wanachama wao ili wawauwe kwa Korona
Mwenyekiti wa Chadema Mh Freeman Mboe anawahadaa wanachama wake kukusanyika licha ya kuwepo kwa ugonjwa wa Korona amabo unapinga mikusanyiko.Lengo kuu ni kuleta taharuki ya maambukizi mapya kwa Watanzania ili waweze kukusanya michango ya misiba kwa ajili ya kampeni za mwaka huu.
Chadema kama chama kinatakiwa kujitahmini juu ya kutumia damu za watu kufikia malengo yao ya kisiasa.Seriakali inatakiwa kuhakikisha kila jambo wanalofanya Chadema lina mustakabali mwema na nchi,sivyo kutumia kila rasilimali iliyopo kulizuia kwa manufaa ya nchi
Mungu ibariki Tanzania